Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 22
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Kutoka—Yaliyomo

      • Waisraeli wapewa sheria (1-31)

        • Kuhusu wizi (1-4)

        • Kuhusu kuharibu mazao (5, 6)

        • Kuhusu kulipia hasara na kumiliki mali (7-15)

        • Kuhusu kutongoza (16, 17)

        • Kuhusu ibada na kutenda haki katika jamii (18-31)

Kutoka 22:1

Marejeo

  • +2Sa 12:6; Lu 19:8

Kutoka 22:2

Marejeo

  • +Kut 20:15

Kutoka 22:7

Marejeo

  • +Kut 22:4

Kutoka 22:8

Marejeo

  • +Kum 16:18; 19:17

Kutoka 22:9

Marejeo

  • +Kum 16:18; 25:1
  • +Kut 22:4

Kutoka 22:11

Marejeo

  • +Law 6:2-5

Kutoka 22:16

Marejeo

  • +Kum 22:28, 29

Kutoka 22:18

Marejeo

  • +Law 19:26; 20:6; Kum 18:10-12; 1Sa 28:3; Gal 5:20; Ufu 22:15

Kutoka 22:19

Marejeo

  • +Law 18:23; 20:15; Kum 27:21

Kutoka 22:20

Marejeo

  • +Hes 25:3; 1Fa 18:40; 1Ko 10:20

Kutoka 22:21

Marejeo

  • +Law 25:35
  • +Law 19:33, 34; Kum 10:19

Kutoka 22:22

Marejeo

  • +Kum 27:19; Yak 1:27

Kutoka 22:23

Marejeo

  • +Zb 10:18; Yak 5:4

Kutoka 22:25

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “mla riba.”

Marejeo

  • +Law 25:35, 36; Kum 23:19; Lu 6:34, 35

Kutoka 22:26

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “rehani.”

Marejeo

  • +Kum 24:6

Kutoka 22:27

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “ngozi yake.”

  • *

    Au “neema.”

Marejeo

  • +Kum 24:13
  • +Kum 10:18; Zb 34:6

Kutoka 22:28

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “mtawala.”

Marejeo

  • +Law 24:11, 14
  • +Mhu 10:20; Mdo 23:5; Yud 8

Kutoka 22:29

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, mashinikizo ya mafuta na mashinikizo ya divai.

Marejeo

  • +Met 3:9; 2Ko 9:7
  • +Kut 13:2

Kutoka 22:30

Marejeo

  • +Kum 15:19
  • +Law 22:27

Kutoka 22:31

Marejeo

  • +Law 19:2; Hes 15:40; 1Pe 1:15
  • +Law 22:3, 8

Jumla

Kut. 22:12Sa 12:6; Lu 19:8
Kut. 22:2Kut 20:15
Kut. 22:7Kut 22:4
Kut. 22:8Kum 16:18; 19:17
Kut. 22:9Kum 16:18; 25:1
Kut. 22:9Kut 22:4
Kut. 22:11Law 6:2-5
Kut. 22:16Kum 22:28, 29
Kut. 22:18Law 19:26; 20:6; Kum 18:10-12; 1Sa 28:3; Gal 5:20; Ufu 22:15
Kut. 22:19Law 18:23; 20:15; Kum 27:21
Kut. 22:20Hes 25:3; 1Fa 18:40; 1Ko 10:20
Kut. 22:21Law 25:35
Kut. 22:21Law 19:33, 34; Kum 10:19
Kut. 22:22Kum 27:19; Yak 1:27
Kut. 22:23Zb 10:18; Yak 5:4
Kut. 22:25Law 25:35, 36; Kum 23:19; Lu 6:34, 35
Kut. 22:26Kum 24:6
Kut. 22:27Kum 24:13
Kut. 22:27Kum 10:18; Zb 34:6
Kut. 22:28Law 24:11, 14
Kut. 22:28Mhu 10:20; Mdo 23:5; Yud 8
Kut. 22:29Met 3:9; 2Ko 9:7
Kut. 22:29Kut 13:2
Kut. 22:30Kum 15:19
Kut. 22:30Law 22:27
Kut. 22:31Law 19:2; Hes 15:40; 1Pe 1:15
Kut. 22:31Law 22:3, 8
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Kutoka 22:1-31

Kutoka

22 “Mtu akiiba ng’ombe dume au kondoo na kumchinja au kumuuza, atalipa ng’ombe dume watano kwa ajili ya ng’ombe dume huyo na kondoo wanne kwa ajili ya kondoo huyo.+

2 (“Mwizi+ akipatikana akivunja nyumba kisha apigwe na kufa, aliyemuua hatakuwa na hatia ya damu. 3 Lakini jambo hilo likitokea baada ya jua kuchomoza, atakuwa na hatia ya damu.)

“Anapaswa kulipa. Ikiwa hana chochote, basi atauzwa ili kulipia vitu alivyoiba. 4 Kama mnyama aliyeibwa anapatikana akiwa hai mikononi mwake, awe ni ng’ombe dume au punda au kondoo, anapaswa kulipa mara mbili.

