Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb25 Septemba kur. 6-7
  • Septemba 22-28

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Septemba 22-28
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2025
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2025
mwb25 Septemba kur. 6-7

SEPTEMBA 22-28

MHUBIRI 1-2

Wimbo 103 na Sala | Utangulizi (Dak. 1)

HAZINA ZA NENO LA MUNGU

1. Endelea Kukizoeza Kizazi Kinachofuata

(Dak. 10)

[Onyesha VIDEO Utangulizi wa Mhubiri.]

Kila kizazi kina jukumu la kuzoeza kizazi kinachofuata (Mhu 1:4; w17.01 27-28 ¶3-4)

Tunapowazoeza na kuwakabidhi wengine majukumu, tunaruhusu wengine wapate shangwe inayotokana na kufanya kazi kwa bidii katika utumishi wa Yehova (Mhu 2:24)

Mzee wa kutaniko ambaye ni kijana anaongoza Funzo la “Mnara wa Mlinzi” na ndugu mwenye umri mkubwa ambaye ni msomaji akimtazama huku akitabasamu.

Usiruhusu shangwe unayopata kwa sababu ya kuwa na mapendeleo ikuzuie kuwazoeza ndugu vijana ili watimize mengi zaidi

2. Hazina za Kiroho

(Dak. 10)

  • Mhu 1:1—Fafanua jukumu la Sulemani akiwa “mkutanishaji.” (it “Mhubiri” ¶1)

  • Ungependa kushiriki nasi hazina gani kutoka kwenye usomaji wako wa Biblia wa juma hili?

3. Usomaji wa Biblia

(Dak. 4) Mhu 1:​1-18 (th somo la 11)

BORESHA HUDUMA YAKO

4. Kuanzisha Mazungumzo

(Dak. 2) MAHUBIRI YASIYO RASMI. Tafuta jambo lililomvutia mtu huyo na ufanye mipango ya kuwasiliana naye tena. (lmd somo la 3 jambo kuu la 5)

5. Kuanzisha Mazungumzo

(Dak. 2) MAHUBIRI YA UMMA. Zungumzia moja ya “Kweli Tunazopenda Kufundisha” kwa kutumia njia inayofafanuliwa kwenye nyongeza A ya broshua Wapende Watu. (lmd somo la 2 jambo kuu la 3)

6. Kufuatia Upendezi

(Dak. 2) MAHUBIRI YASIYO RASMI. Jibu swali ambalo mtu huyo aliuliza mlipozungumza wakati uliopita. (lmd somo la 9 jambo kuu la 5)

7. Kufanya Wanafunzi

(Dak. 5) MAHUBIRI YA UMMA. Mwonyeshe jinsi funzo la Biblia linavyoongozwa na ufanye mipango ya kuendeleza funzo hilo. (lmd somo la 10 jambo kuu la 3)

MAISHA YA MKRISTO

Wimbo 84

8. Masomo Matatu Muhimu Kuhusu Kuzoeza

(Dak. 15) Mazungumzo.

Mkusanyo wa picha: Akina ndugu wakiwazoeza wengine katika maeneo mbalimbali. 1. Ndugu akimzoeza dada kutumia msumeno wa umeme kwenye mradi wa ujenzi. 2. Ndugu mwenye umri mkubwa akimsikiliza ndugu kijana anapofanya mazoezi ya kutoa hotuba yake kwenye Jumba la Ufalme wakiwa peke yao. Ndugu mwenye umri mkubwa ameshika broshua “Boresha Uwezo Wako wa Kusoma na Kufundisha.” 3. Ndugu anamfundisha ndugu kijana jinsi ya kubadilisha betri kwenye maikrofoni. 4. Baba na watoto wake wawili wanasafisha Jumba la Ufalme. Baba na mwana wake mkubwa wakitumia mashine kusafisha sakafu huku mwana mdogo akitumia kitambaa kufuta kinara.

Upendo unatuchochea kuwazoeza wengine ili kukamilisha kazi ambayo Yehova ametupatia

Biblia ina mifano mingi mizuri inayotufundisha jinsi ya kuwazoeza wengine. Tunaweza kujifunza mambo mengi kutokana na jinsi Samweli alivyomzoeza Sauli, Eliya alivyomzoeza Elisha, jinsi Yesu alivyowazoeza wanafunzi wake, na jinsi Paulo alivyomzoeza Timotheo. Bila shaka, Yehova ndiye mzoezaji bora. Tunaweza kujifunza nini kutokana na mfano wake?

Onyesha VIDEO Mwige Yehova Unapowazoeza Wengine (Yoh 5:20)—Kisehemu. Kisha waulize wasikilizaji:

  • Ni masomo gani matatu tunayoweza kujifunza kutoka kwa Yehova akiwa mzoezaji?

9. Funzo la Biblia la Kutaniko

(Dak. 30) lfb somo la 20-21

Umalizio (Dak. 3) | Wimbo 148 na Sala

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki