Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Samweli 16:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Lakini Yehova akamwambia Samweli: “Usiangalie sura yake wala urefu+ wa umbo lake, kwa maana nimemkataa. Kwa kuwa Mungu haoni kama mwanadamu anavyoona,+ kwa maana mwanadamu huona kile kinachoonekana kwa macho,+ lakini Yehova huona jinsi moyo+ ulivyo.”

  • Ayubu 34:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Kwa maana yeye atamlipa+ mtu wa udongo kulingana na matendo yake,

      Na kulingana na pito la mwanadamu yeye ataifanya ije juu yake.

  • Methali 24:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Ikiwa utasema: “Tazama! Hatukujua hili,”+ je, yule anayeipima mioyo hatatambua hilo,+ na yule anayeichunguza nafsi yako mwenyewe hatajua+ hilo naye hakika hatamlipa mtu wa udongo kulingana na utendaji wake?+

  • Yeremia 32:19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 mkuu katika shauri+ na mwingi katika matendo,+ wewe ambaye macho yako yamefunguliwa juu ya njia zote za wanadamu,+ ili kumpa kila mmoja kulingana na njia zake na kulingana na matunda ya matendo yake;+

  • Ezekieli 7:27
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 27 Mfalme mwenyewe ataomboleza;+ hata mkuu atajivika ukiwa,+ na mikono yenyewe ya watu wa nchi itasumbuka. Kulingana na njia yao nitatenda kuwaelekea wao,+ na kwa hukumu zao nitawahukumu wao;+ nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’ ”+

  • Waroma 2:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Naye atamlipa kila mmoja kulingana na matendo yake:+

  • 2 Wakorintho 5:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Kwa maana sisi sote lazima tufunuliwe mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo,+ ili kila mmoja apate thawabu yake kwa ajili ya mambo yaliyofanywa kupitia mwili, kulingana na mambo ambayo ametenda, kama ni mema au ni maovu.+

  • Wagalatia 6:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Msipotoshwe:+ Mungu si wa kudhihakiwa.+ Kwa maana lolote lile analopanda mtu, atavuna hilo pia;+

  • Wakolosai 3:25
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 25 Hakika yule anayetenda kosa atapokea malipo+ kwa lile kosa alilotenda, na hakuna ubaguzi wowote.+

  • 2 Timotheo 4:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Aleksanda+ yule fundi wa shaba alinitendea mimi mambo mengi mabaya—Yehova atamlipa kulingana na vitendo vyake+—

  • 1 Petro 1:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Zaidi ya hayo, ikiwa mnamwitia Baba ambaye huhukumu bila ubaguzi+ kulingana na matendo ya kila mmoja, jiendesheni kwa kuogopa+ katika wakati wa kukaa kwenu ugenini.+

  • Ufunuo 20:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Nami nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo,+ wamesimama mbele ya kile kiti cha ufalme, na vitabu vya kukunjwa vikafunguliwa. Lakini kitabu kingine cha kukunjwa kikafunguliwa; hicho ni kitabu cha uzima.+ Na wafu wakahukumiwa kutokana na mambo yale yaliyoandikwa katika vile vitabu kulingana na matendo yao.+

  • Ufunuo 22:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 “ ‘Tazama! Mimi ninakuja upesi,+ na thawabu+ ninayotoa ipo pamoja nami, ili kumlipa kila mmoja kulingana na matendo yake.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki