Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ezekieli 37
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Ezekieli—Yaliyomo

      • Maono ya bonde la mifupa mikavu (1-14)

      • Vijiti viwili vitaunganishwa pamoja (15-28)

        • Taifa moja chini ya mfalme mmoja (22)

        • Agano la kudumu la amani (26)

Ezekieli 37:1

Marejeo

  • +Ufu 21:10

Ezekieli 37:2

Marejeo

  • +Eze 37:11

Ezekieli 37:3

Marejeo

  • +Kum 32:39; 1Sa 2:6

Ezekieli 37:5

Marejeo

  • +Mwa 2:7; Eze 37:14

Ezekieli 37:9

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “pumzi; roho.”

Ezekieli 37:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “roho.”

Marejeo

  • +Ufu 11:11

Ezekieli 37:11

Marejeo

  • +Eze 36:10
  • +Isa 49:14

Ezekieli 37:12

Marejeo

  • +Isa 66:14
  • +Eze 11:17; Amo 9:14

Ezekieli 37:13

Marejeo

  • +Zb 126:2

Ezekieli 37:14

Marejeo

  • +Isa 32:14, 15; Eze 36:27

Ezekieli 37:16

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “wanaoshirikiana naye.”

  • *

    Au “wanaoshirikiana naye.”

Marejeo

  • +2Nya 15:9; 30:11
  • +1Fa 11:31; 12:20

Ezekieli 37:17

Marejeo

  • +Isa 11:13; Yer 3:18

Ezekieli 37:18

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “wana wa watu wako.”

Ezekieli 37:19

Marejeo

  • +Yer 50:4; Zek 10:6

Ezekieli 37:21

Marejeo

  • +Kum 30:3; Isa 11:12; Yer 16:14, 15; Amo 9:14

Ezekieli 37:22

Marejeo

  • +Yer 3:18; Ho. 1:11
  • +Mwa 49:10; Zb 2:6; Isa 9:6; Yer 23:5; Lu 1:32
  • +Eze 37:19; Zek 10:6

Ezekieli 37:23

Maelezo ya Chini

  • *

    Huenda neno la Kiebrania linahusiana na neno “mavi,” nalo hutumiwa kuonyesha dharau.

Marejeo

  • +Isa 2:18; Eze 11:18; Ho. 14:8; Zek 13:2
  • +Yer 31:33; Eze 36:28

Ezekieli 37:24

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “maamuzi yangu ya hukumu.”

Marejeo

  • +Yer 23:5; 30:9; Ho. 3:5; Lu 1:32
  • +Yoh 10:16; 1Pe 5:4
  • +Kum 30:8-10; Yer 32:39; Eze 36:27

Ezekieli 37:25

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “wana.”

  • *

    Au “mkuu.”

Marejeo

  • +Yer 30:3
  • +Yoe 3:20
  • +Isa 60:21; Amo 9:15
  • +Eze 34:24; Lu 1:32

Ezekieli 37:26

Marejeo

  • +Eze 34:25
  • +Yer 30:19; Zek 8:5

Ezekieli 37:27

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Makao yangu yatakuwa; Nyumba yangu itakuwa.”

  • *

    Au “juu yao.”

Marejeo

  • +Law 26:12; Eze 11:19, 20; 43:7; Ho. 2:23; Ufu 21:3

Ezekieli 37:28

Marejeo

  • +Eze 36:23

Jumla

Eze. 37:1Ufu 21:10
Eze. 37:2Eze 37:11
Eze. 37:3Kum 32:39; 1Sa 2:6
Eze. 37:5Mwa 2:7; Eze 37:14
Eze. 37:10Ufu 11:11
Eze. 37:11Eze 36:10
Eze. 37:11Isa 49:14
Eze. 37:12Isa 66:14
Eze. 37:12Eze 11:17; Amo 9:14
Eze. 37:13Zb 126:2
Eze. 37:14Isa 32:14, 15; Eze 36:27
Eze. 37:162Nya 15:9; 30:11
Eze. 37:161Fa 11:31; 12:20
Eze. 37:17Isa 11:13; Yer 3:18
Eze. 37:19Yer 50:4; Zek 10:6
Eze. 37:21Kum 30:3; Isa 11:12; Yer 16:14, 15; Amo 9:14
Eze. 37:22Yer 3:18; Ho. 1:11
Eze. 37:22Mwa 49:10; Zb 2:6; Isa 9:6; Yer 23:5; Lu 1:32
Eze. 37:22Eze 37:19; Zek 10:6
Eze. 37:23Isa 2:18; Eze 11:18; Ho. 14:8; Zek 13:2
Eze. 37:23Yer 31:33; Eze 36:28
Eze. 37:24Yer 23:5; 30:9; Ho. 3:5; Lu 1:32
Eze. 37:24Yoh 10:16; 1Pe 5:4
Eze. 37:24Kum 30:8-10; Yer 32:39; Eze 36:27
Eze. 37:25Yer 30:3
Eze. 37:25Yoe 3:20
Eze. 37:25Isa 60:21; Amo 9:15
Eze. 37:25Eze 34:24; Lu 1:32
Eze. 37:26Eze 34:25
Eze. 37:26Yer 30:19; Zek 8:5
Eze. 37:27Law 26:12; Eze 11:19, 20; 43:7; Ho. 2:23; Ufu 21:3
Eze. 37:28Eze 36:23
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Ezekieli 37:1-28

Ezekieli

37 Mkono wa Yehova ulikuwa juu yangu, naye Yehova akanichukua kwa roho yake na kuniweka chini katikati ya bonde tambarare,+ nalo lilikuwa limejaa mifupa. 2 Akanizungusha kwenye mifupa hiyo yote, nami nikaona kwamba kulikuwa na mifupa mingi sana katika bonde hilo tambarare, nayo ilikuwa mikavu sana.+ 3 Akaniuliza: “Mwana wa binadamu, je, mifupa hii inaweza kuwa hai?” Nikajibu: “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, wewe ndiye unayejua.”+ 4 Basi akaniambia: “Itabirie mifupa hii, uiambie, ‘Enyi mifupa mikavu, lisikieni neno la Yehova:

5 “‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova ameiambia hivi mifupa hii: “Nitatia pumzi ndani yenu, nanyi mtakuwa hai.+ 6 Nitaweka kano na nyama juu yenu, nami nitawafunika kwa ngozi na kutia pumzi ndani yenu, nanyi mtakuwa hai; nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.”’”

7 Kisha nikatabiri kama nilivyoamriwa. Mara tu nilipotabiri, nikasikia sauti, sauti ya vitu vinavyogongana, nayo mifupa ikaanza kukaribiana, mfupa kwa mfupa. 8 Kisha nikaona kano na nyama zikija juu yake, na ngozi ikazifunika. Lakini bado hakukuwa na pumzi ndani yake.

9 Kisha akaniambia: “Utabirie upepo. Tabiri, mwana wa binadamu, nawe uuambie upepo, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Njoo kutoka kwenye zile pepo nne, ewe upepo,* nawe uwapulizie watu waliouawa, ili wawe hai.”’”

10 Basi nikatabiri kama alivyoniamuru, nayo pumzi* ikaingia ndani yao, nao wakaanza kuishi na kusimama kwa miguu yao;+ walikuwa jeshi kubwa ajabu.

11 Kisha akaniambia: “Mwana wa binadamu, mifupa hii ni watu wote wa nyumba ya Israeli.+ Wanasema, ‘Mifupa yetu imekauka, nalo tumaini letu limepotea.+ Tumeangamizwa kabisa.’ 12 Basi tabiri uwaambie, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Nitayafungua makaburi yenu+ na kuwainua kutoka katika makaburi yenu, watu wangu, na kuwaleta katika nchi ya Israeli.+ 13 Nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova nitakapoyafungua makaburi yenu na nitakapowainua kutoka katika makaburi yenu, enyi watu wangu.”’+ 14 ‘Nitaitia roho yangu ndani yenu,+ nanyi mtakuwa hai, nami nitawafanya mwishi katika nchi yenu; nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi mwenyewe, Yehova, nimesema nami nimelitenda,’ asema Yehova.”

15 Neno la Yehova likanijia tena likisema: 16 “Nawe, mwana wa binadamu, chukua kijiti nawe uandike juu yake, ‘Kwa ajili ya Yuda na kwa ajili ya watu wa Israeli walio pamoja naye.’*+ Kisha uchukue kijiti kingine na kuandika juu yake, ‘Kwa ajili ya Yosefu, kijiti cha Efraimu, na watu wote wa nyumba ya Israeli walio pamoja naye.’*+ 17 Kisha viunganishe ili viwe kijiti kimoja tu mkononi mwako.+ 18 Watu wako* watakapokuuliza, ‘Je, hutatuambia mambo haya yanamaanisha nini?’ 19 waambie, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Nitakichukua kijiti cha Yosefu, kilicho mkononi mwa Efraimu, na makabila ya Israeli yaliyo pamoja naye, nami nitakiunganisha na kijiti cha Yuda; nami nitavifanya viwe kijiti kimoja,+ navyo vitakuwa kijiti kimoja mkononi mwangu.”’ 20 Vijiti utakavyoandika juu yake vinapaswa kuwa mkononi mwako ili wavione.

21 “Kisha uwaambie, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Nitawachukua Waisraeli kutoka katika mataifa ambako walienda, nami nitawakusanya pamoja kutoka kila upande na kuwaleta katika nchi yao.+ 22 Nitawafanya kuwa taifa moja katika nchi hiyo,+ kwenye milima ya Israeli, na mfalme mmoja atawatawala wote,+ nao hawatakuwa tena mataifa mawili; wala hawatagawanyika tena kuwa falme mbili.+ 23 Hawatajitia unajisi tena kwa sanamu zao zinazochukiza* na kwa matendo yao yanayochukiza na kwa makosa yao yote.+ Nitawaokoa kutoka katika ukosefu wao wote wa uaminifu ambao umewafanya watende dhambi, nami nitawatakasa. Watakuwa watu wangu, nami mwenyewe nitakuwa Mungu wao.+

24 “‘“Mtumishi wangu Daudi atakuwa mfalme wao,+ na wote watakuwa na mchungaji mmoja.+ Watatembea katika sheria zangu* na kuzishika amri zangu kwa uangalifu.+ 25 Wataishi katika nchi niliyompa mtumishi wangu, Yakobo, ambamo mababu zenu waliishi,+ nao watakaa humo milele,+ wao na watoto* wao na watoto wa watoto wao;+ na mtumishi wangu Daudi atakuwa kiongozi* wao milele.+

26 “‘“Nami nitafanya agano la amani pamoja nao;+ litakuwa agano la milele pamoja nao. Nitawaimarisha na kuwafanya wawe wengi+ na kupaweka mahali pangu patakatifu miongoni mwao milele. 27 Hema langu litakuwa* pamoja nao,* nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.+ 28 Na mataifa yatalazimika kujua kwamba mimi, Yehova, ninawatakasa Waisraeli mahali pangu patakatifu patakapokuwa kati yao milele.”’”+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki