Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Leo

Ijumaa, Oktoba 24

Zaidi ya mambo yote, pendaneni sana, kwa sababu upendo hufunika dhambi nyingi.—1 Pet. 4:8.

Neno linalotafsiriwa kuwa “sana” ambalo mtume Petro ametumia, kihalisi linamaanisha “kujinyoosha” au “kuvutika.” Sehemu ya pili ya mstari huo inafafanua matokeo ya kupendana sana. Tukiwapenda sana ndugu zetu tutafunika dhambi zao. Tunaweza kuwazia hali hiyo kwa njia hii: Tunaushika upendo wetu kwa mikono miwili, kana kwamba tumeshika kitambaa kinachovutika, na tunakivuta zaidi na zaidi hadi kinafunika, si dhambi moja au mbili, bali “dhambi nyingi.” Kufunika kunamaanisha kusamehe. Kama kitambaa kinavyoweza kufunika doa, upendo unaweza kufunika udhaifu na kutokamilika kwa wengine. Upendo wetu kwa wengine unapaswa kuwa na nguvu sana hivi kwamba tunaweza kusamehe kutokamilika kwa waabudu wenzetu—hata ikiwa ni vigumu kufanya hivyo. (Kol. 3:13) Tunapowasamehe wengine, tunaonyesha kwamba upendo wetu ni wenye nguvu na tunataka kumfurahisha Yehova. w23.11 11-12 ¶13-15

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumamosi, Oktoba 25

Shafani akaanza kukisoma mbele ya mfalme.—2 Nya. 34:18.

Alipokuwa na umri wa miaka 26, Mfalme Yosia alianza kazi ya kurekebisha hekalu. Kazi hiyo ilipokuwa ikiendelea, “kitabu cha Sheria ya Yehova kilichotolewa kupitia Musa” kilipatikana. Mfalme aliposikia kikisomwa, alichochewa kuchukua hatua na kutenda kulingana na mambo yaliyoandikwa humo. (2 Nya. 34:​14, 19-21) Je, ungependa kusoma Biblia kwa ukawaida? Ikiwa tayari unafanya hivyo je, unafurahia? Je, unaweka kumbukumbu ya mistari ambayo inaweza kukusaidia kibinafsi? Yosia alipokuwa na umri wa miaka 39, alifanya uamuzi mbaya uliomsababishia kifo. Alijitegemea mwenyewe badala ya kumwomba Yehova mwongozo. (2 Nya. 35:​20-25) Tunapata somo fulani hapa. Hata iwe tuna umri gani au tumekuwa tukijifunza Biblia kwa muda mrefu kadiri gani, tunapaswa kuendelea kumtafuta Yehova. Hilo linatia ndani kusali kwake kwa ukawaida ili kupata mwongozo, kujifunza Neno lake, na kusikiliza ushauri wa Wakristo wakomavu. Tukifanya hivyo, tutapunguza uwezekano wa kufanya makosa mazito na tutakuwa wenye furaha zaidi.—Yak. 1:25. w23.09 12 ¶15-16

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumapili, Oktoba 26

Mungu huwapinga wenye majivuno, lakini huwapa wanyenyekevu fadhili zisizostahiliwa.—Yak. 4:6.

Biblia inawataja wanawake wengi wa pekee waliompenda Yehova na kumtumikia. Wanawake hao walikuwa “wenye kiasi katika mazoea” na “waaminifu katika mambo yote.” (1 Tim. 3:11) Kwa kuongezea, akina dada vijana wanaweza kupata katika kutaniko lao wanawake Wakristo wakomavu ambao ni mfano mzuri wa kuigwa. Akina dada vijana, je, mnaweza kutafuta kutanikoni wanawake Wakristo wakomavu ambao mnaweza kuiga mfano wao? Chunguzeni sifa zao zinazovutia; kisha mfikirie jinsi mnavyoweza kuonyesha sifa hizo. Sifa muhimu ya kuwa Mkristo mkomavu ni unyenyekevu. Ikiwa mwanamke ni mnyenyekevu, atafurahia uhusiano mzuri na Yehova na watu wengine pia. Kwa mfano, mwanamke anayempenda Yehova, kwa unyenyekevu anachagua kuunga mkono kanuni ya ukichwa ambayo Baba yake wa mbinguni alianzisha. (1 Kor. 11:3) Kanuni hiyo inatumika kwa njia hususa katika kutaniko na katika familia pia. w23.12 18-19 ¶3-5

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki