Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb 7
  • Mnara wa Babeli

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mnara wa Babeli
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Safina ya Noa
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb 7
Baada ya Yehova kuvuruga lugha, watu hawakuweza tena kujenga pamoja Mnara wa Babeli

SOMO LA 7

Mnara wa Babeli

Baada ya Gharika, wana wa Noa na wake zao walizaa watoto wengi. Watu waliongezeka na kuenea duniani, kama Yehova alivyokuwa amewaagiza.

Lakini baadhi ya watu hawakumtii Yehova. Walisema: ‘Acheni tujenge jiji na kukaa pamoja. Tutajenga mnara mrefu sana na kilele chake kitafika mbinguni. Kisha, tutakuwa watu mashuhuri.’

Yehova hakupendezwa na mambo ambayo watu hao walifanya, hivyo aliamua kusimamisha ujenzi huo. Je, unajua alifanya hivyo jinsi gani? Yehova alifanya watu hao wazungumze lugha mbalimbali. Kwa kuwa hawakuelewana, ujenzi ulikoma. Jiji walilojenga liliitwa Babeli, jina linalomaanisha “Machafuko.” Watu walitawanyika na kuishi maeneo mbalimbali ya dunia. Hata hivyo, waliendelea kufanya mambo mabaya katika maeneo mapya walioishi. Je, kuna watu walioendelea kumpenda Yehova? Tutajifunza jambo hilo katika sura inayofuata.

“Kila mtu anayejiinua atafedheheshwa, lakini anayejinyenyekeza atainuliwa.”​—Luka 18:14

Maswali: Watu wa Babeli walifanya nini? Yehova alifanya nini ili kusimamisha mradi wao?

Mwanzo 11:1-9

    Tanzanian sign language publications (2020-2025)
    Toka
    Ingia
    • Lugha ya Alama ya Tanzania
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki