Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Hosea 4
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Hosea—Yaliyomo

      • Kesi ya Yehova dhidi ya Waisraeli (1-8)

        • Watu hawamjui Mungu nchini (1)

      • Waisraeli waabudu sanamu na kufanya ukahaba (9-19)

        • Wapotoshwa na roho ya ukahaba (12)

Hosea 4:1

Marejeo

  • +Mik 6:2
  • +Mik 7:2

Hosea 4:2

Marejeo

  • +Ho. 11:12
  • +1Fa 21:18, 19
  • +Eze 23:37
  • +Ho. 1:4; 6:8, 9

Hosea 4:3

Marejeo

  • +Amo 8:7, 8

Hosea 4:4

Marejeo

  • +Amo 5:10, 13
  • +Kum 17:12

Hosea 4:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “nitamwangamiza.”

Hosea 4:6

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “wataangamizwa.”

  • *

    Au “mafundisho.”

Marejeo

  • +Yer 2:8
  • +2Fa 17:15, 16

Hosea 4:7

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, makuhani.

  • *

    Au labda, “Wameniaibisha badala ya kunitukuza.”

Marejeo

  • +Ezr 9:6, 7

Hosea 4:9

Marejeo

  • +Amo 3:1, 2

Hosea 4:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Watakuwa waasherati kupindukia; Watafanya umalaya.”

Marejeo

  • +Law 26:26; Mik 6:14
  • +Ho. 9:11, 12

Hosea 4:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Umalaya.”

  • *

    Tnn., “Huondoa moyo.”

Marejeo

  • +Met 20:1; 23:31, 33; Isa 28:7

Hosea 4:12

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “fimbo yao ya ubashiri.”

  • *

    Au “umalaya.”

  • *

    Au “umalaya.”

Hosea 4:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “umalaya.”

Marejeo

  • +Yer 3:6
  • +2Fa 17:10-12; Yer 2:20; Eze 20:28

Hosea 4:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “umalaya.”

Marejeo

  • +Yer 4:22

Hosea 4:15

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “umalaya.”

Marejeo

  • +Eze 23:4, 5
  • +2Fa 17:18
  • +Ho. 9:15; 12:11; Amo 4:4
  • +Ho. 5:8; 10:5
  • +Isa 48:1; Yer 5:2; Eze 20:39

Hosea 4:16

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “mahali penye nafasi ya kutosha.”

Marejeo

  • +Zb 78:8; 81:11, 12; Zek 7:11, 12

Hosea 4:17

Marejeo

  • +Ho. 11:2; 13:1, 2

Hosea 4:18

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Pombe yao ya ngano.”

  • *

    Au “Wanafanya uasherati kupindukia; Wanafanya ukahaba.”

  • *

    Tnn., “ngao zao.”

Marejeo

  • +Mik 7:3

Hosea 4:19

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “utawafagilia mbali.”

Jumla

Hos. 4:1Mik 6:2
Hos. 4:1Mik 7:2
Hos. 4:2Ho. 11:12
Hos. 4:21Fa 21:18, 19
Hos. 4:2Eze 23:37
Hos. 4:2Ho. 1:4; 6:8, 9
Hos. 4:3Amo 8:7, 8
Hos. 4:4Amo 5:10, 13
Hos. 4:4Kum 17:12
Hos. 4:6Yer 2:8
Hos. 4:62Fa 17:15, 16
Hos. 4:7Ezr 9:6, 7
Hos. 4:9Amo 3:1, 2
Hos. 4:10Law 26:26; Mik 6:14
Hos. 4:10Ho. 9:11, 12
Hos. 4:11Met 20:1; 23:31, 33; Isa 28:7
Hos. 4:13Yer 3:6
Hos. 4:132Fa 17:10-12; Yer 2:20; Eze 20:28
Hos. 4:14Yer 4:22
Hos. 4:15Eze 23:4, 5
Hos. 4:152Fa 17:18
Hos. 4:15Ho. 9:15; 12:11; Amo 4:4
Hos. 4:15Ho. 5:8; 10:5
Hos. 4:15Isa 48:1; Yer 5:2; Eze 20:39
Hos. 4:16Zb 78:8; 81:11, 12; Zek 7:11, 12
Hos. 4:17Ho. 11:2; 13:1, 2
Hos. 4:18Mik 7:3
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Hosea 4:1-19

Hosea

4 Lisikieni neno la Yehova, enyi Waisraeli,

Kwa maana Yehova ana kesi dhidi ya wakaaji wa nchi,+

Kwa sababu hakuna ukweli wala upendo mshikamanifu wala ujuzi kumhusu Mungu nchini.+

 2 Viapo vya uwongo na udanganyifu+ na mauaji+

Na wizi na uzinzi+ umeenea sana,

Na tendo moja la umwagaji wa damu linafuata tendo lingine la umwagaji wa damu.+

 3 Ndiyo sababu nchi itaomboleza+

Na kila mkaaji nchini atadhoofika;

Wanyama wa mwituni na ndege wa angani,

Hata samaki wa baharini, wataangamia.

 4 “Hata hivyo, mtu yeyote asibishane nanyi wala kuwakaripia,+

Kwa maana watu wenu ni kama wale wanaobishana na kuhani.+

 5 Basi mtajikwaa kweupe kabisa wakati wa mchana,

Na nabii atajikwaa pamoja nanyi, kana kwamba ni usiku.

Nami nitamnyamazisha* mama yenu.

 6 Watu wangu watanyamazishwa,* kwa sababu hawana ujuzi.

Kwa sababu mmekataa ujuzi,+

Nitawakataa pia msinitumikie mkiwa makuhani wangu;

Na kwa sababu mmesahau sheria* ya Mungu wenu,+

Mimi mwenyewe nitawasahau wana wenu.

 7 Kadiri walivyoongezeka,* ndivyo walivyozidi kunitendea dhambi.+

Nitabadili utukufu wao uwe aibu.*

 8 Wanajilisha dhambi ya watu wangu,

Nao wana pupa ya kuona watu wangu wakikosea.

 9 Yatakayowapata watu ndiyo yatakayompata kuhani;

Nitawafanya wawajibike kwa sababu ya njia zao,

Nami nitawaletea matokeo ya matendo yao.+

10 Watakula lakini hawatashiba.+

Watafanya ngono ovyovyo,* lakini hawataongezeka,+

Kwa sababu hawajamheshimu Yehova.

11 Ukahaba* na divai na divai mpya

Huondoa kichocheo cha kutenda lililo jema.*+

12 Watu wangu hutafuta ushauri kutoka kwa sanamu zao za miti,

Wakifanya mambo wanayoambiwa na fimbo yao;*

Kwa sababu roho ya ukahaba* huwapotosha,

Na kwa ukahaba* wao wanakataa kujinyenyekeza kwa Mungu wao.

13 Wanatoa dhabihu juu ya vilele vya milima,+

Na juu ya vilima wanafukiza moshi wa dhabihu,

Chini ya mialoni na milubna na kila mti mkubwa,+

Kwa sababu vivuli vyake ni vizuri.

Ndiyo sababu mabinti wenu wanafanya ukahaba*

Na mabinti wakwe zenu wanafanya uzinzi.

14 Sitawafanya mabinti wenu wawajibike kwa sababu ya ukahaba* wao,

Wala mabinti wakwe zenu kwa sababu ya uzinzi wao.

Kwa maana wanaume huwatafuta makahaba

Nao hutoa dhabihu pamoja na makahaba wa hekaluni;

Watu kama hao wasio na uelewaji+ wataangamia.

15 Ingawa mnafanya ukahaba,* enyi Waisraeli,+

Watu wa Yuda wasiwe na hatia.+

Msije Gilgali+ wala Beth-aveni,+

Na msiape mkisema, ‘Kwa hakika kama Yehova anavyoishi!’+

16 Waisraeli wamekuwa wakaidi kama ng’ombe mkaidi.+

Je, sasa Yehova atawachunga kama mwanakondoo dume malishoni?*

17 Waefraimu wameshikamana na sanamu.+

Waacheni!

18 Pombe yao* inapomalizika,

Wanafanya ngono ovyovyo.*

Na watawala wao* hupenda sana aibu.+

19 Upepo utawafunga katika mabawa yake,*

Nao watazionea aibu dhabihu zao.”

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki