Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yeremia 48
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Yeremia—Yaliyomo

      • Unabii dhidi ya Moabu (1-47)

Yeremia 48:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Kilele salama kimeaibishwa.”

Marejeo

  • +Mwa 19:36, 37; Isa 15:1
  • +Hes 32:37, 38
  • +Yos 13:15, 19; Eze 25:9
  • +Isa 15:2

Yeremia 48:2

Marejeo

  • +Hes 32:37; Isa 16:8

Yeremia 48:3

Marejeo

  • +Isa 15:5; Yer 48:34

Yeremia 48:5

Marejeo

  • +Isa 15:5

Yeremia 48:6

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nafsi zenu.”

Yeremia 48:7

Marejeo

  • +Hes 21:29; 1Fa 11:7

Yeremia 48:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nchi tambarare ya chini itaangamia.”

  • *

    Au “uwanda utaharibiwa.”

Marejeo

  • +Eze 25:9

Yeremia 48:9

Marejeo

  • +Sef 2:9

Yeremia 48:13

Marejeo

  • +1Fa 12:28, 29; Ho. 10:15; Amo 5:5

Yeremia 48:14

Marejeo

  • +Isa 16:6

Yeremia 48:15

Marejeo

  • +Yer 48:8
  • +Isa 34:2
  • +Zb 24:8

Yeremia 48:16

Marejeo

  • +Eze 25:11

Yeremia 48:18

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “kwenye ardhi kavu.”

Marejeo

  • +Hes 21:30; Yos 13:15, 17; Isa 15:2
  • +Yer 48:8

Yeremia 48:19

Marejeo

  • +Hes 32:34; Kum 2:36

Yeremia 48:20

Marejeo

  • +Hes 21:13; Yos 13:8, 9

Yeremia 48:21

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “uwanda.”

Marejeo

  • +Sef 2:9
  • +Hes 21:23; Isa 15:4
  • +Yos 13:15, 18

Yeremia 48:22

Marejeo

  • +Hes 32:34
  • +Hes 32:3, 4

Yeremia 48:23

Marejeo

  • +Hes 32:37; Yer 48:1
  • +Hes 32:37, 38; Yos 13:15, 17; Eze 25:9

Yeremia 48:24

Marejeo

  • +Amo 2:2

Yeremia 48:25

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Pembe ya.”

Yeremia 48:26

Marejeo

  • +Yer 25:15, 16
  • +Yer 48:42

Yeremia 48:27

Marejeo

  • +Omb 2:15; Sef 2:8

Yeremia 48:29

Marejeo

  • +Isa 16:6; 25:10, 11; Sef 2:9, 10

Yeremia 48:31

Marejeo

  • +2Fa 3:24, 25; Isa 16:7

Yeremia 48:32

Marejeo

  • +Hes 21:32; 32:34, 35; Yos 21:8, 39
  • +Hes 32:37, 38; Yos 13:15, 19
  • +Isa 16:8, 9; Yer 48:8

Yeremia 48:33

Marejeo

  • +Yer 25:10
  • +Isa 16:10

Yeremia 48:34

Marejeo

  • +Hes 21:25; Yos 13:15, 17
  • +Hes 32:37; Isa 16:9
  • +Hes 21:23
  • +Yer 48:2, 3
  • +Isa 15:4-6

Yeremia 48:36

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “utakuwa na msukosuko kwa ajili ya.”

  • *

    Yaani, filimbi iliyopigwa wakati wa kuomboleza kwenye mazishi.

  • *

    Au “utakuwa na msukosuko kwa ajili ya.”

  • *

    Yaani, filimbi iliyopigwa wakati wa kuomboleza kwenye mazishi.

Marejeo

  • +Isa 16:11

Yeremia 48:37

Marejeo

  • +Yer 16:6
  • +Law 19:28
  • +Mwa 37:34; Isa 15:2, 3

Yeremia 48:40

Marejeo

  • +Omb 4:19; Hab 1:8
  • +Yer 49:22

Yeremia 48:42

Marejeo

  • +Yer 30:11
  • +Yer 48:29

Yeremia 48:45

Marejeo

  • +Hes 21:26, 28
  • +Hes 24:17; Amo 2:2

Yeremia 48:46

Marejeo

  • +Hes 21:29; 1Fa 11:7
  • +Yer 48:7

Yeremia 48:47

Marejeo

  • +Eze 25:11

Jumla

Yer. 48:1Mwa 19:36, 37; Isa 15:1
Yer. 48:1Hes 32:37, 38
Yer. 48:1Yos 13:15, 19; Eze 25:9
Yer. 48:1Isa 15:2
Yer. 48:2Hes 32:37; Isa 16:8
Yer. 48:3Isa 15:5; Yer 48:34
Yer. 48:5Isa 15:5
Yer. 48:7Hes 21:29; 1Fa 11:7
Yer. 48:8Eze 25:9
Yer. 48:9Sef 2:9
Yer. 48:131Fa 12:28, 29; Ho. 10:15; Amo 5:5
Yer. 48:14Isa 16:6
Yer. 48:15Yer 48:8
Yer. 48:15Isa 34:2
Yer. 48:15Zb 24:8
Yer. 48:16Eze 25:11
Yer. 48:18Hes 21:30; Yos 13:15, 17; Isa 15:2
Yer. 48:18Yer 48:8
Yer. 48:19Hes 32:34; Kum 2:36
Yer. 48:20Hes 21:13; Yos 13:8, 9
Yer. 48:21Sef 2:9
Yer. 48:21Hes 21:23; Isa 15:4
Yer. 48:21Yos 13:15, 18
Yer. 48:22Hes 32:34
Yer. 48:22Hes 32:3, 4
Yer. 48:23Hes 32:37; Yer 48:1
Yer. 48:23Hes 32:37, 38; Yos 13:15, 17; Eze 25:9
Yer. 48:24Amo 2:2
Yer. 48:26Yer 25:15, 16
Yer. 48:26Yer 48:42
Yer. 48:27Omb 2:15; Sef 2:8
Yer. 48:29Isa 16:6; 25:10, 11; Sef 2:9, 10
Yer. 48:312Fa 3:24, 25; Isa 16:7
Yer. 48:32Hes 21:32; 32:34, 35; Yos 21:8, 39
Yer. 48:32Hes 32:37, 38; Yos 13:15, 19
Yer. 48:32Isa 16:8, 9; Yer 48:8
Yer. 48:33Yer 25:10
Yer. 48:33Isa 16:10
Yer. 48:34Hes 21:25; Yos 13:15, 17
Yer. 48:34Hes 32:37; Isa 16:9
Yer. 48:34Hes 21:23
Yer. 48:34Yer 48:2, 3
Yer. 48:34Isa 15:4-6
Yer. 48:36Isa 16:11
Yer. 48:37Yer 16:6
Yer. 48:37Law 19:28
Yer. 48:37Mwa 37:34; Isa 15:2, 3
Yer. 48:40Omb 4:19; Hab 1:8
Yer. 48:40Yer 49:22
Yer. 48:42Yer 30:11
Yer. 48:42Yer 48:29
Yer. 48:45Hes 21:26, 28
Yer. 48:45Hes 24:17; Amo 2:2
Yer. 48:46Hes 21:29; 1Fa 11:7
Yer. 48:46Yer 48:7
Yer. 48:47Eze 25:11
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
  • 33
  • 34
  • 35
  • 36
  • 37
  • 38
  • 39
  • 40
  • 41
  • 42
  • 43
  • 44
  • 45
  • 46
  • 47
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Yeremia 48:1-47

Yeremia

48 Kuhusu Moabu,+ Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi:

“Ole wake Nebo,+ kwa maana ameangamizwa!

Kiriathaimu+ ameaibishwa na kutekwa.

Kimbilio salama limeaibishwa* na kuvunjwavunjwa.+

 2 Hawamsifu tena Moabu.

Kule Heshboni wamepanga njama ya kumwangusha:+

‘Njooni, tumkomeshe asiwe taifa.’

Wewe pia, ewe Madmeni, unapaswa kukaa kimya,

Kwa maana upanga unakufuata.

 3 Kuna sauti ya kilio kutoka Horonaimu,+

Ya uharibifu na anguko kubwa.

 4 Moabu amevunjwa.

Watoto wake wanalia kwa sauti.

 5 Kwenye njia inayopanda kwenda Luhithi wanaendelea kulia huku wakipanda.

Na kwenye njia inayoshuka kutoka Horonaimu wanasikia vilio vya taabu kwa sababu ya msiba.+

 6 Kimbieni, okoeni uhai wenu!*

Ni lazima muwe kama mberoshi nyikani.

 7 Kwa sababu unatumaini kazi zako na hazina zako,

Wewe pia utatekwa.

Na Kemoshi+ atapelekwa uhamishoni,

Pamoja na makuhani wake na wakuu wake.

 8 Mwangamizaji atakuja katika kila jiji,

Na hakuna jiji litakaloponyoka.+

Hakika bonde litaangamia,*

Na nchi tambarare itaharibiwa,* kama alivyosema Yehova.

 9 Mwekeeni Moabu alama,

Kwa maana atakapoanguka na kuwa magofu atakimbia,

Na majiji yake yatakuwa kitu cha kutisha,

Bila mkaaji.+

10 Alaaniwe mtu anayefanya kazi ya Yehova kwa uzembe!

Alaaniwe mtu anayeuzuia upanga wake usimwage damu!

11 Wamoabu hawajasumbuliwa tangu ujana wao,

Kama divai iliyotulia kwenye machicha.

Hawajamiminwa kutoka katika chombo kimoja kwenda kingine,

Nao hawajawahi kamwe kupelekwa uhamishoni.

Ndiyo sababu ladha yao imebaki vilevile,

Na harufu yao haijabadilika.

12 “‘Kwa hiyo tazama! siku zinakuja,’ asema Yehova, ‘nitakapowatuma watu wawapindue. Watawapindua na kumwaga kabisa kile kilicho ndani ya vyombo vyao, nao wataivunja mitungi yao mikubwa vipandevipande. 13 Na Wamoabu wataona aibu kwa sababu ya Kemoshi, kama watu wa nyumba ya Israeli walivyoona aibu kwa sababu ya Betheli, iliyokuwa tegemeo lao.+

14 Mnawezaje kuthubutu kusema: “Sisi ni mashujaa hodari, walio tayari kwa vita”?’+

15 ‘Moabu ameangamizwa,

Majiji yake yamevamiwa,+

Na vijana wao walio bora wamechinjwa,’+

Asema Mfalme, ambaye jina lake ni Yehova wa majeshi.+

16 Msiba wa Wamoabu unakuja hivi karibuni,

Na anguko lao linakaribia upesi.+

17 Wote wanaowazunguka watawasikitikia,

Wote wanaolijua jina lao.

Waambieni hivi: ‘Jinsi fimbo yenye nguvu ilivyovunjwa, fimbo ya urembo!’

18 Shuka chini kutoka kwenye utukufu wako,

Nawe uketi katika kiu,* ewe binti unayekaa Diboni,+

Kwa maana mwangamizaji wa Moabu amekuja kukushambulia,

Ataziharibu sehemu zako zenye ngome.+

19 Simama kando ya barabara utazame, wewe mkaaji wa Aroeri.+

Muulize mwanamume anayekimbia na mwanamke anayeponyoka. ‘Ni nini ambacho kimetokea?’

20 Moabu ameaibishwa na kushikwa na hofu.

Omboleza na ulie kwa sauti.

Tangazeni kule Arnoni+ kwamba Moabu ameangamizwa.

21 “Hukumu imekuja kwenye nchi tambarare,*+ dhidi ya Holoni, Yahazi,+ na Mefaathi;+ 22 dhidi ya Diboni,+ Nebo,+ na Beth-diblathaimu; 23 dhidi ya Kiriathaimu,+ Beth-gamuli, na Beth-meoni;+ 24 dhidi ya Keriothi+ na Bosra; na dhidi ya majiji yote ya nchi ya Moabu, yaliyo mbali na yaliyo karibu.

25 ‘Nguvu za* Moabu zimekatwa;

Na mkono wake umevunjwa,’ asema Yehova.

26 ‘Mlewesheni,+ kwa maana amejikweza dhidi ya Yehova.+

Moabu anagaagaa katika matapishi yake,

Naye ni kitu cha kudhihakiwa.

27 Je, kwako Israeli hakuwa kitu cha kudhihakiwa?+

Je, alipatikana kati ya wezi,

Hivi kwamba utikise kichwa chako na kumshutumu?

28 Ondokeni katika majiji, mkae kwenye jabali, ninyi wakaaji wa Moabu,

Na muwe kama njiwa anayejenga kiota kwenye kuta za korongo.’”

29 “Tumesikia kuhusu kiburi cha Moabu—ana majivuno sana—

Kuhusu kujisifu kwake, kiburi chake, majivuno yake, na jinsi moyo wake ulivyotutumuka.”+

30 “‘Ninajua ghadhabu yake,’ asema Yehova,

‘Lakini maneno yake matupu yatakuwa ya bure.

Hayatafanya chochote.

31 Ndiyo sababu nitaiombolezea Moabu,

Nitalia kwa sauti kwa ajili ya Moabu yote

Na kuwaombolezea wanaume wa Kir-heresi.+

32 Nitakulilia kwa kilio kinachoshinda kilio cha Yazeri,+

Nitakulilia, ewe mzabibu wa Sibma.+

Machipukizi yako yanayositawi yamevuka bahari.

Yamefika mpaka baharini, mpaka Yazeri.

Mwangamizaji ameshuka kwenye

Matunda yako ya wakati wa kiangazi na mavuno yako ya zabibu.+

33 Furaha na shangwe vimeondolewa katika shamba la matunda

Na katika nchi ya Moabu.+

Nimefanya divai iache kutiririka kutoka kwenye shinikizo la divai.

Hakuna mtu atakayelikanyaga shinikizo la divai kwa vigelegele vya shangwe.

Watapaza sauti lakini si kwa shangwe.’”+

34 “‘Kuna kilio kikubwa kutoka Heshboni+ mpaka Eleale.+

Wanapaza sauti yao mpaka Yahazi,+

Kutoka Soari mpaka Horonaimu,+ mpaka Eglath-shelishiya.

Hata maji ya Nimrimu yatabaki ukiwa.+

35 Nitamwondoa kabisa katika Moabu,’ asema Yehova,

‘Mtu anayeleta toleo mahali pa juu

Na mtu anayemtolea dhabihu mungu wake.

36 Ndiyo sababu moyo wangu utaiombolezea* Moabu kama filimbi,*+

Na moyo wangu utawaombolezea* wanaume wa Kir-heresi kama filimbi.*

Kwa kuwa utajiri aliopata utaangamia.

37 Kwa maana kila kichwa kina upara,+

Na ndevu zote zimenyolewa.

Kila mkono umekatwakatwa,+

Nao wamevaa nguo za magunia kiunoni!’”+

38 “‘Juu ya paa zote za Moabu

Na katika viwanja vyake vyote vya jiji,

Hakuna kitu kingine ila maombolezo.

Kwa maana nimemvunja Moabu

Kama chombo kilichotupwa,’ asema Yehova.

39 ‘Jinsi alivyo na hofu! Ombolezeni!

Jinsi Moabu alivyougeuza mgongo wake kwa aibu!

Moabu amekuwa kitu cha kudhihakiwa,

Kitu cha kutisha kwa wote wanaomzunguka.’”

40 “Kwa maana Yehova anasema hivi:

‘Tazama! Kama tai anayeshuka chini kwa ghafla,+

Atanyoosha mabawa yake juu ya Moabu.+

41 Miji itatekwa,

Na ngome zake zitachukuliwa.

Siku hiyo moyo wa mashujaa wa Moabu

Utakuwa kama moyo wa mwanamke anayezaa.’”

42 “‘Na Moabu ataangamizwa asiwe taifa,+

Kwa maana amejikweza dhidi ya Yehova.+

43 Hofu na shimo na mtego viko mbele yako,

Ewe mkaaji wa Moabu,’ asema Yehova.

44 ‘Yeyote anayekimbia hofu ataanguka shimoni,

Na yeyote anayetoka shimoni atanaswa na mtego.’

‘Kwa maana nitawaletea watu wa Moabu mwaka wao wa adhabu,’ asema Yehova.

45 ‘Katika kivuli cha Heshboni, wale wanaokimbia wanasimama wakiwa wameishiwa na nguvu.

Kwa maana moto utatoka Heshboni

Na mwali wa moto utatoka katikati ya Sihoni.+

Utateketeza kabisa paji la uso wa Moabu

Na fuvu la wana wa ghasia.’+

46 ‘Ole wako, ewe Moabu!

Watu wa Kemoshi+ wameangamia.

Kwa maana wana wako wamechukuliwa mateka,

Na mabinti zako wamepelekwa uhamishoni.+

47 Lakini siku za mwisho nitawakusanya watu wa Moabu waliotekwa,’ asema Yehova.

‘Hukumu ya Moabu imefikia hapa.’”+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki