Je! Ukristo wa Kweli Unatokeza Watu Wanaoshikilia Mambo Bila Akili?
TUMUIYA YA WAKRISTO imekuwa na watu wayo wanaoshikilia mambo bila akili—kuanzia watu waliojiteketeza wenyewe kwa moto katika kupinga mambo ya kisiasa kufika watu mmoja mmoja wanaotenda kwa kutovumilia wale walio na maoni ya kidini yaliyo tofauti na yao. Kwa mfano, Vita ya Kidini ya kwanza iliongozwa na Kanisa Katoliki iii kuweka huru Yerusalemu kutoka mikononi mwa watu iliyowafikiria kuwa makafiri. Ilianza kwa vikundi vitatu vya watu wenye ghasia wasio na nidhamu ambavyo jeuri yao yenye kupita kiasi ilitia ndani mauaji ya ujumla ya Wayahudi katika Rhineland. Wakati majeshi ya hii Vita ya Kidini yalipofaulu kuutwaa Yerusalemu, askari hao wenye kuitwa eti Wakristo waligeuza barabara za mji kuwa mito ya damu
Katika kitabu chake The Outline of History, H. G. Wells alisema hivi juu ya hiyo Vita ya Kidini ya kwanza: “Machinjo yalikuwa mabaya sana; damn ya walioshindwa ilitiririka kwenye barabara za mji, mpaka watu wakawa wakirusha damu walipokuwa wanapanda [wanyama wan]. Usiku ulipofika, ‵wakilia kwa kwikwi kwa kuzidiwa na furaha,ʼ wapiganaji hao wa Vita ya Kidini wakaja kwenye kaburi kutoka [kwenye machinjo hayo], wakaweka pamoja mikono yao yenye madoa ya damu katika sala.”
Katika Vita ya Kidini ya baadaye iliyoagizwa na Papa Innocent wa Tatu, Waalbijenesi na Wawaldenesi wenye amani, waliopinga mafundisho ya kidini ya Roma na mambo yenye kupita kiasi ya viongozi wa kidini, walivawa kijumla. Kuhusu hali ya kushikilia mambo bila akili iliyoonyeshwa kwao, Wells anaandika hivi: “Hiyo ilitosha kwa Lateran, na hivyo tuna tamasha hii yenye kuogofya ya Innocent wa Tatu akihubiri hii Vita ya Kidini dhidi ya wafuasi hawa wa madhehebu hizi wenye kupatwa na maafa, akiruhusu kutumiwa kwa kila mlaghai mwenye kutangatanga . . . na kila jeuri inayowazika [itendwe] miongoni mwa raia wenye kuamanika zaidi wa Mfalme wa Ufaransa. Habari ya ukatili na machukizo ya hii Vita ya Kidini ni yenye kuogopesha sana kusoma kuliko habari yo yote ya Wakristo waliouawa na wapagani kwa ajili ya imani.“
Historia ya Jumuiya ya Wakristo imejaa habari za watu wanaoshikilia mambo bila akili, na kwa kawaida wametokeza matunda ya jeuri. Kwa hiyo tunaweza kukata maneno kwamba kushikilia mambo bila akili hakutokezi tunda zuri. Kamusi ya Funk na Wagnalls New Standard Dictionary of the English Language (chapa ya 1929) inafafanua hali ya kushikilia mambo bila akili kwa maneno yafuatayo: “Juhudi yenye kupita kiasi au yenye kichaa.“ Na inaendelea kutoa mfano wa jambo hilo kwa njia hii: “Hakuna kipindi cha historia chenye kuonyesha kiasi kikubwa zaidi cha ukatili, ufisadi, na hali ya kushikilia mambo bila akili kuliko kile cha Vita vya Kidini.“
Pia inapendeza kuona ufafanusi unaopewa kwa maneno “wenye kushikilia mambo bila akili“ na Websterʼs Third New International Dictionary, chapa ya 1961. Inasema: Wanaoshikilia mambo bila akili—Kilatini, wenye kuongozwa na mungu fulani. 1. mwenye kupagawa na au kana kwamba amepagawa na shetani; kwa upana: -enye kichaa, -enye kurushwa akili, -enye wazimu. 2. -enye kuongozwa na, -enye kutokezwa, au -enye tabia ya kuwa na juhudi kubwa mno, -enye kupita kiasi, -siotumia akili; -enye shauku kupita kiasi, hasa katika mambo ya kidini.ʼ Tukiwa na mawazo hayo akilini, je! inaweza kusemwa kwamba Wakristo wa kweli ni wenye kushikilia mambo bila akili?
Wanatambulishwa kwa Matunda
Kama vile tunda la mti linavyoutambulisha, ndivyo na matokeo ya matendo ya kibinadamu hutambulisha ni watu wa aina gani wanaoyatokeza. Yesu Kristo, Mwanzilishi wa Ukristo, alitaja hilo. Yeye alisema: “Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mwovu kuzaa matunda mazuri. [Basil kwa matunda yao mtawatambua [watu hao].“ —Mathayo 7:18, 20
Yesu alianzisha Ukristo wa kweli ukiwa mti mwema. Basi, haungeweza, kuzaa matunda mabaya ya hali ya kushikilia mambo bila akili. Hakuna wakati wo wote ambao Yesu aliwahimi-za wafuasi wake wafanye mambo ya kuwadhuru wao wenyewe kimwili au kudhuru wengine. Badala yake, akitumia maneno ya mojapo amri mbili kubwa, alisema hivi: “Mpende jirani yako kama nafsi yako.“ (Mathayo 22:39) Ilikuwa lazima wafuasi wake wawe wenye fadhili hata kwa adui zao. Akasema Yesu: “Wapendeni adui zenu, watendeeni mema wale ambao wawachukia ninyi, wabarikieni wale ambao wawalaani ninyi, waombeeni wale ambao wawaonea ninyi.“ —Luka 6:27, 28.
Wafuasi wa kweli wa Yesu walienda miongoni mwa watu wa mataifa mengi mbalimbali, si wakiwa na moto na upanga, bali wakiwa na Neno la Mungu lililoandikwa pamoja na usadikisho wenye amani. Hakuna majeshi yaliyoandamana nao kwenye nchi zile nyingine iii kuchinja, kutesa, na kuingilia kinguvu wale waliokataa ubatizo wa Kikristo. Badala yake, wanafunzi wa Yesu walifuata mfano wake wenye amani kwa kuhubiri habari njema za Ufalme wa Mungu kwa wote, wakiwatia moyo watumie akili zao kuona sababu za habari iliyotolewa kutoka katika Maandiko. Matunda ya kazi yao yalitia ndani tunda la roho ya Mungu—“upendo, furaha, amani, ustahimilivu, fadhili, wema, imani, upole, kujiweza.“—Wagalatia 5:22, 23, NW.
Haiko tofauti leo. Ukristo wa kweli ungali unazaa tunda zuri. Ule mti, tengenezo la Kikristo, ambao Yesu alipanda zaidi ya miaka 1,900 iliyopita ulikuwa mwema, na ungali mwema. Kwa hiyo haiwezekani ukazaa matunda mabaya ya kushikilia mambo bila akili, kutovumilia wengine, na jeuri. Ni kwa sababu gani, basi, hali ya kushikilia mambo bila akili imekuwa ya kawaida sana katika Jumuiya ya Wakristo?
Mtume Paulo alionyesha kwamba wakati ungekuja ambapo Wakristo wa mwigo wangetokea. Wangechukua jina Wakristo lakini hawangeishi kulingana nalo au kuzaa matunda yalo mazuri. Yeye aliwaambia wazee kutoka Efeso hivi: “Najua mimi ya kuwa baada ya kuondoka kwangu mbwamwitu wakali wataingia kwenu, wasilihurumie kundi; tena katika ninyi wenyewe watainuka watu, wakisema mapotovu, wawavute hao wanafunzi wawaandamie wao.“ (Matendo 20:29, 30) Kutokana na waasi-imani hawa Jumuiya ya Wakristo iliinuka pamoja na mamia ya matengenezo yayo ya kidini yenye kuhitilafiana ikifundisha mambo yanayoonyeshwa to kuwa ya Kikristo. Kwa kweli, ni mambo “mapotovu,“ mawazo ya wanadamu wala si ukweli wa Neno la Mungu. Imekuwa miongoni mwa hawa Wakristo wa uwongo kwamba tunda baya la kushikilia mambo bila akili limejidhihirisha lenyewe.
Je! Juhudi ya Kikristo Ni Hali ya Kushikilia Mambo Bila Akili?
Ni kweli kwamba hali ya kushikilia mambo bila akili ni namna ya juhudi. Lakini hali ya kushikilia mambo bila akili ni “juhudi yenye kupita kiasi au yenye kichaa,“ juhudi “isiyo ya akili.“ Haiwezi kusemwa hivyo kuhusu Ukristo wa kweli
Kwa kurudiarudia, Biblia inawaonya kwa upole Wakristo wawe wenye kiasi. Kwa mfano, Wafilipi 4:5, NW husema: “Acheni kiasi chenu kijulikane kwa watu wote.“ Na Wakristo wanashauriwa “wasimtukane mtu ye yote, wasiwe wagomvi, wawe wema [ wenye kiasi, NW], wakionyesha upole wote kwa watu wote.“ —Tito 3:2.
Kwa sababu Mashahidi wa Yehova wanatembelea watu katika nyumba zao iii kuongea juu ya habari njema za Ufalme wa Mungu, wao ni tofauti na walio wengi wa wale wanaodai kuwa Wakristo. Juhudi hii katika huduma ya Kikristo si msingi wa kuwaona kuwa watu wenye kushikilia mambo bila akili. Ni juhudi iliyo na kiasi kwa ajili ya kazi ambayo Yesu alifanya na akaagiza wafuasi wake waifanye. (Mathayo 24:14; 28:19, 20) Mtu anayeweka kando utendaji mwingi wa kibinafsi wenye kutumia wakati mwingi sana iii atumie wakati mwingi iwezekanavyo kwenye kazi ya kuhubiri Ufalme si mtu anayeshikilia mambo bila akili. Badala yake, yeye anaonyesha uthamini wake kwa uharaka wa kusaidia wengine wajifunze juu ya kweli zenye kutoa uzima za Neno la Mungu katika wakati mfupi unaobaki wa kufanya kazi hii. Hili ni jambo la akili na lenye kunufaisha. Badala ya kuwa kazi ya watu wenye kushikilia mambo bila akili inayoumiza wengine, utendaji huo hujenga imani katika Mungu na Neno lake. Inatoa tumaini kwa wale wasio na tumaini, inaleta uhuru kutokana na ushirikina wa kidini na ujinga, na inageuza watu wasiohesabika wasio waadilifu na wenye jeuri kuwa Wakristo safi kiadili na wenye amani. Matunda haya mema yanaonyesha tengenezo zuri.
Katika nchi zaidi ya 200, Mashahidi wa Yehova hudumisha ushikamanifu wao kwa Ufalme wa Mungu, hata ingawa wao wanakuwa chini ya marufuku za kiserikali katika mahali pengi. Ushikamanifu wao kwa Mungu, Mwenye Enzi Kuu Aliye Mkuu Zaidi Sana, hauwezi hata kidogo kuitwa hali ya kushikilia mambo bila akili. Yeye ndiye Mamlaka Iliyo Juu Zaidi Sana, na kunapokuwa na kuhitilafiana kati ya sheria zake na zile za serikali za kibinadamu, Mkristo wa kweli ana wajibu wa kumtii yeye. Chini ya serikali za kibinadamu, nyakati nyingine sheria za mahali mahali zinafutwa kwa sababu zinahitilafiana na sheria za serikali kuu. Hali moja na hiyo, kwa Wakristo wa kweli sheria za kibinadamu zinafutiliwa mbali wakati zinapohitilafiana na zile za Yehova Mungu, Mwenye Enzi Kuu ya Ulimwengu Wote Mzima. Kwa kuwa Mkristo wa kweli hawezi kutii sheria mbili zinazohitilafiana, yeye anafanya kama walivyofanya mitume. Walisema: “Ni lazima sisi tutii Mungu kuwa mtawala kuliko wanadamu.“ (Matendo 5: 29, NW) Hilo linapatana na akili.
Hali iyo hiyo ya kupatana na akili inaonyeshwa na Mashahidi wa Yehova kwa habari ya maadhimisho ya kitaifa na ya kidini ambayo yanahitilafiana na Neno la Mungu. Si hali ya kushikilia mambo bila akili kukataa kushiriki katika maadhimisho ambayo walio wengi katika nchi wanaadhimisha. Kuwa tofauti kwa sababu ya dhamiri yao ya kidini kunawafanya Mashahidi kuwa katika hali moja na Wakristo wa kwanza-kwanza, ambao hawakushiriki katika maadhimisho yaliyopendwa na watu wengi katika siku zao. Na Mashahidi wa Yehova wanafurahia kutoa sababu ya Kimaandiko kwa kutoshiriki kwao—1 Petro 3:15
Watu fulai huenda wakawaweka Mashahidi pamoja na kikundi chenye kushikilia mambo bila akili kwa sababu kukataa kutiwa damu mishipani ma,na ya maibabu ambayo inapendwa na madaktari walio wengi. Hapa pia ni jambo la utii kwa sheria ya Mungu, Wafuasi wa kweli wa Yesu Kristo wanaamuliwa waendelee kushika mwito wa damu—Matendo15:28,29, NW
Je! mtu anakuwa mwenye kushikilia mambo bila akili kwa sababu, kwa ajili ya dhamiri, anakataa namna ya matibabu ambayo kwa wakati huu inapendelewa na watu wengi? Watu fulani wasio Mashahidi wa Yehova wanakataa kutiwa damu mishipani kwa sababu ya kuogopa kuambukizwa UKIMWI au magonjwa mengine. Kwa hiyo je! ni jambo lisilopatana na akili kwa Mashahidi kuomba matibabu ya kitiba yasiyochafua dhamiri zao?
Basi, ni jambo gani, linalopaswa kukatw; kutokana na hili? Kwamba Mashahidi wa Yeho va si watu wenye kushikilia mambo bila akil kwa sababu wao ni tofauti na walio wengi n. wanasisitiza kuwa watiifu kwa Mungu. Ijapoku wa wana juhudi kwa Mungu, wao hawan; “juhudi yenye kupita kiasi au yenye kichaa kana kwamba wamepagawa na shetani; wao hawaonekani kuwa ‵wenye kichaa, wenye kurushwa akili,ʼ au ‵wenye wazimu.ʼ Hakum wakati wo wote ambao kwa sababu ya juhudi 3T kidini wanawafanyia wengine jeuri yenye ku dhuru au kujidhuru wenyewe. Badala yake kupatana na yanayosemwa na Biblia juu Wakristo wa kweli, wao ni “wenye kuamanilv pamoja na watu wote.“—Warumi 12:18, NW.
Kwa hiyo tengenezo la Kikristo ambalo Yesi Kristo alianzisha katika karne ya kwanza mti mwema linaendelea leo kuzaa tunda zuri tu Kwa hiyo, haiwezekani Ukristo wa kweli utoke ze watu wenye kushikilia mambo bila akili
[Blabu katika ukurasa wa 30]
Hakuna sababu ya kuwaona Mashahidi wa Yehova kuwa watu wenye kushikilia mambo bila akili kwa sababu ya juhudi yao katika huduma ya Kikristo