Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
Tanzanian sign language publications (2020-2025)
Toka
Ingia
Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Leo

Jumamosi, Septemba 20

Mpendane.—Yoh. 13:34.

Hatuwezi kutii amri ya Yesu kuhusu kupendana ikiwa tunawaonyesha upendo baadhi ya watu kutanikoni na kuwabagua wengine. Ukweli ni kwamba huenda tukawa na uhusiano wa karibu zaidi na baadhi ya watu kama ilivyokuwa kwa Yesu. (Yoh. 13:23; 20:2) Lakini mtume Petro anatuonyesha kwamba tunapaswa kujitahidi kuonyesha “upendo wa kindugu”—uhusiano mchangamfu kama wa familia—kuwaelekea ndugu na dada zetu wote. (1 Pet. 2:17) Petro alituhimiza ‘tupendane sana kutoka moyoni.’ (1 Pet. 1:22) Katika muktadha huo, kupendana “sana” kunatia ndani kumpenda mtu hata kama ni vigumu kumwonyesha upendo. Namna gani ikiwa ndugu anatukasirisha au anatuumiza kwa njia fulani? Huenda tukashawishiwa kulipiza kisasi badala ya kuonyesha upendo. Ingawa hivyo, Petro alijifunza kutoka kwa Yesu kwamba Mungu hafurahishwi na watu wanaolipiza kisasi. (Yoh. 18:​10, 11) Petro aliandika hivi: “Msilipe ubaya kwa ubaya au matukano kwa matukano. Badala yake, lipeni kwa baraka.” (1 Pet. 3:9) Unapowaonyesha wengine upendo mwingi, utachochewa kuwatendea kwa fadhili na ufikirio. w23.09 41:9-11

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumapili, Septemba 21

Vilevile wanawake wanapaswa . . . wawe wenye kiasi katika mazoea, na waaminifu katika mambo yote.—1 Tim. 3:11

Tunastaajabishwa na jinsi mtoto anavyokua haraka na kuwa mtu mzima. Inaonekana ni kama watoto wanakua tu bila kufanya jitihada yoyote. Hata hivyo, jitihada inahitajika ili kuwa Mkristo mkomavu. (1 Kor. 13:11; Ebr. 6:1) Ili kufikia lengo hilo, tunahitaji kuwa na uhusiano wa karibu pamoja na Yehova. Pia, tunahitaji roho takatifu ili tusitawishe sifa zinazompendeza Yehova, tuwe na ustadi unaofaa, na tujitayarishe kwa ajili ya majukumu ya wakati ujao. (Met. 1:5) Yehova alimuumba mwanamume na mwanamke. (Mwa. 1:27) Ni wazi kwamba wanaume na wanawake wanatofautiana kimwili, lakini wanatofautiana kwa njia nyingine pia. Kwa mfano, Yehova aliwapatia wanaume na wanawake majukumu hususa, hivyo wanahitaji sifa na ustadi ili waweze kutimiza majukumu yao.—Mwa. 2:18. w23.12 52:1-2

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumatatu, Septemba 22

Fanyeni wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, mkiwabatiza katika jina la Baba na la Mwana.—Mt. 28:19.

Je, Yesu alitaka wengine watumie jina la kibinafsi la Baba yake? Bila shaka. Huenda baadhi ya viongozi wa dini wa siku za Yesu waliamini kwamba jina la Mungu lilikuwa takatifu sana hivi kwamba halikupaswa kutamkwa, lakini Yesu hakuruhusu desturi hizo zisizo za kimaandiko zimzuie kuliheshimu jina la Baba yake. Fikiria wakati ambapo Yesu alimponya mwanamume mwenye roho waovu katika eneo la Wagerasene. Watu katika eneo hilo waliogopa na kumsihi Yesu aondoke, hivyo hakubaki katika eneo hilo. (Marko 5:​16, 17) Lakini bado Yesu alitaka jina la Yehova lijulikane huko. Hivyo, alimwambia mwanamume aliyemponya awaambie watu mambo ambayo Yehova alikuwa amefanya, si mambo ambayo Yesu alikuwa amefanya. (Marko 5:19) Leo pia, anataka tufanye vivyo hivyo, yaani, tuwajulishe watu ulimwenguni pote kuhusu jina la Baba yake! (Mt. 24:14; 28:20) Tunapofanya sehemu yetu, tunamfurahisha Mfalme wetu, Yesu. w24.02 6:10

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki