WIMBO NA. 28
Kuwa Rafiki ya Yehova
- 1. Nani rafikiyo? - Akaaye kwako? - Nani ambaye wamwamini? - Nani akujua? - Washikao Neno, - Wakuaminio, - Watenda haki na walio - washikamanifu. 
- 2. Nani awezaye - kukukaribia? - Umpendaye na ambaye - wamjua jina? - Wanaokusifu, - Wanaokutii, - Wote wa’minifu moyoni, - Wasemao kweli. 
- 3. Twakumiminia - yaliyo moyoni. - Unatuvuta, Watupenda, - Nawe watutunza. - Rafikizo wewe, - tunataka tuwe. - Wewe ni Rafiki mkuu, - hakuna mwingine. 
(Ona pia Zab. 139:1; 1 Pet. 5:6, 7.)