Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ezekieli 8
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Ezekieli—Yaliyomo

      • Ezekieli apelekwa Yerusalemu katika maono (1-4)

      • Vitu vinavyochukiza vyaonekana hekaluni (5-18)

        • Wanawake wakimlilia Tamuzi (14)

        • Wanaume wakiabudu jua (16)

Ezekieli 8:2

Marejeo

  • +Da 7:9
  • +Eze 1:4, 27

Ezekieli 8:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “mfano wa.”

Marejeo

  • +Yer 20:2; Eze 9:2
  • +Kum 32:16

Ezekieli 8:4

Marejeo

  • +Kut 40:34
  • +Eze 1:27, 28

Ezekieli 8:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “mfano huu wa.”

Ezekieli 8:6

Marejeo

  • +2Nya 36:14
  • +Yer 26:4, 6

Ezekieli 8:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Huenda neno la Kiebrania linahusiana na neno “mavi,” nalo hutumiwa kuonyesha dharau.

Marejeo

  • +Law 11:10
  • +Kut 20:4, 5

Ezekieli 8:11

Marejeo

  • +2Fa 22:3, 4; 25:22; Yer 26:24
  • +Eze 16:17, 18

Ezekieli 8:12

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “katika vyumba vya ndani vya sanamu yake bora?”

Marejeo

  • +Isa 29:15; Eze 9:9

Ezekieli 8:15

Marejeo

  • +2Nya 36:14

Ezekieli 8:16

Marejeo

  • +2Nya 4:9
  • +Kum 4:19; 2Fa 17:16; Yer 8:1, 2

Ezekieli 8:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Inaonekana ni tawi lililotumiwa katika ibada ya sanamu.

Marejeo

  • +2Fa 21:16; Yer 19:4; Eze 9:9

Ezekieli 8:18

Marejeo

  • +Eze 5:11; 7:9
  • +Isa 1:15; Mik 3:4

Jumla

Eze. 8:2Da 7:9
Eze. 8:2Eze 1:4, 27
Eze. 8:3Yer 20:2; Eze 9:2
Eze. 8:3Kum 32:16
Eze. 8:4Kut 40:34
Eze. 8:4Eze 1:27, 28
Eze. 8:62Nya 36:14
Eze. 8:6Yer 26:4, 6
Eze. 8:10Law 11:10
Eze. 8:10Kut 20:4, 5
Eze. 8:112Fa 22:3, 4; 25:22; Yer 26:24
Eze. 8:11Eze 16:17, 18
Eze. 8:12Isa 29:15; Eze 9:9
Eze. 8:152Nya 36:14
Eze. 8:162Nya 4:9
Eze. 8:16Kum 4:19; 2Fa 17:16; Yer 8:1, 2
Eze. 8:172Fa 21:16; Yer 19:4; Eze 9:9
Eze. 8:18Eze 5:11; 7:9
Eze. 8:18Isa 1:15; Mik 3:4
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Ezekieli 8:1-18

Ezekieli

8 Na katika mwaka wa sita, mwezi wa sita, siku ya tano ya mwezi huo, nilipokuwa nimeketi nyumbani mwangu na wazee wa Yuda walipokuwa wameketi mbele yangu, mkono wa Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova ulinishika nikiwa hapo. 2 Nilipokuwa nikitazama, niliona umbo lililoonekana kama moto; kulikuwa na moto chini ya kitu kilichoonekana kama kiuno chake,+ na kuanzia kiuno chake kwenda juu, mwonekano wake uling’aa kama mchanganyiko wa dhahabu na fedha.+ 3 Kisha akanyoosha kitu kilichoonekana kama mkono na kuniinua kwa kishungi cha nywele za kichwa changu, na roho ikanibeba katikati ya dunia na mbingu na kunileta Yerusalemu kupitia maono kutoka kwa Mungu, kwenye njia inayoelekea kwenye lango la ndani+ linalotazama kaskazini, mahali ilipokuwa ishara ya* ibada ya sanamu inayochochea wivu.+ 4 Na tazama! utukufu wa Mungu wa Israeli ulikuwa hapo,+ kama mwonekano niliokuwa nimeuona katika bonde tambarare.+

5 Kisha akaniambia: “Mwana wa binadamu, tafadhali inua macho yako kuelekea kaskazini.” Basi nikainua macho yangu kuelekea kaskazini, na huko, upande wa kaskazini wa lango la madhabahu kulikuwa na ishara hii ya* wivu langoni. 6 Naye akaniambia: “Mwana wa binadamu, je, unaona mambo mabaya sana na yenye kuchukiza ambayo watu wa nyumba ya Israeli wanafanya hapa,+ mambo yanayonifanya niende mbali sana na mahali pangu patakatifu?+ Lakini utaona mambo yanayochukiza yaliyo mabaya hata zaidi.”

7 Kisha akanileta kwenye mlango wa ua, nami nilipotazama, niliona tundu ukutani. 8 Akaniambia: “Mwana wa binadamu, tafadhali toboa ukuta.” Nami nikautoboa ukuta na kuona mlango. 9 Akaniambia: “Ingia ndani uone mambo maovu na yenye kuchukiza wanayofanya hapa.” 10 Basi nikaingia na kutazama, nikaona mifano mbalimbali ya viumbe wanaotambaa na wanyama wanaochukiza+ na sanamu zote zinazochukiza* za watu wa nyumba ya Israeli;+ zilikuwa zimechongwa ukutani kuzunguka pande zote. 11 Na wazee 70 wa nyumba ya Israeli walikuwa wamesimama mbele ya vitu hivyo, naye Yaazania mwana wa Shafani+ alikuwa amesimama miongoni mwao. Kila mmoja wao alikuwa na chetezo chake mkononi mwake, na wingu la uvumba lenye manukato lilikuwa likipanda juu.+ 12 Akaniambia: “Mwana wa binadamu, je, umeona mambo ambayo wazee wa nyumba ya Israeli wanafanya gizani, kila mmoja akiwa katika vyumba vya ndani ambamo sanamu zake za kuchongwa zimewekwa ili zionekane?* Kwa maana wanasema, ‘Yehova hatuoni. Yehova ameiacha nchi hii.’”+

13 Naye akaendelea kuniambia: “Utaona mambo yanayochukiza yaliyo mabaya hata zaidi ambayo wanafanya.” 14 Basi akanileta kwenye njia inayoelekea kwenye lango la kaskazini la nyumba ya Yehova, na huko nikaona wanawake wameketi wakimlilia mungu Tamuzi.

15 Naye akaendelea kuniambia: “Je, unaona mambo haya, ewe mwana wa binadamu? Utaona mambo yanayochukiza ambayo ni mabaya hata zaidi kuliko haya.”+ 16 Basi akanileta katika ua wa ndani wa nyumba ya Yehova.+ Hapo kwenye mlango wa hekalu la Yehova, katikati ya ukumbi na madhabahu, kulikuwa na wanaume 25 hivi ambao migongo yao ilielekea hekalu la Yehova na nyuso zao zilitazama mashariki; nao walikuwa wakiliinamia jua kuelekea mashariki.+

17 Akaniambia: “Mwana wa binadamu, je, unaona hili? Je, ni jambo dogo sana kwa watu wa nyumba ya Yuda kufanya mambo haya yanayochukiza, kuijaza nchi ukatili+ na kuendelea kunikasirisha? Tazama, wanaidunga pua yangu kwa lile tawi.* 18 Basi nitatenda kwa ghadhabu. Jicho langu halitasikitika; wala sitawahurumia.+ Hata wakilia kwa sauti kubwa masikioni mwangu, sitawasikia.”+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki