Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ezekieli 43
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Ezekieli—Yaliyomo

      • Utukufu wa Yehova wajaa hekaluni (1-12)

      • Madhabahu (13-27)

Ezekieli 43:1

Marejeo

  • +Eze 40:6; 42:15; 44:1

Ezekieli 43:2

Marejeo

  • +Eze 9:3; 11:23
  • +Eze 1:24; Yoh 12:28, 29
  • +Isa 6:3; Eze 10:4

Ezekieli 43:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “alipokuja.”

Marejeo

  • +Eze 1:3, 4; 3:23

Ezekieli 43:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “kwenye ile nyumba.”

Marejeo

  • +Eze 10:19; 44:1, 2

Ezekieli 43:5

Marejeo

  • +Kut 40:34; 1Fa 8:10; Eze 44:4

Ezekieli 43:6

Marejeo

  • +Eze 40:3

Ezekieli 43:7

Marejeo

  • +Isa 6:1; Yer 3:17; Eze 1:26
  • +1Nya 28:2
  • +Kut 29:45; Zb 68:16; 132:14; Yoe 3:17
  • +Eze 39:7; Zek 13:2

Ezekieli 43:8

Marejeo

  • +Eze 8:3
  • +Da 9:12

Ezekieli 43:9

Marejeo

  • +Eze 37:23, 26; 2Ko 6:16

Ezekieli 43:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “kupima kielelezo chake.”

Marejeo

  • +Eze 40:4
  • +Eze 16:63

Ezekieli 43:11

Marejeo

  • +Eze 44:5
  • +Eze 11:19, 20; 36:27

Ezekieli 43:12

Marejeo

  • +Zb 93:5; Eze 40:2; 42:20

Ezekieli 43:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Hiki ni kipimo cha mikono mirefu. Angalia Nyongeza B14.

  • *

    Yaani, upana wa kiganja cha mkono kuanzia kidole gumba hadi kidole kidogo, karibu sentimita 22.2 ( inchi 8.75). Angalia Nyongeza B14.

Marejeo

  • +Kut 27:1; 2Nya 4:1

Ezekieli 43:15

Marejeo

  • +Kut 27:2; Ufu 9:13

Ezekieli 43:16

Marejeo

  • +Kut 38:1; 2Nya 4:1

Ezekieli 43:18

Marejeo

  • +Kut 40:29; Law 1:5; 8:18-21; Eze 45:19

Ezekieli 43:19

Marejeo

  • +Eze 40:46; 44:15; 48:11
  • +Kut 29:10; Law 8:14

Ezekieli 43:20

Marejeo

  • +Kut 29:36, 37; Law 8:15; Ebr 9:23

Ezekieli 43:21

Marejeo

  • +Kut 29:14; Law 8:17; Ebr 13:11

Ezekieli 43:24

Marejeo

  • +Law 2:13

Ezekieli 43:25

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “walio kamili.”

Marejeo

  • +Kut 29:35

Ezekieli 43:27

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, za watu.

Marejeo

  • +Law 9:1
  • +Eze 20:40

Jumla

Eze. 43:1Eze 40:6; 42:15; 44:1
Eze. 43:2Eze 9:3; 11:23
Eze. 43:2Eze 1:24; Yoh 12:28, 29
Eze. 43:2Isa 6:3; Eze 10:4
Eze. 43:3Eze 1:3, 4; 3:23
Eze. 43:4Eze 10:19; 44:1, 2
Eze. 43:5Kut 40:34; 1Fa 8:10; Eze 44:4
Eze. 43:6Eze 40:3
Eze. 43:7Isa 6:1; Yer 3:17; Eze 1:26
Eze. 43:71Nya 28:2
Eze. 43:7Kut 29:45; Zb 68:16; 132:14; Yoe 3:17
Eze. 43:7Eze 39:7; Zek 13:2
Eze. 43:8Eze 8:3
Eze. 43:8Da 9:12
Eze. 43:9Eze 37:23, 26; 2Ko 6:16
Eze. 43:10Eze 40:4
Eze. 43:10Eze 16:63
Eze. 43:11Eze 44:5
Eze. 43:11Eze 11:19, 20; 36:27
Eze. 43:12Zb 93:5; Eze 40:2; 42:20
Eze. 43:13Kut 27:1; 2Nya 4:1
Eze. 43:15Kut 27:2; Ufu 9:13
Eze. 43:16Kut 38:1; 2Nya 4:1
Eze. 43:18Kut 40:29; Law 1:5; 8:18-21; Eze 45:19
Eze. 43:19Eze 40:46; 44:15; 48:11
Eze. 43:19Kut 29:10; Law 8:14
Eze. 43:20Kut 29:36, 37; Law 8:15; Ebr 9:23
Eze. 43:21Kut 29:14; Law 8:17; Ebr 13:11
Eze. 43:24Law 2:13
Eze. 43:25Kut 29:35
Eze. 43:27Law 9:1
Eze. 43:27Eze 20:40
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Ezekieli 43:1-27

Ezekieli

43 Kisha akanipeleka kwenye lango linalotazama mashariki.+ 2 Hapo nikaona utukufu wa Mungu wa Israeli ukija kutoka mashariki,+ na sauti yake ilikuwa kama sauti ya maji yenye kishindo;+ nayo dunia iling’aa kwa utukufu wake.+ 3 Mambo niliyoona yalikuwa kama maono niliyoona nilipokuja* kuliangamiza jiji, na yalionekana kama mambo niliyoona karibu na mto Kebari;+ nami nikaanguka kifudifudi.

4 Kisha utukufu wa Yehova ukaingia hekaluni* kupitia lango lililotazama mashariki.+ 5 Ndipo roho ikaniinua na kuniingiza kwenye ua wa ndani, nami nikaona kwamba hekalu lilikuwa limejaa utukufu wa Yehova.+ 6 Kisha nikasikia mtu akizungumza nami kutoka katika lile hekalu, na mtu huyo akaja na kusimama kando yangu.+ 7 Akaniambia:

“Mwana wa binadamu, hapa ndipo mahali pa kiti changu cha ufalme+ na mahali pa nyayo za miguu yangu,+ ambapo nitakaa kati ya watu wa Israeli milele.+ Watu wa nyumba ya Israeli hawatalichafua tena jina langu takatifu,+ wao na wafalme wao, kwa ukahaba wao wa kiroho na kwa maiti za wafalme wao wanapokufa. 8 Kwa kuweka kizingiti chao kando ya kizingiti changu na mwimo wa mlango wao kando ya mwimo wa mlango wangu, kukiwa na ukuta tu kati yangu nao,+ walilichafua jina langu takatifu kwa mambo yanayochukiza waliyotenda hivi kwamba nikawaangamiza kabisa kwa hasira yangu.+ 9 Basi sasa na wauweke mbali nami ukahaba wao wa kiroho na maiti za wafalme wao, nami nitakaa miongoni mwao milele.+

10 “Na wewe, mwana wa binadamu, waeleze watu wa nyumba ya Israeli kuhusu hekalu+ ili waaibike kwa sababu ya makosa yao,+ nao wanapaswa kuichunguza ramani yake.* 11 Ikiwa wataaibika kwa sababu ya mambo yote ambayo wamefanya, unapaswa kuwaonyesha ramani ya hekalu, mpangilio wake, na njia zake za kutokea, na za kuingilia.+ Waonyeshe ramani zake zote na maagizo yake, ramani zake na sheria zake, nawe uziandike mbele ya macho yao, ili waone ramani zake zote na kufuata maagizo yake.+ 12 Hii ndiyo sheria ya hekalu. Eneo lote kuzunguka juu ya mlima ni takatifu zaidi.+ Tazama! Hii ndiyo sheria ya hekalu.

13 “Hivi ndivyo vipimo vya madhabahu kwa kipimo cha mikono+ (kila mkono uliongezwa kiganja kimoja).* Sehemu yake ya chini ni mkono mmoja na upana wake mkono mmoja. Ina ukingo ambao upana wake ni shubiri* moja kuzunguka pembeni. Hiyo ndiyo sehemu ya chini ya madhabahu. 14 Kuanzia sehemu ya chini ya sakafu mpaka kwenye kidato cha chini kinachozunguka pande zote ni mikono miwili, na upana wake ni mkono mmoja. Kuanzia kidato kidogo kinachozunguka pande zote mpaka kwenye kidato kikubwa kinachozunguka pande zote ni mikono minne, na upana wake ni mkono mmoja. 15 Jiko la madhabahu lina urefu wa mikono minne, na kutoka kwenye jiko la madhabahu kuelekea juu kuna zile pembe nne.+ 16 Jiko la madhabahu ni la mraba, urefu wake ni mikono 12 na upana wake ni mikono 12.+ 17 Pande nne za kidato kinachozunguka zina urefu wa mikono 14 na upana wa mikono 14; na ukingo unaozunguka ni nusu mkono, na sehemu yake ya chini ni mkono mmoja pande zote.

“Na ngazi zake zinatazama upande wa mashariki.”

18 Kisha akaniambia: “Mwana wa binadamu, Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Hii ndiyo miongozo ya kufuata madhabahu inapotengenezwa, ili dhabihu nzima za kuteketezwa zitolewe na damu inyunyizwe juu yake.’+

19 “‘Utawapa makuhani Walawi wazao wa Sadoki+ wanaonikaribia ili kunihudumia ng’ombe dume mchanga wa kundi kwa ajili ya dhabihu ya dhambi,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. 20 ‘Unapaswa kuchukua kiasi fulani cha damu yake na kuitia kwenye zile pembe nne za madhabahu, juu ya ncha nne za kidato kinachozunguka pande zote, na juu ya ukingo unaozunguka pande zote, ili kuitakasa kutokana na dhambi na kufunika dhambi yake.+ 21 Kisha utamchukua yule ng’ombe dume mchanga, ile dhabihu ya dhambi, ili umteketeze mahali palipochaguliwa pa hekalu, nje ya patakatifu.+ 22 Katika siku ya pili utatoa mbuzi dume ambaye hana kasoro kwa ajili ya dhabihu ya dhambi; nao wataitakasa madhabahu kutokana na dhambi kama walivyoitakasa kutokana na dhambi kwa kutumia yule ng’ombe dume mchanga.’

23 “‘Utakapomaliza kuitakasa kutokana na dhambi, utatoa ng’ombe dume mchanga wa kundi ambaye hana kasoro na kondoo dume wa kundi ambaye hana kasoro. 24 Nawe utawaleta kwa Yehova, na makuhani watawanyunyizia chumvi+ na kuwatoa kwa Yehova wakiwa dhabihu nzima ya kuteketezwa. 25 Kwa siku saba utamtoa mbuzi dume kwa ajili ya dhabihu ya dhambi kila siku,+ pia ng’ombe dume mchanga wa mifugo, na kondoo dume kutoka katika kundi; utawatoa wanyama ambao hawana kasoro.* 26 Kwa siku saba watafunika dhambi ya madhabahu, nao wataitakasa na kuiweka tayari. 27 Baada ya siku hizo kwisha, siku ya nane+ na kuendelea, kuhani atatoa dhabihu zenu* nzima za kuteketezwa na dhabihu za ushirika kwenye madhabahu; nami nitafurahishwa nanyi,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki