Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ezekieli 7
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Ezekieli—Yaliyomo

      • Mwisho umefika (1-27)

        • Msiba wa pekee (5)

        • Pesa zatupwa barabarani (19)

        • Hekalu litatiwa unajisi (22)

Ezekieli 7:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kukufanya uwajibike.”

Ezekieli 7:4

Marejeo

  • +Eze 5:11
  • +Yer 16:18; Eze 16:43
  • +Eze 6:13

Ezekieli 7:5

Marejeo

  • +2Fa 21:12; Da 9:12

Ezekieli 7:6

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “utaamka.”

Ezekieli 7:7

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “Shada lako la maua limefika.”

Marejeo

  • +Sef 1:14

Ezekieli 7:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kukufanya uwajibike.”

Marejeo

  • +2Nya 34:21
  • +Yer 7:20; Eze 5:13

Ezekieli 7:9

Marejeo

  • +Yer 13:14
  • +Isa 66:6; Eze 33:29

Ezekieli 7:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “Shada lako la maua limefika.”

Marejeo

  • +Sef 1:14

Ezekieli 7:11

Marejeo

  • +Isa 59:6; Yer 6:7; Mik 6:12

Ezekieli 7:12

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, wale wanaonunua mali na pia wale wanaouza hawatafaidika, kwa maana wote wataangamizwa.

Marejeo

  • +Sef 1:18

Ezekieli 7:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “kwa kosa lake.”

Ezekieli 7:14

Marejeo

  • +Yer 4:5
  • +Yer 7:20; 12:12

Ezekieli 7:15

Marejeo

  • +Law 26:25
  • +Yer 14:18; Eze 5:12

Ezekieli 7:16

Marejeo

  • +Isa 59:11

Ezekieli 7:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, watajikojolea kwa sababu ya woga.

Marejeo

  • +Eze 21:7

Ezekieli 7:18

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “wamefunikwa na hofu.”

  • *

    Yaani, vichwa vyao vitanyolewa kwa sababu ya maombolezo.

Marejeo

  • +Isa 3:24
  • +Isa 22:12

Ezekieli 7:19

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Nafsi zao hazitashiba.”

  • *

    Yaani, fedha yao na dhahabu yao.

Marejeo

  • +Met 11:4; Sef 1:18

Ezekieli 7:20

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, mapambo ya dhahabu na fedha.

Marejeo

  • +2Fa 21:1, 7; Yer 7:30

Ezekieli 7:21

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, fedha yao na dhahabu yao waliyotumia kutengeneza sanamu.

Ezekieli 7:22

Maelezo ya Chini

  • *

    Inaonekana ni sehemu ya ndani zaidi ya mahali patakatifu pa Yehova.

Marejeo

  • +Yer 18:17
  • +2Nya 36:19; Omb 1:10

Ezekieli 7:23

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, minyororo ya utekwa.

Marejeo

  • +Yer 39:6, 7; Omb 3:7
  • +2Fa 21:16; 24:3, 4; Yer 2:34; Eze 9:9
  • +Isa 59:6; Mik 2:2

Ezekieli 7:24

Marejeo

  • +Kum 28:48-51; Eze 21:31; Hab 1:6
  • +Yer 6:12; Omb 5:2
  • +Eze 21:2

Ezekieli 7:25

Marejeo

  • +Isa 57:21; Yer 8:15

Ezekieli 7:26

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “mafundisho yatatoweka.”

  • *

    Au “mashauri.”

Marejeo

  • +Yer 21:1, 2; 37:17
  • +Zb 74:9; Omb 2:9; Eze 20:3

Ezekieli 7:27

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “ukiwa.”

Marejeo

  • +Yer 52:10
  • +Eze 6:13

Jumla

Eze. 7:4Eze 5:11
Eze. 7:4Yer 16:18; Eze 16:43
Eze. 7:4Eze 6:13
Eze. 7:52Fa 21:12; Da 9:12
Eze. 7:7Sef 1:14
Eze. 7:82Nya 34:21
Eze. 7:8Yer 7:20; Eze 5:13
Eze. 7:9Yer 13:14
Eze. 7:9Isa 66:6; Eze 33:29
Eze. 7:10Sef 1:14
Eze. 7:11Isa 59:6; Yer 6:7; Mik 6:12
Eze. 7:12Sef 1:18
Eze. 7:14Yer 4:5
Eze. 7:14Yer 7:20; 12:12
Eze. 7:15Law 26:25
Eze. 7:15Yer 14:18; Eze 5:12
Eze. 7:16Isa 59:11
Eze. 7:17Eze 21:7
Eze. 7:18Isa 3:24
Eze. 7:18Isa 22:12
Eze. 7:19Met 11:4; Sef 1:18
Eze. 7:202Fa 21:1, 7; Yer 7:30
Eze. 7:22Yer 18:17
Eze. 7:222Nya 36:19; Omb 1:10
Eze. 7:23Yer 39:6, 7; Omb 3:7
Eze. 7:232Fa 21:16; 24:3, 4; Yer 2:34; Eze 9:9
Eze. 7:23Isa 59:6; Mik 2:2
Eze. 7:24Kum 28:48-51; Eze 21:31; Hab 1:6
Eze. 7:24Yer 6:12; Omb 5:2
Eze. 7:24Eze 21:2
Eze. 7:25Isa 57:21; Yer 8:15
Eze. 7:26Yer 21:1, 2; 37:17
Eze. 7:26Zb 74:9; Omb 2:9; Eze 20:3
Eze. 7:27Yer 52:10
Eze. 7:27Eze 6:13
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Ezekieli 7:1-27

Ezekieli

7 Neno la Yehova likanijia tena likisema: 2 “Nawe Mwana wa binadamu, hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anavyoiambia nchi ya Israeli: ‘Mwisho! Mwisho umezifikia pembe nne za nchi. 3 Sasa mwisho umekufikia, nami nitakumwagia hasira yangu, nami nitakuhukumu kulingana na njia zako na kukuadhibu* kwa sababu ya matendo yako yote yanayochukiza. 4 Jicho langu halitakusikitikia; wala sitakuhurumia,+ kwa maana nitakuletea matokeo ya njia zako mwenyewe, nawe utapatwa na madhara ya matendo yako yanayochukiza.+ Nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’+

5 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Tazama! Msiba, msiba wa pekee, unakuja.+ 6 Mwisho unakuja; mwisho utakuja; utainuka* wenyewe dhidi yako. Tazama! Unakuja. 7 Zamu yako imefika,* wewe unayekaa nchini. Wakati unakuja, siku hiyo iko karibu.+ Kuna vurugu, wala si kelele za shangwe milimani.

8 “‘Hivi karibuni nitakumwagia ghadhabu yangu,+ nami nitakumwagia hasira yangu yote,+ nami nitakuhukumu kulingana na njia zako na kukuadhibu* kwa sababu ya matendo yako yote yanayochukiza. 9 Jicho langu halitakusikitikia; wala sitakuhurumia.+ Kwa maana nitakuletea matokeo ya njia zako mwenyewe, nawe utapatwa na madhara ya matendo yako mwenyewe yanayochukiza. Nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi, Yehova, ndiye ninayewapiga.+

10 “‘Tazama, ile siku! Tazama, inakuja!+ Zamu yako imefika;* fimbo imechanua na kimbelembele kimechipuka. 11 Ukatili umesitawi na kuwa fimbo ya uovu.+ Wao wenyewe, mali yao, umati wao, wala umashuhuri wao hautaokoka. 12 Wakati utakuja, siku hiyo itafika. Mnunuzi asishangilie, na muuzaji asiomboleze, kwa maana kuna ghadhabu dhidi ya umati wao wote.*+ 13 Kwa maana muuzaji hatakirudia kitu alichouza, hata uhai wake ukiokolewa, kwa maana maono hayo yanahusu umati wote. Hakuna atakayerudi, na kwa sababu ya kosa lake,* hakuna atakayeokoa uhai wake.

14 “‘Wamepiga tarumbeta+ na kila mtu yuko tayari, lakini hakuna anayeenda vitani, kwa sababu nina ghadhabu dhidi ya umati wote.+ 15 Upanga uko nje,+ na ugonjwa hatari na njaa kali zimo ndani. Yeyote aliye uwanjani atakufa kwa upanga, na njaa kali na ugonjwa hatari vitawameza wale walio jijini.+ 16 Watu wao watakaofanikiwa kuponyoka wataenda milimani, na kama njiwa wa mabondeni, kila mmoja ataomboleza kwa sababu ya kosa lake.+ 17 Mikono yao yote italegea, na magoti yao yote yatadondosha maji.*+ 18 Wamevaa nguo za magunia,+ nao wanatetemeka.* Kila mtu ataaibishwa, na kila kichwa kitakuwa na upara.*+

19 “‘Watatupa fedha yao barabarani, nayo dhahabu yao itawachukiza. Wala fedha yao wala dhahabu yao haitaweza kuwaokoa katika siku ya ghadhabu ya Yehova.+ Hawatashiba,* wala kuyajaza matumbo yao, kwa maana vitu hivyo* vimekuwa kikwazo kinachosababisha kosa lao. 20 Walijivunia urembo wa mapambo yao, nao wakayatumia* kutengeneza mifano yao inayochukiza, sanamu zao zinazochukiza.+ Ndiyo sababu nitaifanya fedha na dhahabu yao kuwa chukizo kwao. 21 Nami nitaitia* mikononi mwa wageni ili waipore na kuwapa waovu wa dunia kuwa nyara, nao wataitia unajisi.

22 “‘Nami nitaugeuza uso wangu kutoka kwao,+ nao watapatia unajisi mahali pangu palipofichika,* na wanyang’anyi wataingia mahali hapo na kupatia unajisi.+

23 “‘Tengeneza mnyororo,*+ kwa maana nchi imejaa hukumu yenye madoa ya damu+ na jiji limejaa ukatili.+ 24 Nami nitaingiza mataifa mabaya kabisa,+ nayo yatamiliki nyumba zao,+ nami nitakikomesha kiburi cha wenye nguvu, na mahali pao patakatifu patatiwa unajisi.+ 25 Maumivu yao yatakapokuja, watatafuta amani lakini haitakuwepo.+ 26 Msiba utakuja juu ya msiba, na habari baada ya habari, na watu watatafuta maono kutoka kwa nabii,+ lakini sheria itatoweka* kutoka kwa kuhani na ushauri* kutoka kwa wazee.+ 27 Mfalme ataomboleza,+ naye mkuu atavaa kukata tamaa,* na mikono ya watu wa nchi itatetemeka kwa hofu. Nitawatendea kulingana na njia zao, nami nitawahukumu kama walivyohukumu. Nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’”+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki