Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yoshua 10:8-14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Ndipo Yehova akamwambia Yoshua: “Usiwaogope,+ kwa maana nimewatia mikononi mwako.+ Hakuna mtu yeyote kati yao atakayekushinda.”+ 9 Yoshua akawashambulia ghafla baada ya kutembea usiku kucha kutoka Gilgali. 10 Yehova akawavuruga,+ na Waisraeli wakawaangamiza wengi wao kule Gibeoni, wakawafuatia kwenye njia inayopanda kwenda Beth-horoni na kuwaua mpaka Azeka na Makeda. 11 Walipokuwa wakiwakimbia Waisraeli, Yehova akawanyeshea mvua ya mawe makubwa kutoka angani kwenye mteremko wa Beth-horoni mpaka Azeka, nao wakafa. Kwa kweli, wale waliouawa na mvua ya mawe walikuwa wengi kuliko wale waliouawa na Waisraeli kwa upanga.

      12 Ni siku hiyo, siku ambayo Yehova aliwashinda kabisa Waamori mbele ya Waisraeli, ndipo Yoshua alipomwambia hivi Yehova mbele ya Waisraeli:

      “Jua, simama tuli+ juu ya Gibeoni,+

      Na mwezi, juu ya Bonde la* Aiyaloni.”

      13 Basi jua likasimama tuli na mwezi ukatulia mpaka taifa la Israeli lilipolipiza kisasi dhidi ya maadui wake. Je, haijaandikwa hivi katika kitabu cha Yashari:+ Jua lilisimama tuli katikati ya mbingu na halikutua kwa siku nzima? 14 Haijawahi kamwe kutokea siku kama hiyo, kabla au baada yake, ambayo Yehova aliisikiliza sauti ya mwanadamu+ katika njia hiyo, kwa sababu Yehova alikuwa akiwapigania Waisraeli.+

  • 2 Samweli 5:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 Basi Daudi akaenda Baal-perasimu na kuwaua huko. Ndipo akasema: “Yehova amewapasua na kuwapita+ maadui wangu mbele yangu, kama ufa uliopasuliwa na maji.” Ndiyo sababu alipaita mahali hapo Baal-perasimu.*+

  • 1 Mambo ya Nyakati 14:10-16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Daudi akamuuliza Mungu: “Je, nipande kwenda kuwashambulia Wafilisti? Je, utawatia mikononi mwangu?” Ndipo Yehova akamwambia: “Panda uende, nami hakika nitawatia mikononi mwako.”+ 11 Basi Daudi akapanda kwenda Baal-perasimu,+ naye akawaua huko. Ndipo Daudi akasema: “Mungu wa kweli amewapasua na kuwapita maadui wangu kwa mkono wangu, kama ufa uliopasuliwa na maji.” Ndiyo sababu walipaita mahali hapo Baal-perasimu.* 12 Wafilisti wakaacha miungu yao hapo, na Daudi alipotoa amri, miungu hiyo iliteketezwa motoni.+

      13 Baadaye Wafilisti wakaja tena na kuvamia bondeni.*+ 14 Daudi akamwomba Mungu ushauri tena, lakini Mungu wa kweli akamwambia: “Usipande moja kwa moja na kuwafuatia. Badala yake, zunguka nyuma yao, uwashambulie mbele ya vichaka vya mibaka.+ 15 Na utakaposikia sauti ya watu wakipiga mwendo juu ya vichaka vya mibaka, washambulie, kwa sababu mimi Mungu wa kweli nitakuwa nimetangulia mbele yako ili kuliua jeshi la Wafilisti.”+ 16 Basi Daudi akafanya kama Mungu wa kweli alivyomwamuru,+ wakaliua jeshi la Wafilisti kuanzia Gibeoni mpaka Gezeri.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki