Methali
8 Je, hekima haipazi sauti?
Je, utambuzi hauinui sauti yake?+
2 Kwenye sehemu zilizoinuka+ pembeni mwa barabara,
Husimama kwenye makutano ya barabara.
3 Karibu na malango yanayoelekea jijini,
Kwenye njia zinazoelekea milangoni,
Huendelea kulia kwa sauti kubwa:+
4 “Ninawaita, enyi watu, ninawaita;
Ninampazia sauti kila mtu.*
6 Sikilizeni, kwa maana ninayosema ni muhimu,
Midomo yangu husema yaliyo sawa;
7 Kwa maana kinywa changu husema ukweli kwa sauti ya chini,
Na midomo yangu huchukia jambo ovu.
8 Maneno yote ya kinywa changu ni ya uadilifu.
Hakuna neno hata moja lililopinda wala kupotoka.
9 Yote yako wazi kabisa kwa mtu mwenye utambuzi
Nayo ni sawa kwa wale ambao wamepata ujuzi.
10 Chukueni nidhamu yangu badala ya fedha,
Na ujuzi badala ya dhahabu bora zaidi,+
11 Kwa maana hekima ni bora kuliko marijani;*
Vitu vingine vyote vinavyotamanika haviwezi kulinganishwa nayo.
12 Mimi, hekima, ninakaa pamoja na werevu;
Nimepata ujuzi na uwezo wa kufikiri.+
13 Kumwogopa Yehova humaanisha kuchukia uovu.+
Ninachukia kujikweza na kiburi+ na njia ya uovu na maneno mapotovu.+
15 Kwa msaada wangu wafalme huendelea kutawala,
Na maofisa wakuu hutunga sheria za uadilifu.+
16 Kwa msaada wangu wakuu huendelea kutawala,
Na viongozi huhukumu kwa uadilifu.
17 Ninawapenda wale wanaonipenda,
Na wale wanaonitafuta watanipata.+
18 Nina utajiri na utukufu,
Mali inayodumu* na uadilifu.
19 Tunda langu ni bora kuliko dhahabu, hata kuliko dhahabu safi,
Na mazao yangu ni bora kuliko fedha bora kabisa.+
20 Mimi hutembea katika kijia cha uadilifu,
Katikati ya vijia vya haki;
21 Mimi huwapa urithi mwingi wale wanaonipenda,
Nami huyajaza maghala yao.
24 Wakati ambapo hakukuwa na vilindi vya maji,+ nilizaliwa,*
Wakati ambapo hakukuwa na chemchemi zilizofurika maji.
25 Kabla milima haijawekwa mahali pake,
Kabla ya vilima, nilizaliwa,
26 Wakati ambapo hakuwa ameiumba dunia na mashamba yake
Wala mabonge ya kwanza ya udongo.
27 Alipozitayarisha mbingu,+ nilikuwepo;
Alipouweka upeo* juu ya maji,+
28 Alipoyafanya imara mawingu yaliyo juu,
Alipojenga msingi wa chemchemi za vilindini,
29 Alipoiwekea bahari sheria
Kwamba maji yake yasipite agizo lake,+
Alipoiweka* misingi ya dunia,
30 Wakati huo nilikuwa kando yake nikiwa mfanyakazi stadi.+
Mimi ndiye aliyenipenda sana+ siku baada ya siku;
Nilishangilia mbele zake wakati wote;+
31 Nilishangilia dunia yake inayokaliwa,
Nami niliwapenda sana wanadamu.
32 Na sasa, wanangu, nisikilizeni;
Naam, wenye furaha ni wale wanaoshika njia zangu.
33 Sikilizeni nidhamu+ muwe na hekima,
Msiipuuze kamwe.