5 “Mtu yeyote akiwalisha wanyama wake katika shamba au shamba la mizabibu la mtu mwingine, atalipa kwa mazao bora ya shamba lake mwenyewe au mazao bora ya shamba lake mwenyewe la mizabibu.

6 “Moto ukiwaka na kuenea katika vichaka vya miiba na kuteketeza masuke au nafaka iliyo shambani au shamba, yule aliyewasha moto huo lazima alipie kilichoteketea.

7 “Mtu akimpa jirani yake pesa au vitu amtunzie, navyo viibwe kutoka katika nyumba ya jirani huyo, mwizi akipatikana, lazima alipe mara mbili.+ 8 Mwizi asipopatikana, mwenye nyumba ataletwa mbele za Mungu wa kweli+ ili ithibitishwe ikiwa alichukua vitu vya jirani yake au la. 9 Katika visa vyote vya kumiliki vitu isivyo halali, iwe ni ng’ombe dume, punda, kondoo, nguo, au kitu chochote kilichopotea ambacho huenda mtu akasema, ‘Hiki ni changu!’ wote wawili wataleta kesi yao mbele za Mungu wa kweli.+ Yule ambaye Mungu atasema ana hatia atamlipa jirani yake mara mbili.+

10 “Mtu akimpa jirani yake punda au ng’ombe dume au kondoo au mnyama yeyote wa kufugwa amtunzie, kisha mnyama huyo afe au alemazwe au achukuliwe bila mtu yeyote kuona, 11 yule aliyepewa mali hiyo ataapa mbele za Yehova kwamba hakuchukua mali ya jirani yake; na mwenye mali anapaswa kukubali jambo hilo. Mtu huyo hatalipa chochote.+ 12 Lakini ikiwa mnyama huyo ameibwa kutoka kwake, atamlipa mwenye mnyama huyo. 13 Ikiwa mnyama huyo aliraruliwa na mnyama wa mwituni, atamleta kama ushahidi. Hatalipia kitu kilichoraruliwa na mnyama wa mwituni.

14 “Lakini mtu yeyote akiazima mnyama kutoka kwa jirani yake, na mnyama huyo alemazwe au afe wakati mwenyewe hayupo, aliyeazima mnyama huyo lazima alipe. 15 Ikiwa mwenyewe yupo, aliyeazima hatalipa. Ikiwa mnyama huyo alikodiwa, pesa iliyolipwa ili kumkodi ndiyo itakayokuwa malipo yake.

16 “Sasa mwanamume akimtongoza bikira ambaye hajachumbiwa kisha alale naye, lazima alipe mahari ili msichana huyo awe mke wake.+ 17 Baba yake akikataa kabisa kumpa msichana huyo, mwanamume huyo atalipa kiasi cha pesa kinacholingana na mahari.

18 “Hampaswi kumwacha mwanamke mchawi aishi.+

19 “Mtu yeyote anayefanya ngono na mnyama lazima auawe.+

20 “Mtu yeyote anayetoa dhabihu kwa miungu mingine isipokuwa kwa Yehova peke yake lazima auawe.+

21 “Msimtese wala kumkandamiza mkaaji mgeni,+ kwa sababu ninyi mlikuwa wakaaji wageni katika nchi ya Misri.+

22 “Msimtese mjane wala yatima.+ 23 Mkimtesa hata kidogo, naye anililie, hakika nitasikia kilio chake;+ 24 nami nitawaka hasira, nami nitawaua kwa upanga, na wake zenu watakuwa wajane, na watoto wenu watakuwa mayatima.

25 “Ukimkopesha pesa mtu yeyote maskini miongoni mwa watu wangu, mtu anayeishi nawe, usiwe kama mtu anayemkopesha pesa.* Hupaswi kumtoza riba.+

26 “Ukichukua nguo ya jirani yako kuwa dhamana ya mkopo,*+ unapaswa kumrudishia kabla ya jua kutua. 27 Kwa sababu hiyo ndiyo nguo pekee aliyo nayo ya kujifunika, nguo ya kufunika mwili wake,* atajifunikia nini anapolala?+ Akinililia, hakika nitasikia, kwa sababu mimi ni mwenye huruma.*+

28 “Usimtukane Mungu+ wala kumlaani kiongozi* miongoni mwa watu wako.+

29 “Usisite kutoa matoleo kutoka katika mazao yako mengi na kutoka kwenye mafuriko ya mashinikizo yako.*+ Unapaswa kunipa mzaliwa wa kwanza kati ya wanao.+ 30 Hivi ndivyo utakavyofanya kuhusu ng’ombe dume wako na kondoo wako:+ Atakaa na mama yake kwa siku saba. Siku ya nane, utanipa mimi.+

31 “Mnapaswa kujithibitisha wenyewe kuwa watu watakatifu mbele zangu,+ nanyi hampaswi kula nyama ya mnyama yeyote ambaye ameraruliwa na mnyama wa mwituni.+ Mnapaswa kuwatupia mbwa nyama hiyo.

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki