Zaburi
Muziki wa Asafu.+
79 Ee Mungu, mataifa yamevamia urithi wako;+
Yamelichafua hekalu lako takatifu;+
Yamebadili Yerusalemu kuwa rundo la magofu.+
2 Wamewapa ndege wa angani maiti za watumishi wako kuwa chakula chao
Na miili ya washikamanifu wako wamewapa wanyama wa mwituni wa dunia.+
3 Wamemwaga damu yao kama maji kotekote Yerusalemu,
Na hakuna aliyebaki wa kuwazika.+
4 Tumekuwa kitu cha kushutumiwa na majirani wetu;+
Wale wanaotuzunguka wanatudhihaki na kutufanyia mzaha.
5 Ee Yehova, utaendelea kuwaka hasira mpaka lini? Milele?+
Ghadhabu yako itaendelea kuwaka kama moto mpaka lini?+
6 Yamwagie ghadhabu yako mataifa ambayo hayakujui
Na falme ambazo haziliitii jina lako.+
7 Kwa maana wamemnyafua Yakobo
Nao wameifanya nchi yake ukiwa.+
8 Usitufanye tuwajibike kwa sababu ya makosa ya mababu zetu.+
Tuonyeshe haraka rehema yako,+
Kwa maana tumeshushwa chini sana.
9 Tusaidie, Ee Mungu wa wokovu wetu,+
Kwa ajili ya jina lako tukufu;
10 Kwa nini mataifa yaseme: “Mungu wao yuko wapi?”+
Na ijulikane miongoni mwa mataifa mbele ya macho yetu
Kwamba damu iliyomwagwa ya watumishi wako imelipiziwa kisasi.+
11 Na usikie kilio cha maumivu cha mfungwa.+
Tumia nguvu zako kuu* kuwahifadhi* wale waliohukumiwa kifo.*+