Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Leo

Jumamosi, Agosti 30

[Tuwafariji] wengine . . . kwa faraja ambayo tunapokea kutoka kwa Mungu.—2 Kor. 1:4.

Yehova anawaburudisha na kuwafariji wale wanaokabili hali ngumu. Tunawezaje kumwiga Yehova kwa kuwaonyesha wengine huruma na kuwafariji? Njia moja tunayoweza kufanya hivyo ni kwa kusitawisha sifa zitakazotusaidia kuonyesha huruma na kuwafariji wengine. Baadhi ya sifa hizo ni zipi? Ni nini kitakachotusaidia tudumishe upendo wetu na ‘kuendelea kufarijiana’ kila siku? (1 The. 4:18) Tunahitaji kusitawisha sifa nyororo kama vile hisia-mwenzi, upendo wa kindugu, na fadhili. (Kol. 3:12; 1 Pet. 3:8) Sifa hizo zitatusaidiaje? Tunapowahurumia ndugu zetu na kuwajali kikweli, tutakuwa na tamaa yenye nguvu ya kuwafariji wanapoteseka. Kama Yesu alivyosema, “kinywa husema mambo yaliyojaa moyoni. Mtu mwema hutoa mambo mema katika hazina yake njema.” (Mt. 12:​34, 35) Kuwafariji ndugu na dada zetu wenye uhitaji ni njia muhimu sana ya kuwaonyesha kwamba tunawapenda. w23.11 10 ¶10-11

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumapili, Agosti 31

Wale walio na ufahamu wataelewa.—Dan. 12:10.

Tunahitaji kuomba msaada ili tuelewe unabii wa Biblia. Fikiria mfano ufuatao. Wazia kwamba unatembelea eneo fulani ambalo hulifahamu, lakini rafiki yako ambaye mnasafiri pamoja analielewa vizuri eneo hilo. Anajua kabisa mahali mlipo na anajua kila barabara katika eneo hilo. Bila shaka, utafurahi kwamba rafiki yako alikubali kusafiri pamoja nawe! Vivyo hivyo, Yehova anajua mahali tulipo katika mkondo wa wakati na mambo yatakayotokea wakati ujao. Basi, ili kuelewa unabii wa Biblia, tunapaswa kumwomba Yehova msaada kwa unyenyekevu. (Dan. 2:28; 2 Pet. 1:​19, 20) Kama mzazi mwenye upendo, Yehova anataka watoto wake wawe na wakati ujao wenye furaha. (Yer. 29:11) Lakini tofauti na wazazi wa kibinadamu, Yehova anaweza kutabiri kuhusu wakati ujao kwa usahihi kabisa. Aliagiza unabii uandikwe katika Neno lake ili tujue matukio muhimu kabla hayajatokea.—Isa. 46:10. w23.08 8 ¶3-4

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumatatu, Septemba 1

Tutapata mapambazuko kutoka juu.—Luka 1:78.

Mungu amempa Yesu nguvu za kutatua matatizo yote ya wanadamu. Kupitia miujiza yake, Yesu alionyesha kwamba ana nguvu za kutatua matatizo yote ambayo hatuwezi kusuluhisha. Kwa mfano, ana uwezo wa kutuweka huru kutoka kwa chanzo cha matatizo ya wanadamu, yaani, dhambi tuliyorithi na matokeo yake, ugonjwa na kifo. (Mt. 9:​1-6; Rom. 5:​12, 18, 19) Miujiza aliyofanya inathibitisha kwamba anaweza kuponya “kila aina ya ugonjwa” na hata kuwafufua wafu. (Mt. 4:23; Yoh. 11:​43, 44) Pia, ana nguvu za kudhibiti dhoruba kali ya upepo na kuwashinda roho waovu. (Marko 4:​37-39; Luka 8:2) Tunafarijika kujua kwamba Yehova amempa Mwana wake nguvu hizo! Tunaweza kuwa na uhakika kabisa kwamba baraka za wakati ujao chini ya Ufalme wa Mungu zitatimia. Miujiza ambayo Yesu alifanya alipokuwa mwanadamu duniani, inatufundisha mambo atakayofanya kwa kiwango kikubwa zaidi akiwa Mfalme wa Ufalme wa Mungu ulio mbinguni. w23.04 3 ¶5-7

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki