Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mathayo 27
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Mathayo—Yaliyomo

      • Yesu akabidhiwa kwa Pilato (1, 2)

      • Yuda ajinyonga (3-10)

      • Yesu mbele ya Pilato (11-26)

      • Adhihakiwa hadharani (27-31)

      • Atundikwa kwenye mti huko Golgotha (32-44)

      • Yesu afa (45-56)

      • Yesu azikwa (57-61)

      • Kaburi lawekewa ulinzi mkali (62-66)

Mathayo 27:1

Marejeo

  • +Mk 15:1; Lu 22:66

Mathayo 27:2

Marejeo

  • +Zb 2:2; Mt 20:18, 19; Lu 23:1; Yoh 18:28; Mdo 3:13

Mathayo 27:3

Marejeo

  • +Mt 26:14, 15; Mk 14:10, 11

Mathayo 27:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Utajua utakachofanya.”

Mathayo 27:5

Marejeo

  • +Mdo 1:16, 18

Mathayo 27:8

Marejeo

  • +Mdo 1:19

Mathayo 27:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Nyongeza A5.

Marejeo

  • +Zek 11:12, 13

Mathayo 27:11

Marejeo

  • +Mk 15:2-5; Lu 23:3; Yoh 18:33, 37

Mathayo 27:12

Marejeo

  • +Isa 53:7; Mt 26:63; Yoh 19:9

Mathayo 27:15

Marejeo

  • +Mk 15:6-10; Yoh 18:39

Mathayo 27:20

Marejeo

  • +Lu 23:18; Yoh 18:40; Mdo 3:14
  • +Mk 15:11-14

Mathayo 27:22

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Auawe kwenye mti!”

Marejeo

  • +Lu 23:21

Mathayo 27:23

Marejeo

  • +Lu 23:23; Mdo 3:13

Mathayo 27:25

Marejeo

  • +Mdo 5:27, 28; 1Th 2:14, 15

Mathayo 27:26

Marejeo

  • +Lu 18:33; Yoh 19:1
  • +Mk 15:15; Lu 23:25

Mathayo 27:27

Marejeo

  • +Mk 15:16-20

Mathayo 27:28

Marejeo

  • +Yoh 19:2, 3

Mathayo 27:29

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Usifiwe.”

Mathayo 27:30

Marejeo

  • +Isa 50:6; Mt 26:67

Mathayo 27:31

Marejeo

  • +Isa 53:7; Mt 20:18, 19

Mathayo 27:32

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Kamusi.

Marejeo

  • +Mk 15:21; Lu 23:26

Mathayo 27:33

Marejeo

  • +Mk 15:22-24; Lu 23:33; Yoh 19:17

Mathayo 27:34

Maelezo ya Chini

  • *

    Kinywaji kichungu.

Marejeo

  • +Zb 69:21

Mathayo 27:35

Marejeo

  • +Zb 22:18; Mk 15:24; Lu 23:34; Yoh 19:23, 24

Mathayo 27:37

Marejeo

  • +Mk 15:26; Lu 23:38; Yoh 19:19

Mathayo 27:38

Marejeo

  • +Isa 53:12; Mk 15:27; Lu 23:33; Yoh 19:18

Mathayo 27:39

Marejeo

  • +Lu 18:32; Ebr 12:3
  • +Zb 22:7; 109:25

Mathayo 27:40

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Kamusi.

Marejeo

  • +Mt 26:60, 61; Yoh 2:19
  • +Mk 15:29-32

Mathayo 27:41

Marejeo

  • +Lu 23:35

Mathayo 27:42

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Kamusi.

Marejeo

  • +Yoh 1:49; 12:13

Mathayo 27:43

Marejeo

  • +Zb 22:8
  • +Mk 14:62; Yoh 5:18; 10:36

Mathayo 27:44

Marejeo

  • +Lu 23:39

Mathayo 27:45

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, karibu saa 6 mchana.

  • *

    Yaani, karibu saa 9 alasiri.

Marejeo

  • +Mk 15:33; Lu 23:44

Mathayo 27:46

Marejeo

  • +Zb 22:1; Isa 53:10; Mk 15:34

Mathayo 27:47

Marejeo

  • +Mk 15:35, 36

Mathayo 27:48

Marejeo

  • +Zb 69:21; Lu 23:36; Yoh 19:29

Mathayo 27:50

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “akaitoa roho yake.” Au “akakata pumzi.”

Marejeo

  • +Mk 15:37; Lu 23:46; Yoh 19:30

Mathayo 27:51

Marejeo

  • +Kut 26:31-33; Ebr 9:3
  • +Ebr 10:19, 20
  • +Mk 15:38; Lu 23:45

Mathayo 27:52

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “makaburi ya ukumbusho.”

Mathayo 27:54

Marejeo

  • +Mk 15:39

Mathayo 27:55

Marejeo

  • +Mk 15:40, 41; Lu 8:2, 3

Mathayo 27:56

Marejeo

  • +Mt 20:20; Yoh 19:25

Mathayo 27:57

Marejeo

  • +Mk 15:42, 43; Lu 23:50-53

Mathayo 27:58

Marejeo

  • +Kum 21:22, 23
  • +Mk 15:45-47; Yoh 19:38

Mathayo 27:59

Marejeo

  • +Yoh 19:40, 41

Mathayo 27:60

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kaburi lake jipya la ukumbusho.”

  • *

    Au “kaburi la ukumbusho.”

Marejeo

  • +Isa 53:9

Mathayo 27:61

Marejeo

  • +Lu 23:55

Mathayo 27:62

Marejeo

  • +Mk 15:42; Lu 23:54; Yoh 19:14

Mathayo 27:63

Marejeo

  • +Mt 12:40; Yoh 2:19

Mathayo 27:64

Marejeo

  • +Mt 28:12, 13

Jumla

Mt. 27:1Mk 15:1; Lu 22:66
Mt. 27:2Zb 2:2; Mt 20:18, 19; Lu 23:1; Yoh 18:28; Mdo 3:13
Mt. 27:3Mt 26:14, 15; Mk 14:10, 11
Mt. 27:5Mdo 1:16, 18
Mt. 27:8Mdo 1:19
Mt. 27:10Zek 11:12, 13
Mt. 27:11Mk 15:2-5; Lu 23:3; Yoh 18:33, 37
Mt. 27:12Isa 53:7; Mt 26:63; Yoh 19:9
Mt. 27:15Mk 15:6-10; Yoh 18:39
Mt. 27:20Lu 23:18; Yoh 18:40; Mdo 3:14
Mt. 27:20Mk 15:11-14
Mt. 27:22Lu 23:21
Mt. 27:23Lu 23:23; Mdo 3:13
Mt. 27:25Mdo 5:27, 28; 1Th 2:14, 15
Mt. 27:26Lu 18:33; Yoh 19:1
Mt. 27:26Mk 15:15; Lu 23:25
Mt. 27:27Mk 15:16-20
Mt. 27:28Yoh 19:2, 3
Mt. 27:30Isa 50:6; Mt 26:67
Mt. 27:31Isa 53:7; Mt 20:18, 19
Mt. 27:32Mk 15:21; Lu 23:26
Mt. 27:33Mk 15:22-24; Lu 23:33; Yoh 19:17
Mt. 27:34Zb 69:21
Mt. 27:35Zb 22:18; Mk 15:24; Lu 23:34; Yoh 19:23, 24
Mt. 27:37Mk 15:26; Lu 23:38; Yoh 19:19
Mt. 27:38Isa 53:12; Mk 15:27; Lu 23:33; Yoh 19:18
Mt. 27:39Lu 18:32; Ebr 12:3
Mt. 27:39Zb 22:7; 109:25
Mt. 27:40Mt 26:60, 61; Yoh 2:19
Mt. 27:40Mk 15:29-32
Mt. 27:41Lu 23:35
Mt. 27:42Yoh 1:49; 12:13
Mt. 27:43Zb 22:8
Mt. 27:43Mk 14:62; Yoh 5:18; 10:36
Mt. 27:44Lu 23:39
Mt. 27:45Mk 15:33; Lu 23:44
Mt. 27:46Zb 22:1; Isa 53:10; Mk 15:34
Mt. 27:47Mk 15:35, 36
Mt. 27:48Zb 69:21; Lu 23:36; Yoh 19:29
Mt. 27:50Mk 15:37; Lu 23:46; Yoh 19:30
Mt. 27:51Kut 26:31-33; Ebr 9:3
Mt. 27:51Ebr 10:19, 20
Mt. 27:51Mk 15:38; Lu 23:45
Mt. 27:54Mk 15:39
Mt. 27:55Mk 15:40, 41; Lu 8:2, 3
Mt. 27:56Mt 20:20; Yoh 19:25
Mt. 27:57Mk 15:42, 43; Lu 23:50-53
Mt. 27:58Kum 21:22, 23
Mt. 27:58Mk 15:45-47; Yoh 19:38
Mt. 27:59Yoh 19:40, 41
Mt. 27:60Isa 53:9
Mt. 27:61Lu 23:55
Mt. 27:62Mk 15:42; Lu 23:54; Yoh 19:14
Mt. 27:63Mt 12:40; Yoh 2:19
Mt. 27:64Mt 28:12, 13
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
  • 33
  • 34
  • 35
  • 36
  • 37
  • 38
  • 39
  • 40
  • 41
  • 42
  • 43
  • 44
  • 45
  • 46
  • 47
  • 48
  • 49
  • 50
  • 51
  • 52
  • 53
  • 54
  • 55
  • 56
  • 57
  • 58
  • 59
  • 60
  • 61
  • 62
  • 63
  • 64
  • 65
  • 66
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Mathayo 27:1-66

Kulingana na Mathayo

27 Ilipofika asubuhi, wakuu wote wa makuhani na wazee wa watu wakashauriana pamoja kumhusu Yesu ili auawe.+ 2 Baada ya kumfunga, wakampeleka na kumkabidhi kwa Pilato, gavana.+

3 Ndipo Yuda, ambaye alimsaliti, alipoona Yesu amehukumiwa, akajuta na kuwarudishia wakuu wa makuhani na wazee vile vipande 30 vya fedha,+ 4 akisema: “Nilitenda dhambi niliposaliti damu isiyo na hatia.” Wakamwambia: “Hilo linatuhusuje? Shauri yako!”* 5 Basi akavitupa vile vipande vya fedha hekaluni. Kisha akaenda zake akajinyonga.+ 6 Lakini wakuu wa makuhani wakachukua pesa hizo wakasema: “Si halali kuziweka katika hazina takatifu, kwa sababu ni bei ya damu.” 7 Baada ya kushauriana, wakatumia pesa hizo kununua shamba la mfinyanzi liwe mahali pa kuzika wageni. 8 Kwa hiyo, shamba hilo limeitwa Shamba la Damu+ hadi leo hii. 9 Ndipo yakatimia maneno haya yaliyosemwa kupitia nabii Yeremia: “Nao wakavichukua vile vipande 30 vya fedha, bei iliyoamuliwa juu ya mtu huyo, ambaye bei yake iliamuliwa na baadhi ya wana wa Israeli, 10 nao wakavitoa ili kununua shamba la mfinyanzi, kama Yehova* alivyoniamuru.”+

11 Sasa Yesu akasimama mbele ya gavana, naye gavana akamuuliza: “Je, wewe ndiye Mfalme wa Wayahudi?” Yesu akajibu: “Wewe mwenyewe umesema.”+ 12 Lakini alipokuwa akishtakiwa na wakuu wa makuhani na wazee, hakujibu.+ 13 Ndipo Pilato akamwambia: “Je, husikii ni mambo mangapi wanayoshuhudia dhidi yako?” 14 Lakini hakumjibu hata neno moja, hivi kwamba gavana akashangaa sana.

15 Sasa kila sherehe ya pasaka, gavana alikuwa na desturi ya kumfungua mfungwa yeyote ambaye umati ulimtaka.+ 16 Wakati huo walikuwa wamemkamata mhalifu sugu aitwaye Baraba. 17 Basi walipokuwa wamekusanyika, Pilato akawauliza: “Mnataka niwafungulie nani, Baraba au Yesu anayeitwa Kristo?” 18 Kwa maana Pilato alijua kwamba walikuwa wamemkabidhi Yesu kwake kwa sababu ya wivu. 19 Zaidi ya hayo, alipokuwa ameketi kwenye kiti cha hukumu, mke wake akampelekea ujumbe huu: “Mwache mtu huyo mwadilifu, kwa maana niliteseka sana leo katika ndoto kwa sababu yake.” 20 Lakini wakuu wa makuhani na wazee wakaushawishi umati uombe Baraba afunguliwe,+ lakini Yesu auawe.+ 21 Gavana akawauliza: “Mnataka niwafungulie nani kati ya hawa wawili?” Wakasema: “Baraba.” 22 Pilato akawaambia: “Basi, nifanye nini na Yesu anayeitwa Kristo?” Wote wakasema: “Atundikwe mtini!”*+ 23 Akawauliza: “Kwa nini? Amefanya kosa gani?” Wakaendelea kusema kwa sauti kubwa hata zaidi: “Atundikwe mtini!”+

24 Pilato alipoona jitihada zake hazifaulu, na badala yake ghasia zilikuwa zikitokea, akachukua maji akanawa mikono mbele ya umati, akisema: “Mimi sina hatia ya damu ya mtu huyu. Shauri yenu.” 25 Ndipo watu wote wakajibu: “Damu yake na iwe juu yetu na juu ya watoto wetu.”+ 26 Ndipo akawafungulia Baraba, lakini akaagiza Yesu apigwe mijeledi+ na kumtoa ili auawe kwenye mti.+

27 Ndipo wanajeshi wa gavana wakampeleka Yesu katika makao ya gavana, wakakusanya kikosi chote cha wanajeshi kumzunguka.+ 28 Wakamvua kanzu yake na kumvisha joho jekundu,+ 29 kisha wakasokota taji la miiba na kumvisha kichwani na kutia utete kwenye mkono wake wa kuume. Wakampigia magoti, wakamdhihaki wakisema: “Salamu,* ewe Mfalme wa Wayahudi!” 30 Wakamtemea mate+ na kuuchukua ule utete, wakaanza kumpiga kichwani. 31 Mwishowe, baada ya kumdhihaki, wakamvua lile joho wakamvisha mavazi yake ya nje, wakampeleka akatundikwe mtini.+

32 Walipokuwa wakitoka wakakutana na mwanamume kutoka Kirene aitwaye Simoni. Wakamlazimisha aubebe mti wa mateso*+ wa Yesu. 33 Na walipofika mahali panapoitwa Golgotha, yaani, Mahali pa Fuvu la Kichwa,+ 34 wakampa divai iliyochanganywa na nyongo* anywe;+ lakini alipoionja, akakataa kuinywa. 35 Baada ya kumtundika kwenye mti, wakagawana mavazi yake ya nje kwa kupiga kura,+ 36 kisha wakaketi hapo wakimlinda. 37 Pia, wakabandika juu ya kichwa chake mashtaka dhidi yake, yalikuwa yameandikwa: “Huyu ni Yesu Mfalme wa Wayahudi.”+

38 Ndipo wezi wawili wakatundikwa kwenye mti kando yake, mmoja upande wake wa kuume na mwingine upande wake wa kushoto.+ 39 Na wale waliokuwa wakipita hapo wakamtukana,+ huku wakitikisa vichwa vyao+ 40 wakisema: “Wewe uliyetaka kuliangusha chini hekalu na kulijenga kwa siku tatu,+ jiokoe mwenyewe! Ikiwa wewe ni mwana wa Mungu, shuka kutoka kwenye mti wa mateso!”*+ 41 Vivyo hivyo, wakuu wa makuhani, waandishi, na wazee wakaanza kumdhihaki wakisema:+ 42 “Aliwaokoa wengine lakini hawezi kujiokoa mwenyewe! Yeye ni Mfalme wa Israeli;+ acheni sasa ashuke kutoka kwenye mti wa mateso* nasi tutamwamini. 43 Amemtegemea Mungu; acheni Mungu amwokoe ikiwa anamtaka,+ kwa maana alisema, ‘Mimi ni Mwana wa Mungu.’”+ 44 Vivyo hivyo, hata wezi waliotundikwa mtini kando yake walikuwa wakimshutumu.+

45 Kukawa na giza katika nchi yote kuanzia saa sita* mpaka saa tisa.*+ 46 Karibu saa tisa, Yesu akapaza sauti, akisema: “Eli, Eli, lama sabakthani?” yaani, “Mungu wangu, Mungu wangu, kwa nini umeniacha?”+ 47 Waliposikia hilo, baadhi ya wale waliokuwa wamesimama hapo wakaanza kusema: “Mtu huyu anamwita Eliya.”+ 48 Mara moja, mmoja wao akakimbia, akachukua sifongo akailowesha katika divai kali akaiweka kwenye utete akampa anywe.+ 49 Lakini wengine wakasema: “Mwacheni! Acheni tuone kama Eliya atakuja kumwokoa.” 50 Yesu akapaza tena sauti kisha akafa.*+

51 Na tazama! pazia la patakatifu+ likapasuka vipande viwili,+ kuanzia juu mpaka chini,+ dunia ikatetemeka, na miamba ikapasuka. 52 Makaburi* yakafunguka na miili mingi ya watakatifu waliokuwa wamelala usingizi ikainuliwa 53 (na watu waliokuwa wakitoka makaburini baada ya kufufuliwa kwake wakaingia katika jiji takatifu), nayo ikaonwa na watu wengi. 54 Lakini yule ofisa wa jeshi na wale waliokuwa pamoja naye wakimlinda Yesu walipoona tetemeko la ardhi na mambo yaliyokuwa yakitokea, wakaogopa sana na kusema: “Hakika huyu alikuwa Mwana wa Mungu.”+

55 Na wanawake wengi ambao walikuwa wamemfuata Yesu kutoka Galilaya ili kumhudumia walikuwa wakitazama kwa mbali;+ 56 miongoni mwao kulikuwa na Maria Magdalene, Maria mama ya Yakobo na Yose, na pia mama ya wana wa Zebedayo.+

57 Sasa kwa kuwa ilikuwa jioni, akaja tajiri mmoja wa Arimathea, aitwaye Yosefu, ambaye pia alikuwa mwanafunzi wa Yesu.+ 58 Mtu huyu alienda kwa Pilato akaomba apewe mwili wa Yesu.+ Naye Pilato akaamuru apewe.+ 59 Yosefu akauchukua mwili huo, akaufunga kwa kitani bora kilicho safi,+ 60 akaulaza katika kaburi lake jipya,*+ alilokuwa amechimba katika mwamba. Kisha akaviringisha jiwe kubwa kwenye mwingilio wa lile kaburi,* akaondoka. 61 Lakini Maria Magdalene na yule Maria mwingine wakabaki hapo, wakiwa wameketi mbele ya kaburi.+

62 Siku iliyofuata, baada ya Matayarisho,+ wakuu wa makuhani na Mafarisayo wakakusanyika mbele ya Pilato, 63 wakisema: “Bwana, tumekumbuka mjanja huyo alipokuwa hai alisema, ‘Nitafufuliwa baada ya siku tatu.’+ 64 Kwa hiyo, amuru kaburi lilindwe mpaka siku ya tatu, ili wanafunzi wake wasije wakamwiba+ na kuwaambia watu, ‘Alifufuliwa kutoka kwa wafu!’ Kisha udanganyifu huu wa mwisho utakuwa mbaya zaidi kuliko ule wa kwanza.” 65 Pilato akawaambia: “Mnaweza kuweka walinzi. Nendeni mkalilinde jinsi mnavyotaka.” 66 Basi wakaenda na kulilinda kaburi kwa kulitia jiwe muhuri na kuweka walinzi.

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki