-
Marko 3:22-27Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
22 Pia, waandishi walioshuka kutoka Yerusalemu walikuwa wakisema: “Ana Beelzebuli,* naye anawafukuza roho waovu kwa nguvu za mtawala wa roho waovu.”+ 23 Kisha akawaita na kuzungumza nao kwa mifano: “Shetani anawezaje kumfukuza Shetani? 24 Ufalme ukigawanyika dhidi yake wenyewe, hauwezi kusimama;+ 25 na nyumba ikigawanyika dhidi yake yenyewe, haiwezi kusimama. 26 Pia, ikiwa Shetani anajipinga mwenyewe na amegawanyika, hawezi kusimama, bali ataangamia. 27 Kwa kweli, hakuna yeyote anayeweza kuingia ndani ya nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuiba mali zake isipokuwa kwanza amfunge mtu huyo. Hapo ndipo atakapoweza kuipora nyumba yake.
-
-
Luka 11:15-23Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
15 Lakini baadhi yao wakasema: “Anawafukuza roho waovu kwa nguvu za Beelzebuli,* mtawala wa roho waovu.”+ 16 Na wengine, ili kumjaribu, wakamwomba afanye ishara+ kutoka mbinguni. 17 Akijua mawazo yao,+ akawaambia: “Kila ufalme uliogawanyika dhidi yake wenyewe utaangamia, na nyumba iliyogawanyika dhidi yake yenyewe itaanguka. 18 Vivyo hivyo, ikiwa Shetani amegawanyika dhidi yake mwenyewe, ufalme wake utawezaje kusimama? Kwa maana mnasema ninafukuza roho waovu kupitia Beelzebuli. 19 Ikiwa ninawafukuza roho waovu kupitia Beelzebuli, wana wenu wanawafukuza kupitia nani? Hiyo ndiyo sababu watakuwa waamuzi wenu. 20 Lakini ikiwa ninawafukuza roho waovu kupitia kidole cha Mungu,+ kwa kweli Ufalme wa Mungu umewafikia ninyi ghafla.+ 21 Mtu mwenye nguvu aliye na silaha, anapolinda jumba lake, mali yake huwa salama. 22 Lakini mtu mwingine mwenye nguvu zaidi yake anapomshambulia na kumshinda, humnyang’anya silaha zake zote alizotegemea, naye hugawa vitu alivyompora. 23 Yeyote asiye upande wangu ananipinga, na yeyote asiyekusanya pamoja nami anatawanya.+
-