Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ezekieli 35
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Ezekieli—Yaliyomo

      • Unabii dhidi ya milima ya Seiri (1-15)

Ezekieli 35:2

Marejeo

  • +Mwa 32:3; Kum 2:5
  • +Yer 49:8; Omb 4:22; Eze 25:8, 9; Oba 1

Ezekieli 35:3

Marejeo

  • +Eze 25:12, 13

Ezekieli 35:4

Marejeo

  • +Yoe 3:19; Mal 1:3

Ezekieli 35:5

Marejeo

  • +Mwa 27:41; Amo 1:11
  • +Zb 137:7; Oba 10

Ezekieli 35:6

Marejeo

  • +Oba 15
  • +Eze 25:14

Ezekieli 35:7

Marejeo

  • +Eze 25:13

Ezekieli 35:9

Marejeo

  • +Yer 49:17, 18; Eze 25:13; Mal 1:4

Ezekieli 35:10

Marejeo

  • +Eze 36:5; Oba 13

Ezekieli 35:11

Marejeo

  • +Amo 1:11

Ezekieli 35:12

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “tumepewa kama chakula.”

Ezekieli 35:13

Marejeo

  • +Oba 3

Ezekieli 35:15

Marejeo

  • +Omb 4:21; Oba 12, 15
  • +Isa 34:5; Eze 25:12, 13; 36:5

Jumla

Eze. 35:2Mwa 32:3; Kum 2:5
Eze. 35:2Yer 49:8; Omb 4:22; Eze 25:8, 9; Oba 1
Eze. 35:3Eze 25:12, 13
Eze. 35:4Yoe 3:19; Mal 1:3
Eze. 35:5Mwa 27:41; Amo 1:11
Eze. 35:5Zb 137:7; Oba 10
Eze. 35:6Oba 15
Eze. 35:6Eze 25:14
Eze. 35:7Eze 25:13
Eze. 35:9Yer 49:17, 18; Eze 25:13; Mal 1:4
Eze. 35:10Eze 36:5; Oba 13
Eze. 35:11Amo 1:11
Eze. 35:13Oba 3
Eze. 35:15Omb 4:21; Oba 12, 15
Eze. 35:15Isa 34:5; Eze 25:12, 13; 36:5
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Ezekieli 35:1-15

Ezekieli

35 Neno la Yehova likanijia tena likisema: 2 “Mwana wa binadamu, uelekeze uso wako kwenye eneo lenye milima la Seiri,+ na utabiri dhidi yake.+ 3 Uliambie, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Niko dhidi yako, ewe eneo lenye milima la Seiri, nami nitaunyoosha mkono wangu dhidi yako na kukufanya uwe mahame na ukiwa.+ 4 Nitayafanya majiji yako kuwa magofu, nawe utakuwa mahame na ukiwa;+ nawe utalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova. 5 Kwa maana ulikuwa na chuki isiyo na mwisho,+ nawe uliwatia Waisraeli mikononi mwa upanga wakati wa msiba wao, wakati wa adhabu yao ya mwisho.”’+

6 “‘Kwa hiyo, kwa hakika kama ninavyoishi,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘nitakutayarisha kwa ajili ya umwagaji wa damu, na umwagaji wa damu utakufuatia.+ Kwa maana uliichukia damu, umwagaji wa damu utakufuatia.+ 7 Nitalifanya eneo lenye milima la Seiri kuwa mahame na ukiwa,+ nami nitamwangamiza mtu yeyote anayepitia humo na yeyote anayerudi. 8 Nitaijaza milima yake watu waliouawa; na wale waliouawa kwa upanga wataanguka kwenye vilima vyako, katika mabonde yako, na katika vijito vyako vyote. 9 Nitakufanya uwe ukiwa wa kudumu, na majiji yako hayatakaliwa;+ nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’

10 “Kwa sababu ulisema, ‘Mataifa haya mawili na nchi hizi mbili zitakuwa zangu, nasi tutazimiliki zote mbili,’+ hata ingawa Yehova mwenyewe alikuwa humo, 11 ‘kwa hiyo kwa hakika kama ninavyoishi,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘nitakutendea kulingana na hasira ileile na wivu uleule ulioonyesha ulipowachukia;+ nami nitajijulisha miongoni mwao nitakapokuhukumu. 12 Kisha utalazimika kujua kwamba mimi mwenyewe, Yehova, nimesikia mambo yote ya dharau uliyosema kuhusu milima ya Israeli, uliposema, “Imefanywa ukiwa nasi tumepewa ili tuinyafue.”* 13 Nanyi mlizungumza kwa kiburi dhidi yangu, na kuzidisha maneno yenu dhidi yangu.+ Niliyasikia yote.’

14 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Dunia yote itashangilia nitakapokufanya uwe mahame na ukiwa. 15 Kama ulivyoshangilia urithi wa watu wa nyumba ya Israeli ulipofanywa ukiwa, hivyo ndivyo nitakavyokutendea.+ Utakuwa magofu yaliyo ukiwa, ewe eneo lenye milima la Seiri, naam, Edomu yote;+ nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’”

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki