Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ezekieli 25
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Ezekieli—Yaliyomo

      • Unabii dhidi ya Amoni (1-7)

      • Unabii dhidi ya Moabu (8-11)

      • Unabii dhidi ya Edomu (12-14)

      • Unabii dhidi ya Ufilisti (15-17)

Ezekieli 25:2

Marejeo

  • +Mwa 19:36, 38
  • +Yer 49:1; Amo 1:13; Sef 2:9

Ezekieli 25:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kambi zao zenye ukuta.”

Ezekieli 25:5

Marejeo

  • +2Sa 12:26; Eze 21:20

Ezekieli 25:6

Marejeo

  • +Omb 2:15
  • +Sef 2:8

Ezekieli 25:7

Marejeo

  • +Yer 49:2; Amo 1:14

Ezekieli 25:8

Marejeo

  • +Isa 15:1; Yer 48:1; Amo 2:1
  • +Kum 2:4

Ezekieli 25:9

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “mteremko.”

  • *

    Au “pambo la.”

Marejeo

  • +Hes 32:37, 38; Yos 13:15, 19

Ezekieli 25:10

Marejeo

  • +Eze 25:4
  • +Eze 21:28, 32

Ezekieli 25:11

Marejeo

  • +Yer 48:1

Ezekieli 25:12

Marejeo

  • +2Nya 28:17; Zb 137:7; Omb 4:22; Amo 1:11; Oba 10

Ezekieli 25:13

Marejeo

  • +Mal 1:4
  • +Yer 49:7, 8

Ezekieli 25:14

Marejeo

  • +Isa 11:14; 63:1
  • +Nah 1:2

Ezekieli 25:15

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kwa dharau iliyo katika nafsi yao.”

Marejeo

  • +2Nya 28:18; Isa 9:11, 12; 14:29; Yer 47:1; Yoe 3:4-6; Amo 1:6

Ezekieli 25:16

Marejeo

  • +Yer 25:17, 20; Sef 2:4
  • +Sef 2:5
  • +Yer 47:4

Jumla

Eze. 25:2Mwa 19:36, 38
Eze. 25:2Yer 49:1; Amo 1:13; Sef 2:9
Eze. 25:52Sa 12:26; Eze 21:20
Eze. 25:6Omb 2:15
Eze. 25:6Sef 2:8
Eze. 25:7Yer 49:2; Amo 1:14
Eze. 25:8Isa 15:1; Yer 48:1; Amo 2:1
Eze. 25:8Kum 2:4
Eze. 25:9Hes 32:37, 38; Yos 13:15, 19
Eze. 25:10Eze 25:4
Eze. 25:10Eze 21:28, 32
Eze. 25:11Yer 48:1
Eze. 25:122Nya 28:17; Zb 137:7; Omb 4:22; Amo 1:11; Oba 10
Eze. 25:13Mal 1:4
Eze. 25:13Yer 49:7, 8
Eze. 25:14Isa 11:14; 63:1
Eze. 25:14Nah 1:2
Eze. 25:152Nya 28:18; Isa 9:11, 12; 14:29; Yer 47:1; Yoe 3:4-6; Amo 1:6
Eze. 25:16Yer 25:17, 20; Sef 2:4
Eze. 25:16Sef 2:5
Eze. 25:16Yer 47:4
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Ezekieli 25:1-17

Ezekieli

25 Neno la Yehova likanijia tena likisema: 2 “Mwana wa binadamu, uelekeze uso wako kwa Waamoni,+ na utabiri dhidi yao.+ 3 Unapaswa kusema hivi kuhusu Waamoni, ‘Sikieni neno la Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Kwa sababu ulisema ‘Aha!’ dhidi ya mahali pangu patakatifu wakati palipotiwa unajisi, na dhidi ya nchi ya Israeli ilipofanywa ukiwa, na dhidi ya watu wa nyumba ya Yuda, walipopelekwa uhamishoni, 4 kwa hiyo, ninakutia mikononi mwa Watu wa Mashariki uwe mali yao. Watapiga kambi zao* ndani yako na kusimamisha mahema yao kati yako. Watakula matunda yako, na kunywa maziwa yako. 5 Nitalifanya jiji la Raba+ liwe malisho ya ngamia, na nchi ya Waamoni iwe mahali pa kupumzika kwa ajili ya mifugo; nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.”’”

6 “Kwa maana Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Kwa sababu ulipiga makofi+ na kupiga miguu yako chini nawe ukashangilia kwa dharau kubwa dhidi ya nchi ya Israeli,+ 7 kwa hiyo nitaunyoosha mkono wangu dhidi yako ili nikutie mikononi mwa mataifa uwe kitu cha kuporwa. Nitakukatilia mbali kutoka kati ya mataifa na kukuharibu kutoka katika nchi hizi.+ Nitakuangamiza, nawe utalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’

8 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Kwa sababu watu wa Moabu+ na Seiri+ wamesema, “Tazama! Nyumba ya Yuda ni kama mataifa mengine yote,” 9 ninauacha wazi mpaka* wa Moabu kwenye majiji yake ya mpakani, uzuri wa* nchi yake, Beth-yeshimothi, Baal-meoni, hadi Kiriathaimu.+ 10 Nitaitoa pamoja na Waamoni kuwa mali ya watu wa Mashariki,+ ili Waamoni wasikumbukwe kati ya mataifa.+ 11 Nami nitatekeleza hukumu katika Moabu,+ nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’

12 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Nchi ya Edomu imelipiza kisasi dhidi ya nyumba ya Yuda nayo imepata hatia kubwa kwa kulipiza kisasi dhidi yake;+ 13 kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Pia nitaunyoosha mkono wangu dhidi ya Edomu na kuwaangamiza wanadamu na wanyama waliomo, nami nitaifanya kuwa ukiwa.+ Kuanzia Temani mpaka Dedani, watauawa kwa upanga.+ 14 ‘Nitalipiza kisasi dhidi ya Edomu kwa mkono wa watu wangu Waisraeli.+ Watawaletea watu wa Edomu hasira yangu na ghadhabu yangu, ili wapatwe na kisasi changu mwenyewe,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”’

15 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Kwa sababu ya chuki yao isiyo na mwisho, Wafilisti wamejaribu kwa nia ovu* kulipiza kisasi na kuleta maangamizi.+ 16 Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Ninaunyoosha mkono wangu dhidi ya Wafilisti,+ nami nitawakatilia mbali Wakerethi+ na kuwaangamiza wakaaji wanaobaki wa pwani ya bahari.+ 17 Nitatekeleza matendo makubwa ya kisasi dhidi yao kwa adhabu kali, nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova nitakapoleta kisasi changu dhidi yao.”’”

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki