SEPTEMBA 29–OKTOBA 5
MHUBIRI 3-4
Wimbo 93 na Sala | Utangulizi (Dak. 1)
Tumieni wakati pamoja na mtumie wakati na Yehova
1. Imarisheni Kamba Yenu ya Nyuzi Tatu
(Dak. 10)
Tengeni wakati ili muwe na mazungumzo yenye kujenga (Mhu 3:1; ijwhf makala ya 10 ¶2-8)
Fanyeni mambo pamoja (Mhu 4:9; w23.05 23-24 ¶12-14)
Sitawisheni uhusiano wenye nguvu na Yehova (Mhu 4:12; w23.05 21 ¶3)
JIULIZE, ‘Kutumia muda mrefu mbali na mwenzi wangu, kwenda likizo bila mwenzi wangu wa ndoa, au kuwa mbali na mwenzi wangu kwa sababu ya kazi, kutaathirije ndoa yangu?’
2. Hazina za Kiroho
(Dak. 10)
Mhu 3:8—Ni wakati gani ambao si “wakati wa kupenda”? (it “Upendo” ¶39)
Ungependa kushiriki nasi hazina gani kutoka kwenye usomaji wa Biblia wa juma hili?
3. Usomaji wa Biblia
(Dak. 4) Mhu 4:1-16 (th somo la 2)
4. Kuanzisha Mazungumzo
(Dak. 3) NYUMBA KWA NYUMBA. Tumia Mnara wa Mlinzi Na. 1 2025 kuanzisha mazungumzo. Badili utangulizi wako mwenye nyumba anapopendezwa na jambo lingine. (lmd somo la 2 jambo kuu la 5)
5. Kufuatia Upendezi
(Dak. 4) MAHUBIRI YASIYO RASMI. Mwalike mtu ambaye ulimwachia gazeti la Mnara wa Mlinzi Na. 1 2025 ajifunze Biblia. (lmd somo la 9 jambo kuu la 4)
6. Hotuba
(Dak. 5) lmd nyongeza A jambo kuu la 12—Kichwa: Mungu Hana Ubaguzi na Anatenda kwa Haki. (th somo la 19)
Wimbo 131
7. Matatizo Yanapotokea Katika Ndoa Yako, Endelea Kutumaini Mwongozo wa Yehova
(Dak. 15) Mazungumzo.
Yehova amewapatia wenzi wa ndoa Wakristo kila kitu wanachohitaji ili wawe na ndoa yenye mafanikio na furaha. Hata hivyo, pindi fulani bado wenzi wa ndoa watakabili matatizo. (1Ko 7:28) Ikiwa hayatashughulikiwa mapema, matatizo hayo yanaweza kusababisha maumivu ya kihisia, na huenda wakahisi kwamba hawawezi tena kutatua matatizo wanayokabili. Vipi ikiwa ndoa yako inakabili matatizo kama hayo?
Video Upendo wa Kweli Ni Nini? ina simulizi la wenzi wa ndoa vijana ambao walikabili matatizo makubwa katika ndoa yao. Je, unakumbuka ushauri ambao baba alimpa binti yake alipokuwa karibu kufanya uamuzi bila kutafakari maoni ya Yehova?
Onyesha VIDEO Upendo wa Kweli Ni Nini?—Kisehemu. Kisha waulize wasikilizaji:
Kwa nini tunapaswa kutegemea mwongozo wa Yehova tunapokabili matatizo katika ndoa?—Isa 48:17; Mt 19:6
Ikiwa unakabili matatizo makubwa katika ndoa yako, endelea kumhusisha Yehova kwa kudumisha ratiba nzuri ya kiroho. Jitahidi kusuluhisha matatizo yenu kwa kutumia kanuni za Biblia, na kutafuta habari kutoka katika machapisho yetu zitakazokusaidia kuwa na maoni kama ya Yehova kuhusu hali yenu. Ukifanya hivyo, utaonyesha kwamba unahitaji baraka na utegemezo wa Yehova.—Met 10:22; Isa 41:10.
Onyesha VIDEO Usidanganywe na Amani ya Uwongo!—Darrel na Deborah Freisinger. Kisha waulize wasikilizaji:
Umejifunza nini kuhusu kushughulikia matatizo makubwa katika ndoa kutokana na simulizi la Ndugu na Dada Freisinger?
8. Funzo la Biblia la Kutaniko
(Dak. 30) lfb somo la 22, utangulizi wa sehemu ya 5, na somo la 23