Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb 74
  • Yesu Anakuwa Masihi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yesu Anakuwa Masihi
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Yohana Anatayarisha Njia
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb 74
Baada ya Yesu kubatizwa na Yohana, roho ya Mungu ikishuka juu yake kama njiwa

SOMO LA 74

Yesu Anakuwa Masihi

Yohana alihubiri hivi: ‘Kuna mtu mwenye nguvu kuliko mimi anayekuja.’ Yesu alipokuwa na umri wa karibu miaka 30, alitoka Galilaya na kwenda kwenye Mto Yordani ambapo Yohana alikuwa akiwabatiza watu. Yesu alitaka Yohana ambatize, lakini Yohana akasema: ‘Sipaswi kukubatiza. Wewe ndiye unayepaswa kunibatiza.’ Yesu akamwambia Yohana hivi: ‘Yehova anataka wewe unibatize.’ Kwa hiyo, wakaingia ndani ya Mto Yordani, na Yohana akamzamisha Yesu ndani ya maji.

Baada ya Yesu kubatizwa, alisali. Wakati huohuo, mbingu zikafunguliwa, na roho ya Mungu ikashuka juu yake kama njiwa. Kisha Yehova akasema kutoka mbinguni: “Wewe ni Mwanangu, mpendwa; nimekukubali wewe.”

Roho ya Yehova iliposhuka juu ya Yesu, akawa Kristo, au Masihi. Sasa angeanza kufanya kazi ambayo Yehova alimtuma afanye duniani.

Mara tu baada ya ubatizo wake, Yesu akaingia nyikani na kukaa huko kwa siku 40. Aliporudi, akaenda kumwona Yohana. Yesu alipomkaribia, Yohana akasema: ‘Huyu ndiye Mwana-Kondoo wa Mungu ambaye huondolea mbali dhambi ya ulimwengu.’ Kwa kusema hivyo, Yohana alikuwa akiwajulisha kwamba Yesu ndiye Masihi. Je, unajua kilichompata Yesu alipokuwa nyikani? Acheni tuone.

“Sauti ikasikika kutoka mbinguni: ‘Wewe ni Mwanangu, mpendwa; nimekukubali.’”​—Marko 1:11

Maswali: Kwa nini Yesu alibatizwa? Kwa nini Yohana alisema kwamba Yesu alikuwa Mwana-Kondoo wa Mungu?

Mathayo 3:13-17; Marko 1:9-11; Luka 3:21-23; Yohana 1:29-34; Isaya 42:1; Waebrania 10:7-9

    Tanzanian sign language publications (2020-2025)
    Toka
    Ingia
    • Lugha ya Alama ya Tanzania
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki