Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Leo

Jumanne, Agosti 12

Kifo hakitakuwapo tena.—Ufu. 21:4.

Ni uhakikisho gani tunaoweza kushiriki na wale ambao wana shaka kwamba ahadi ya Mungu ya Paradiso itatimia? Kwanza, Yehova mwenyewe ndiye anayetoa ahadi hiyo. Kitabu cha Ufunuo kinasema: “Yule aliyeketi kwenye kiti cha ufalme akasema: ‘Tazama! Ninafanya vitu vyote kuwa vipya.’” Yeye ana hekima, nguvu, na tamaa ya kutimiza ahadi yake. Pili, utimizo wa ahadi hiyo ni hakika kabisa, hivi kwamba kwa maoni ya Yehova tayari mambo hayo yametukia. Ndiyo sababu anasema: “Maneno haya ni ya uaminifu na ya kweli. . . . Yametimia!” Tatu, Yehova anapoanza kufanya jambo, anahakikisha linakamilika kwa mafanikio, kama inavyothibitishwa na maneno haya: “Mimi ndiye Alfa na Omega.” (Ufu. 21:6) Yehova atathibitisha kwamba Shetani ni mwongo na ameshindwa. Hivyo, mtu anaposema, “Ahadi hii haiwezi kutimia,” unaweza kusoma na kufafanua Ufunuo 21:​5, 6. Mwonyeshe jinsi ambavyo Yehova ametoa uhakikisho wa ahadi yake, kwa kuitia saini yake mwenyewe kwa njia ya mfano.—Isa. 65:16. w23.11 7 ¶18-19

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumatano, Agosti 13

Nitakufanya kuwa taifa kubwa.—Mwa. 12:2.

Yehova alitoa ahadi hiyo kwa Abrahamu alipokuwa na umri wa miaka 75 na bila mtoto. Je, Abrahamu aliona ahadi hiyo ikitimizwa? Hakuona ikitimizwa kikamili. Baada ya kuvuka Mto Efrati na kusubiri kwa miaka 25, Abrahamu aliona mwana wake, Isaka, akizaliwa kimuujiza, na baada ya miaka mingine 60, wajukuu wake, Esau na Yakobo walizaliwa. (Ebr. 6:15) Lakini Abrahamu hakuona kamwe wazao wake wakiwa taifa kubwa na kurithi Nchi ya Ahadi. Hata hivyo, mwanamume huyo mwaminifu alifurahia urafiki wa karibu pamoja na Muumba wake. (Yak. 2:23) Na Abrahamu atakapofufuliwa, atasisimka sana kujua kwamba imani na subira yake ilitokeza baraka kwa mataifa yote! (Mwa. 22:18) Somo ni nini? Huenda sisi binafsi hatutaona ahadi zote za Yehova zikitimizwa moja kwa moja. Hata hivyo, ikiwa tutakuwa wenye subira kama Abrahamu, tunaweza kuwa na uhakika kwamba Yehova atatuthawabisha sasa na kwa njia kubwa hata zaidi katika ulimwengu mpya alioahidi.—Marko 10:​29, 30. w23.08 24 ¶14

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Alhamisi, Agosti 14

Wakati alipokuwa akimtafuta Yehova, Mungu wa kweli alimfanikisha.—2 Nya. 26:5.

Alipokuwa kijana Mfalme Uzia alikuwa mnyenyekevu. Alijifunza “kumwogopa Mungu wa kweli.” Aliishi kwa miaka 68, na kwa sehemu kubwa ya maisha yake Yehova alimbariki. (2 Nya. 26:​1-4) Uzia aliwashinda maadui wengi na aliimarisha ulinzi wa jiji la Yerusalemu. (2 Nya. 26:​6-15) Bila shaka, Uzia alifurahia mambo yote ambayo Mungu alimsaidia kufanya. (Mhu. 3:​12, 13) Mfalme Uzia alizoea kuwapa watu maagizo. Je, hilo lilimfanya afikiri kwamba angeweza kufanya chochote alichotaka? Siku moja, Uzia aliingia katika hekalu la Yehova na kwa kimbelembele alijaribu kufukiza uvumba kwenye madhabahu, jambo ambalo wafalme hawakuruhusiwa kufanya. (2 Nya. 26:​16-18) Kuhani Mkuu Azaria alijaribu kumrekebisha, lakini Uzia alikasirika sana. Kwa kusikitisha, Uzia aliharibu rekodi yake ya kutumikia kwa uaminifu na Yehova akampiga kwa ukoma. (2 Nya. 26:​19-21) Maisha yake yangekuwa tofauti sana ikiwa angeendelea kuwa mnyenyekevu! w23.09 10 ¶9-10

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki