WIMBO NA. 57
Kuwahubiria Watu wa Namna Zote
- 1. Twatamani kumwiga Yehova, - Mungu asiye na ubaguzi. - Ni mapenzi yake watu wote, - Wapate uzima wa milele. - (KORASI) - Hatutazami sura; - Wala hali za watu. - Twatangazia wote ujumbe. - Kwa kuwa twawajali, - Twawakaribisha wote, - Wawe rafiki za Yehova. 
- 2. Haidhuru wapatikanapo, - Wanavyoonekana mwanzoni. - La muhimu, walivyo moyoni— - Alivyo yule mtu wa ndani. - (KORASI) - Hatutazami sura; - Wala hali za watu. - Twatangazia wote ujumbe. - Kwa kuwa twawajali, - Twawakaribisha wote, - Wawe rafiki za Yehova. 
- 3. Yehova awapa wote fursa, - Waache njia za ulimwengu. - Tuna hamu kujulisha wengi, - Basi tuwahubirie wote. - (KORASI) - Hatutazami sura; - Wala hali za watu. - Twatangazia wote ujumbe. - Kwa kuwa twawajali, - Twawakaribisha wote, - Wawe rafiki za Yehova. 
(Ona pia Yoh. 12:32; Mdo. 10:34; 1 Tim. 4:10; Tit. 2:11.)