Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Leo

Jumatatu, Septemba 22

Fanyeni wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, mkiwabatiza katika jina la Baba na la Mwana.—Mt. 28:19.

Je, Yesu alitaka wengine watumie jina la kibinafsi la Baba yake? Bila shaka. Huenda baadhi ya viongozi wa dini wa siku za Yesu waliamini kwamba jina la Mungu lilikuwa takatifu sana hivi kwamba halikupaswa kutamkwa, lakini Yesu hakuruhusu desturi hizo zisizo za kimaandiko zimzuie kuliheshimu jina la Baba yake. Fikiria wakati ambapo Yesu alimponya mwanamume mwenye roho waovu katika eneo la Wagerasene. Watu katika eneo hilo waliogopa na kumsihi Yesu aondoke, hivyo hakubaki katika eneo hilo. (Marko 5:​16, 17) Lakini bado Yesu alitaka jina la Yehova lijulikane huko. Hivyo, alimwambia mwanamume aliyemponya awaambie watu mambo ambayo Yehova alikuwa amefanya, si mambo ambayo Yesu alikuwa amefanya. (Marko 5:19) Leo pia, anataka tufanye vivyo hivyo, yaani, tuwajulishe watu ulimwenguni pote kuhusu jina la Baba yake! (Mt. 24:14; 28:20) Tunapofanya sehemu yetu, tunamfurahisha Mfalme wetu, Yesu. w24.02 10 ¶10

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumanne, Septemba 23

Umestahimili kwa ajili ya jina langu.—Ufu. 2:3.

Tuna pendeleo kubwa sana kuwa sehemu ya tengenezo la Yehova katika siku hizi za mwisho zilizo ngumu. Hali za ulimwengu zinavyozidi kuzorota, Yehova anatupatia familia ya ndugu na dada iliyo na umoja. (Zab. 133:1) Anatusaidia tuwe na maisha ya familia yenye furaha. (Efe. 5:33–6:1) Na anatupatia ufahamu na hekima tunayohitaji ili tuwe na amani ya kweli ya moyoni na akilini. Hata hivyo, ni lazima tujitahidi ili tuendelee kumtumikia Yehova kwa uaminifu. Kwa nini? Kwa sababu nyakati nyingine tunaweza kukasirishwa na kutokamilika kwa wengine. Pia, tunaweza kuvunjika moyo kwa sababu ya makosa tunayofanya, hasa ikiwa tunarudia makosa yaleyale mara kwa mara. Tunahitaji kuendelea kumtumikia Yehova kwa uaminifu (1) mwabudu mwenzetu anapotukosea, (2) mwenzi wetu wa ndoa anapotuvunja moyo, na (3) tunapovunjika moyo kwa sababu ya makosa yetu. w24.03 14 ¶1-2

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumatano, Septemba 24

Kwa kadiri ambavyo tumefanya maendeleo, na tuendelee kutembea kwa utaratibu katika mwendo huohuo.—Flp. 3:16.

Mara kwa mara, utasikia kuhusu mambo yaliyoonwa ya ndugu na dada ambao wamepanua utumishi wao mtakatifu. Labda walihudhuria Shule ya Waeneza-Injili wa Ufalme au walihamia maeneo yenye uhitaji mkubwa. Ikiwa hali zako zinakuruhusu, hilo ni lengo zuri sana la kujiwekea. Watu wa Yehova wanatafuta fursa mbalimbali za kupanua huduma yao. (Mdo. 16:9) Namna gani ikiwa hali zako za sasa hazikuruhusu kufanya hivyo? Usihisi kwamba wewe ni duni kuliko wale wanaofanya hivyo. (Mt. 10:22) Usisahau kwamba unamfurahisha sana Yehova unapofanya utumishi wake kwa bidii kulingana na uwezo na hali zako. Hiyo ni njia muhimu ya kuendelea kumfuata Yesu baada ya ubatizo.—Zab. 26:1. w24.03 10 ¶11

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki