Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ezekieli 4
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Ezekieli—Yaliyomo

      • Aonyesha jinsi Yerusalemu litakavyozingirwa (1-17)

        • Abeba hatia kwa siku 390 na siku 40 (4-7)

Ezekieli 4:2

Marejeo

  • +2Fa 24:11; Yer 39:1
  • +2Fa 25:1
  • +Yer 6:6; 32:24
  • +Eze 21:22

Ezekieli 4:3

Marejeo

  • +Eze 12:6; 24:24

Ezekieli 4:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “juu yake,” yaani, upande wa kushoto wa Ezekieli.

Marejeo

  • +2Fa 17:21

Ezekieli 4:5

Marejeo

  • +Hes 14:34; 1Fa 12:19, 20

Ezekieli 4:6

Marejeo

  • +2Fa 23:27

Ezekieli 4:7

Marejeo

  • +Yer 52:4

Ezekieli 4:9

Marejeo

  • +Eze 4:5

Ezekieli 4:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Karibu gramu 230. Angalia Nyongeza B14.

Ezekieli 4:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Karibu lita 0.6. Angalia Nyongeza B14.

Ezekieli 4:13

Marejeo

  • +Ho. 9:3

Ezekieli 4:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nafsi yangu haijatiwa.”

  • *

    Au “mbaya.”

Marejeo

  • +Kut 22:31; Law 7:24; 11:40
  • +Kum 14:3; Isa 65:4; 66:17

Ezekieli 4:16

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “nitazivunja fito za mikate.” Labda ni fito zilizotumiwa kuhifadhia mikate.

Marejeo

  • +Law 26:26; Isa 3:1; Eze 5:16
  • +2Fa 25:3; Yer 37:21; Omb 1:11; 4:9; 5:9, 10
  • +Eze 12:18

Jumla

Eze. 4:22Fa 24:11; Yer 39:1
Eze. 4:22Fa 25:1
Eze. 4:2Yer 6:6; 32:24
Eze. 4:2Eze 21:22
Eze. 4:3Eze 12:6; 24:24
Eze. 4:42Fa 17:21
Eze. 4:5Hes 14:34; 1Fa 12:19, 20
Eze. 4:62Fa 23:27
Eze. 4:7Yer 52:4
Eze. 4:9Eze 4:5
Eze. 4:13Ho. 9:3
Eze. 4:14Kut 22:31; Law 7:24; 11:40
Eze. 4:14Kum 14:3; Isa 65:4; 66:17
Eze. 4:16Law 26:26; Isa 3:1; Eze 5:16
Eze. 4:162Fa 25:3; Yer 37:21; Omb 1:11; 4:9; 5:9, 10
Eze. 4:16Eze 12:18
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Ezekieli 4:1-17

Ezekieli

4 “Na wewe, mwana wa binadamu, chukua tofali na uliweke mbele yako. Uchonge jiji juu yake—Yerusalemu. 2 Lizingire na ujenge ukuta wa kulizingira,+ utengeneze boma la kulizingira,+ upige kambi kulizunguka,+ na kulizungushia mitambo ya kubomolea.+ 3 Chukua kiokeo cha chuma, na ukiweke kuwa ukuta wa chuma kati yako na jiji hilo. Kisha ukaze uso wako dhidi yake, nalo litazingirwa; nawe utalizingira. Hiyo ni ishara kwa watu wa nyumba ya Israeli.+

4 “Kisha ulalie upande wako wa kushoto na uweke hatia ya watu wa nyumba ya Israeli juu yako.*+ Utabeba hatia yao kwa idadi ya siku utakazolalia upande wako wa kushoto. 5 Na mimi nitakupa wewe siku 390, zinazolingana na miaka ya hatia yao,+ nawe utaibeba hatia ya watu wa nyumba ya Israeli. 6 Nawe lazima uzitimize.

“Kisha kwa mara ya pili utalala chini, utalalia upande wako wa kulia, nawe utaibeba hatia ya watu wa nyumba ya Yuda+ kwa siku 40. Nimekupa wewe siku moja kwa mwaka mmoja, siku moja kwa mwaka mmoja. 7 Nawe utauelekeza uso wako kwa jiji la Yerusalemu lililozingirwa,+ mkono wako ukiwa wazi, nawe utatabiri dhidi ya jiji hilo.

8 “Tazama! Nitakufunga kwa kamba ili usiweze kugeuka kutoka upande mmoja kwenda upande mwingine, mpaka utakapotimiza siku zako za kulizingira.

9 “Na uchukue ngano, shayiri, maharagwe mapana, dengu, mtama, na kusemethi, nawe uvitie katika chombo kimoja na ujitengenezee mkate. Kwa idadi ya siku unazolalia upande wako, siku 390, utaula.+ 10 Utapima na kula shekeli 20* za chakula kwa siku. Utaula nyakati hususa.

11 “Na utakunywa maji kwa kipimo, sehemu ya sita ya hini.* Utayanywa nyakati hususa.

12 “Utaula kama ambavyo ungekula mkate wa mviringo wa shayiri; utauoka mbele ya macho yao, ukitumia mavi ya wanadamu yaliyokauka.” 13 Na Yehova akaendelea kusema: “Hivyo ndivyo Waisraeli watakavyoula mkate wao—usio safi—kati ya mataifa ambako nitawatawanya.”+

14 Ndipo nikasema: “Isiwe hivyo, Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova! Tangu ujana wangu mpaka sasa sijatiwa* unajisi kwa kula nyama ya mnyama ambaye amepatikana amekufa wala mnyama aliyeraruliwa,+ na nyama isiyo safi* haijawahi kuingia kinywani mwangu.”+

15 Basi akaniambia: “Sawa, nitakuruhusu utumie mavi ya ng’ombe badala ya mavi ya wanadamu, nawe utaoka mkate wako juu yake.” 16 Naye akaniambia: “Mwana wa binadamu, nitafanya chakula kikosekane* Yerusalemu,+ na kwa wasiwasi mwingi watakula mkate wao kwa kipimo,+ na kwa hofu nyingi watakunywa maji yao kwa kipimo.+ 17 Hili litatukia ili wakose mkate na maji, nao waangaliane kwa mshtuko na kudhoofika kwa sababu ya kosa lao.

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki