WIMBO NA. 8
Yehova Ni Kimbilio Letu
- 1. Yehova, kimbilio, - Ndiye twatumai. - Yeye ni ngome yetu; - Kwake twajificha. - Mungu atatuokoa, - Kamwe hatutaogopa. - Yehova, kimbilio, - Kwa waadilifu wote. 
- 2. Maelfu waanguka, - Kando yetu sisi. - Kati ya wa’dilifu, - Kuna usalama. - Hatuna hofu moyoni, - Dhara halitatupata. - Chini ya mbawa zake, - Yehova atatulinda. 
- 3. Yehova yuko nasi, - Hatutajikwaa. - Vitisho, hatuhofu, - Hatubabaiki. - Mwana-simba hatuhofu; - Nyoka tutamkanyaga. - Yehova, kimbilio, - Atuongoza milele. 
(Ona pia Zab. 97:10; 121:3, 5; Isa. 52:12.)