Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Leo

Jumatano, Oktoba 8

Sitakuacha kamwe.—Ebr. 13:5.

Washiriki wa Baraza Linaloongoza wamekuwa wakiwazoeza kibinafsi wasaidizi katika halmashauri mbalimbali za Baraza Linaloongoza. Kwa sasa wasaidizi hao wanashughulikia majukumu mazito kwa uaminifu. Wako tayari kabisa kuendeleza kazi ya kuwatunza kondoo wa Kristo. Watiwa-mafuta wa mwisho watakapochukuliwa na kwenda mbinguni mwishoni mwa ile dhiki kuu, ibada safi itaendelea hapa duniani. Kwa sababu ya uongozi mzuri wa Yesu Kristo, waabudu wa Mungu hawatakosa chochote. Ni kweli kwamba wakati huo tutakuwa tukishambuliwa na Gogu wa Magogu, muungano wa mataifa yenye chuki. (Eze. 38:​18-20) Lakini shambulizi hilo fupi halitafaulu; halitawafanya watu wa Mungu waache kumwabudu Yehova. Bila shaka atawaokoa! Katika maono, mtume Yohana aliona “umati mkubwa” wa kondoo wengine wa Kristo. Yohana aliambiwa kwamba ‘umati huo mkubwa’ unatoka “katika ile dhiki kuu.” (Ufu. 7:​9, 14) Naam, tuna uhakika kwamba watakuwa salama! w24.02 5-6 ¶13-14

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Alhamisi, Oktoba 9

Msiuzime moto wa roho.—1 The. 5:19.

Tunaweza kufanya nini ili tupokee roho takatifu? Tunaweza kusali ili tupate roho takatifu, kujifunza Neno la Mungu lililoongozwa na roho, na kushirikiana na tengenezo lake linaloongozwa na roho. Kufanya hivyo, kutatusaidia kusitawisha sifa za “tunda la roho.” (Gal. 5:​22, 23) Mungu huwapa roho yake wale tu ambao wanadumisha mawazo safi na mwenendo safi. Hataendelea kutupatia roho yake ikiwa tutaendelea kuwa na mawazo yasiyo safi na kutenda kulingana na mawazo hayo. (1 The. 4:​7, 8) Ili tuendelee kupokea roho takatifu, pia hatupaswi ‘kuutendea unabii kwa dharau.’ (1 The. 5:20) Hapa “unabii” unamaanisha ujumbe uliotokezwa na roho ya Mungu, kutia ndani ujumbe kuhusu siku ya Yehova na uhitaji wa kutenda haraka katika nyakati zetu. Hatuahirishi siku hiyo katika akili zetu na kufikiri kwamba Har–​Magedoni haitakuja tukiwa hai. Badala yake, tunaiweka karibu akilini kwa kudumisha mwenendo unaofaa na kuendelea kuwa na bidii katika “vitendo vya ujitoaji-kimungu.”—2 Pet. 3:​11, 12. w23.06 12 ¶13-14

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Ijumaa, Oktoba 10

Kumwogopa Yehova ndio mwanzo wa hekima.—Met. 9:10.

Tukiwa Wakristo, tunapaswa kufanya nini ikiwa picha ya ponografia itatokea bila kutarajia kwenye kifaa chetu cha kielektroni? Tunapaswa kuacha mara moja kutazama picha hiyo. Itakuwa rahisi kufanya hivyo ikiwa tutakumbuka kwamba uhusiano wetu pamoja na Yehova ndilo jambo lenye thamani zaidi kwetu. Hata baadhi ya picha ambazo hazionwi kuwa za ponografia zinaweza kuchochea hamu ya ngono. Kwa nini tunapaswa kuziepuka? Kwa sababu hatungependa hata kuwazia kufanya uasherati katika moyo wetu. (Mt. 5:​28, 29) David, mzee wa kutaniko anayeishi nchini Thailand, anasema hivi: “Mimi hujiuliza: ‘Ingawa picha hizo si ponografia, je, nitamfurahisha Yehova ikiwa nitaendelea kuzitazama?’ Kufikiria kwa njia hiyo hunisaidia kutenda kwa hekima.” Tutatenda kwa hekima ikiwa tutasitawisha woga unaofaa kwa kuepuka kufanya jambo linalomchukiza Yehova. Kumwogopa Mungu ndio “mwanzo,” au msingi, “wa hekima.” w23.06 23 ¶12-13

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki