Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ezekieli 9
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Ezekieli—Yaliyomo

      • Wanaume sita wanaoangamiza na mwanamume mwenye kidau cha wino (1-11)

        • Hukumu itaanzia patakatifu (6)

Ezekieli 9:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “chombo cha kuwekea wino cha mwandishi.”

Marejeo

  • +Yer 20:2; Eze 8:3
  • +2Nya 4:1

Ezekieli 9:3

Marejeo

  • +Eze 3:23; 8:3, 4; 11:22
  • +Eze 10:4

Ezekieli 9:4

Marejeo

  • +Zb 119:53; 2Pe 2:7, 8
  • +Eze 5:11

Ezekieli 9:5

Marejeo

  • +Kut 32:26, 27; Eze 7:4

Ezekieli 9:6

Marejeo

  • +2Nya 36:17
  • +Kut 12:23; Yos 2:17-19; Ufu 9:4
  • +2Fa 25:18, 21; Yer 25:29
  • +Eze 8:11

Ezekieli 9:7

Marejeo

  • +Omb 2:21

Ezekieli 9:8

Marejeo

  • +Mwa 18:23; Eze 11:13

Ezekieli 9:9

Marejeo

  • +2Nya 36:14; Isa 1:4
  • +2Fa 21:16; Yer 2:34; Mt 23:30
  • +Eze 22:29
  • +Isa 29:15; Eze 8:12

Ezekieli 9:10

Marejeo

  • +Eze 5:11; 7:4

Jumla

Eze. 9:2Yer 20:2; Eze 8:3
Eze. 9:22Nya 4:1
Eze. 9:3Eze 3:23; 8:3, 4; 11:22
Eze. 9:3Eze 10:4
Eze. 9:4Zb 119:53; 2Pe 2:7, 8
Eze. 9:4Eze 5:11
Eze. 9:5Kut 32:26, 27; Eze 7:4
Eze. 9:62Nya 36:17
Eze. 9:6Kut 12:23; Yos 2:17-19; Ufu 9:4
Eze. 9:62Fa 25:18, 21; Yer 25:29
Eze. 9:6Eze 8:11
Eze. 9:7Omb 2:21
Eze. 9:8Mwa 18:23; Eze 11:13
Eze. 9:92Nya 36:14; Isa 1:4
Eze. 9:92Fa 21:16; Yer 2:34; Mt 23:30
Eze. 9:9Eze 22:29
Eze. 9:9Isa 29:15; Eze 8:12
Eze. 9:10Eze 5:11; 7:4
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Ezekieli 9:1-11

Ezekieli

9 Kisha nikamsikia akisema hivi kwa sauti kubwa: “Waiteni wale watakaoliadhibu jiji hili, kila mmoja wao akiwa na silaha yake ya kuangamiza mkononi mwake!”

2 Nikaona wanaume sita wakija kutoka upande wa lango la juu+ linalotazama kaskazini, kila mmoja akiwa na silaha yake ya kuponda mkononi mwake; na kulikuwa na mwanamume mmoja kati yao aliyevaa kitani, akiwa na kidau cha wino cha mwandishi kiunoni,* nao wakaingia ndani na kusimama kando ya madhabahu ya shaba.+

3 Kisha utukufu wa Mungu wa Israeli+ ukainuka kutoka mahali ulipokuwa umetulia juu ya makerubi na kwenda kwenye kizingiti cha mlango wa nyumba hiyo,+ naye akaanza kumwita kwa sauti yule mwanamume aliyevaa kitani, ambaye alikuwa na kidau cha wino cha mwandishi kiunoni. 4 Yehova akamwambia: “Pita kotekote jijini, katika jiji lote la Yerusalemu, nawe uyatie alama mapaji ya nyuso za watu wanaolia kwa uchungu na kwa maumivu makali+ kwa sababu ya mambo yote yanayochukiza yanayofanywa jijini.”+

5 Naye akawaambia wale wengine huku nikisikia: “Piteni kotekote jijini baada yake na kuua. Jicho lenu lisisikitike, wala msiwe na huruma hata kidogo.+ 6 Mnapaswa kuwaua wote kabisa, mzee, kijana, bikira, mtoto mdogo, na wanawake.+ Lakini msimkaribie mtu yeyote aliye na ile alama.+ Mnapaswa kuanzia mahali pangu patakatifu.”+ Kwa hiyo wakaanza na wale wazee waliokuwa mbele ya ile nyumba.+ 7 Kisha akawaambia: “Itieni nyumba unajisi na kuzijaza nyua wale waliouawa.+ Nendeni!” Basi wakaenda na kuwaua watu jijini.

8 Walipokuwa wakiwaua, nilibaki mimi peke yangu, nikaanguka kifudifudi na kupaza sauti: “Ole wangu, Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova! Je, utawaangamiza Waisraeli wote wanaobaki unapolimwagia ghadhabu yako jiji la Yerusalemu?”+

9 Basi akaniambia: “Kosa la watu wa nyumba ya Israeli na Yuda ni kubwa sana, kubwa kwelikweli.+ Nchi imejaa umwagaji wa damu,+ nalo jiji limejaa ufisadi.+ Kwa maana wanasema, ‘Yehova ameiacha nchi hii, na Yehova haoni.’+ 10 Lakini mimi, jicho langu halitasikitika; wala sitawahurumia.+ Nitawaletea madhara ya njia yao juu ya kichwa chao wenyewe.”

11 Ndipo nikamwona yule mwanamume aliyevaa kitani, ambaye alikuwa na kidau cha wino kiunoni, akirudi na kuleta habari akisema: “Nimefanya kama ulivyoniamuru.”

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki