Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Leo

Jumatatu, Agosti 11

Usawaziko wenu na ujulikane kwa watu wote.—Flp. 4:5.

Yesu aliiga usawaziko wa Yehova. Alitumwa duniani ili awahubirie “kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.” Lakini alikuwa mwenye usawaziko alipokuwa akitimiza mgawo huo. Pindi moja, mwanamke asiye Mwisraeli alimsihi Yesu amponye binti yake ambaye alikuwa “anasumbuliwa kikatili na roho mwovu.” Kwa huruma, Yesu alifanya jambo ambalo mwanamke huyo alimwomba na akamponya binti yake. (Mt. 15:​21-28) Fikiria mfano mwingine. Mwanzoni mwa huduma yake, Yesu alisema hivi: “Yeyote anayenikana . . . , mimi pia nitamkana.” (Mt. 10:33) Lakini je, alimkana Petro alipomkana mara tatu? Hapana. Yesu alijua kwamba Petro alitubu na alikuwa mwenye imani. Baada ya kufufuliwa, Yesu alimtokea Petro na inaelekea alimhakikishia kwamba amemsamehe na anampenda. (Luka 24:​33, 34) Yehova Mungu na Yesu Kristo ni wenye usawaziko. Namna gani sisi? Yehova anatarajia tuwe wenye usawaziko. w23.07 21 ¶6-7

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumanne, Agosti 12

Kifo hakitakuwapo tena.—Ufu. 21:4.

Ni uhakikisho gani tunaoweza kushiriki na wale ambao wana shaka kwamba ahadi ya Mungu ya Paradiso itatimia? Kwanza, Yehova mwenyewe ndiye anayetoa ahadi hiyo. Kitabu cha Ufunuo kinasema: “Yule aliyeketi kwenye kiti cha ufalme akasema: ‘Tazama! Ninafanya vitu vyote kuwa vipya.’” Yeye ana hekima, nguvu, na tamaa ya kutimiza ahadi yake. Pili, utimizo wa ahadi hiyo ni hakika kabisa, hivi kwamba kwa maoni ya Yehova tayari mambo hayo yametukia. Ndiyo sababu anasema: “Maneno haya ni ya uaminifu na ya kweli. . . . Yametimia!” Tatu, Yehova anapoanza kufanya jambo, anahakikisha linakamilika kwa mafanikio, kama inavyothibitishwa na maneno haya: “Mimi ndiye Alfa na Omega.” (Ufu. 21:6) Yehova atathibitisha kwamba Shetani ni mwongo na ameshindwa. Hivyo, mtu anaposema, “Ahadi hii haiwezi kutimia,” unaweza kusoma na kufafanua Ufunuo 21:​5, 6. Mwonyeshe jinsi ambavyo Yehova ametoa uhakikisho wa ahadi yake, kwa kuitia saini yake mwenyewe kwa njia ya mfano.—Isa. 65:16. w23.11 7 ¶18-19

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumatano, Agosti 13

Nitakufanya kuwa taifa kubwa.—Mwa. 12:2.

Yehova alitoa ahadi hiyo kwa Abrahamu alipokuwa na umri wa miaka 75 na bila mtoto. Je, Abrahamu aliona ahadi hiyo ikitimizwa? Hakuona ikitimizwa kikamili. Baada ya kuvuka Mto Efrati na kusubiri kwa miaka 25, Abrahamu aliona mwana wake, Isaka, akizaliwa kimuujiza, na baada ya miaka mingine 60, wajukuu wake, Esau na Yakobo walizaliwa. (Ebr. 6:15) Lakini Abrahamu hakuona kamwe wazao wake wakiwa taifa kubwa na kurithi Nchi ya Ahadi. Hata hivyo, mwanamume huyo mwaminifu alifurahia urafiki wa karibu pamoja na Muumba wake. (Yak. 2:23) Na Abrahamu atakapofufuliwa, atasisimka sana kujua kwamba imani na subira yake ilitokeza baraka kwa mataifa yote! (Mwa. 22:18) Somo ni nini? Huenda sisi binafsi hatutaona ahadi zote za Yehova zikitimizwa moja kwa moja. Hata hivyo, ikiwa tutakuwa wenye subira kama Abrahamu, tunaweza kuwa na uhakika kwamba Yehova atatuthawabisha sasa na kwa njia kubwa hata zaidi katika ulimwengu mpya alioahidi.—Marko 10:​29, 30. w23.08 24 ¶14

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki