OKTOBA 6-12
MHUBIRI 5-6
Wimbo 42 na Sala | Utangulizi (Dak. 1)
Kikundi cha Waisraeli wakisikiliza kwa makini kuhani anapofafanua Sheria
1. Tunaonyeshaje Kwamba Tunamheshimu Sana Mungu Wetu Mkuu?
(Dak. 10)
Tunaonyesha heshima kwenye mikutano tunaposikiliza kwa makini na tunapochagua kwa uangalifu mavazi na mapambo yetu (Mhu 5:1; w08 8/15 15-16 ¶17-18)
Tunapotoa sala mbele ya wengine kwenye mikutano tunahakikisha kwamba sala zetu si ndefu na tunazitoa kwa njia ya heshima (Mhu 5:2; w09 11/15 11 ¶21)
Kwa kuishi kulingana na wakfu wetu (Mhu 5:4-6; w17.04 6 ¶12)
2. Hazina za Kiroho
(Dak. 10)
Mhu 5:8—Mstari huu unawezaje kutufariji tunapotendewa isivyo haki? (w20.09 31 ¶3-5)
Ungependa kushiriki nasi hazina gani kutoka kwenye usomaji wa Biblia wa juma hili?
3. Usomaji wa Biblia
(Dak. 4) Mhu 5:1-17 (th somo la 12)
4. Kuanzisha Mazungumzo
(Dak. 1) NYUMBA KWA NYUMBA. Mwenye nyumba anataka kubishana. (lmd somo la 4 jambo kuu la 5)
5. Kuanzisha Mazungumzo
(Dak. 2) MAHUBIRI YASIYO RASMI. Zungumzia moja ya “Kweli Tunazopenda Kufundisha” kutoka kwenye nyongeza A ya broshua Wapende Watu. (lmd somo la 1 jambo kuu la 3)
6. Kufuatia Upendezi
(Dak. 3) NYUMBA KWA NYUMBA. Zungumzia video kutoka kwenye Sanduku la Vifaa vya Kufundishia. (lmd somo la 7 jambo kuu la 3)
7. Kufanya Wanafunzi
Wimbo 160
8. Je, Unatumia “Kweli Tunazopenda Kufundisha”?
(Dak. 15) Mazungumzo.
Tangu broshua Wapende Watu—Fanya Wanafunzi ilipotolewa, imetusaidia kuboresha njia yetu ya kuanzisha mazungumzo na watu. Nyongeza A ilikusudiwa hasa kutusaidia kuzungumzia kweli rahisi za Biblia tunapozungumza na watu. (Ebr 4:12) Je, unafahamu mambo tisa yaliyo chini ya sehemu yenye kichwa “Kweli Tunazopenda Kufundisha”?
Tunawezaje kuzungumzia kweli rahisi ya Biblia kwa wakati unaofaa tunapozungumza na mtu?—lmd nyongeza A
Ni habari gani zinazowavutia watu zaidi katika eneo lenu?
Unaweza kufanya nini ili ukumbuke maandiko yanayopatikana katika sehemu ya nyongeza A?
Kadiri tunavyotumia maandiko hayo zaidi katika huduma, ndivyo tutakavyoyakumbuka zaidi. Hata hivyo, ili tuyatumie kwa ukawaida, ni lazima kwanza tuzungumze na watu katika eneo letu.
Onyesha VIDEO “Chuma Hunoa Chuma”—Kuwafikia Watu Wengi Zaidi. Kisha waulize wasikilizaji:
Ni nini kinachoweza kutusaidia kuzungumza na watu wengi zaidi katika eneo letu?
9. Funzo la Biblia la Kutaniko
(Dak. 30) lfb somo la 24-25