WIMBO NA. 114
“Iweni na Subira”
- 1. Yehova, Baba yetu, - Anapenda jina lake. - Ataka litakaswe, - Lawama liondolewe. - Kavumilia mengi, - Tena muda mrefu; - Ana subira nyingi, - Hajachoka kamwe. - Ataka watu wote - Wapate kuokolewa. - Aonyesha subira, - Kwa faida yetu sote. 
- 2. Nasi tunahitaji, - Kuionyesha subira. - Ghadhabu tuepuke. - Tukae kwa utulivu. - Tuzingatie mema, - Wafanyayo wengine. - Tutumaini mema, - Japo matatizo. - Na sifa za Kikristo, - Tuonyeshe sikuzote. - Na kwa kufanya hivyo, - Tumuige Mungu wetu. 
(Ona pia Kut. 34:14; Isa. 40:28; 1 Kor. 13:4, 7; 1 Tim. 2:4.)