Alhamisi, Agosti 28
Yehova yuko karibu na wote wanaomwitia, wote wanaomwitia yeye katika ukweli.—Zab. 145:18.
Yehova, “Mungu wa upendo,” yuko pamoja nasi! (2 Kor. 13:11) Anapendezwa nasi kibinafsi. Tunasadiki kwamba “[tumezungukwa] na upendo Wake mshikamanifu.” (Zab. 32:10) Kadiri tunavyotafakari jinsi ambavyo ameonyesha upendo wake kwetu, ndivyo anavyokuwa halisi zaidi kwetu, na tunahisi yuko karibu zaidi nasi. Tunaweza kumkaribia kwa uhuru na kumweleza jinsi tunavyohitaji sana upendo wake. Tunaweza kumweleza mahangaiko yetu yote, tukiwa na uhakika kwamba anatuelewa na kwamba yuko tayari kutusaidia. (Zab. 145:19) Kama tunavyovutiwa kuota moto katika siku yenye baridi, ndivyo tunavyovutiwa na upendo mwororo wa Yehova. Ingawa upendo wa Yehova ni wenye nguvu, ni mwororo pia. Kwa hiyo, uruhusu upendo mwororo wa Yehova maishani mwako. Kwa sababu Yehova anatupenda, acheni sisi sote tuseme hivi kwa sauti: “Ninampenda Yehova”!—Zab. 116:1. w24.01 31 ¶19-20
Ijumaa, Agosti 29
Nimewajulisha jina lako.—Yoh. 17:26.
Yesu alifanya mengi zaidi ya kuwaambia tu watu kwamba jina la Mungu ni Yehova. Wayahudi ambao Yesu aliwafundisha tayari walilijua jina la Mungu. Lakini Yesu ndiye aliyekuwa mstari wa mbele akiwa yule ‘aliyeeleza kumhusu.’ (Yoh. 1:17, 18) Kwa mfano, Maandiko ya Kiebrania yanafunua kwamba Yehova ni mwenye rehema na huruma. (Kut. 34:5-7) Yesu alifafanua kweli hiyo hata zaidi aliposimulia kuhusu mfano wa mwana mpotevu na baba yake. Tunaposoma kuhusu jinsi baba huyo anavyomwona mwana wake aliyetubu “akiwa mbali,” anavyokimbia ili kukutana naye, anavyomkumbatia, na kumsamehe kutoka moyoni, tunapata picha kamili zaidi ya rehema na huruma ya Yehova. (Luka 15:11-32) Yesu aliwasaidia wengine waelewe vizuri kabisa utu wa Baba yake. w24.02 10 ¶8-9
Jumamosi, Agosti 30
[Tuwafariji] wengine . . . kwa faraja ambayo tunapokea kutoka kwa Mungu.—2 Kor. 1:4.
Yehova anawaburudisha na kuwafariji wale wanaokabili hali ngumu. Tunawezaje kumwiga Yehova kwa kuwaonyesha wengine huruma na kuwafariji? Njia moja tunayoweza kufanya hivyo ni kwa kusitawisha sifa zitakazotusaidia kuonyesha huruma na kuwafariji wengine. Baadhi ya sifa hizo ni zipi? Ni nini kitakachotusaidia tudumishe upendo wetu na ‘kuendelea kufarijiana’ kila siku? (1 The. 4:18) Tunahitaji kusitawisha sifa nyororo kama vile hisia-mwenzi, upendo wa kindugu, na fadhili. (Kol. 3:12; 1 Pet. 3:8) Sifa hizo zitatusaidiaje? Tunapowahurumia ndugu zetu na kuwajali kikweli, tutakuwa na tamaa yenye nguvu ya kuwafariji wanapoteseka. Kama Yesu alivyosema, “kinywa husema mambo yaliyojaa moyoni. Mtu mwema hutoa mambo mema katika hazina yake njema.” (Mt. 12:34, 35) Kuwafariji ndugu na dada zetu wenye uhitaji ni njia muhimu sana ya kuwaonyesha kwamba tunawapenda. w23.11 10 ¶10-11