Zaburi
Wimbo wa Safari za Kupanda. Wa Daudi.
131 Ee Yehova, moyo wangu hauna kiburi,
Wala macho yangu hayana majivuno;+
Wala sijitafutii mambo makubwa sana,+
Wala mambo yanayopita uwezo wangu.
2 Hasha, badala yake nimeituliza na kuinyamazisha nafsi yangu*+
Kama mtoto aliyeachishwa kunyonya aliye na mama yake;
Nimeridhika kama mtoto aliyeachishwa kunyonya.
3 Watu wa Israeli na wamngojee Yehova+
Kuanzia sasa mpaka milele.