Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Leo

Jumamosi, Septemba 27

Upendo wa Mungu umemiminwa ndani ya mioyo yetu kupitia roho takatifu, ambayo tulipewa.—Rom. 5:5

Ona neno “umemiminwa” ambalo limetumiwa kwenye andiko la leo. Kitabu kimoja cha marejeo kinalinganisha neno “umemiminwa” na kijito cha maji, yaani, kinachotiririka maji mengi. Mfano huo unaonyesha jinsi Yehova anavyowapenda sana watiwa-mafuta! Watiwa-mafuta wanajua kwamba “wanapendwa na Mungu.” (Yuda 1) Mtume Yohana alieleza hisia zao alipoandika hivi: “Oneni upendo ambao Baba ametuonyesha, kwamba tunapaswa kuitwa watoto wa Mungu!” (1 Yoh. 3:1) Je, Yehova anawapenda tu watiwa-mafuta? La, Yehova amethibitisha upendo wake kwetu sisi sote. Ni nini kinachotuhakikishia zaidi kwamba Yehova anatupenda? Fidia—wonyesho mkubwa zaidi wa upendo katika ulimwengu wote!—Yoh. 3:16; Rom. 5:8. w24.01 28 ¶9-10

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumapili, Septemba 28

Maadui wangu watakimbia siku nitakayoomba msaada. Nina hakika kuhusu jambo hili: Mungu yuko upande wangu.—Zab. 56:9.

Mstari huo unafunua njia iliyomsaidia Daudi kushinda woga wake. Ingawa uhai wake ulikuwa hatarini, alitafakari mambo ambayo Yehova angemfanyia wakati ujao. Daudi alijua kwamba Yehova angemwokoa kwa wakati unaofaa. Isitoshe, Yehova alikuwa ametangaza kwamba Daudi angekuwa mfalme anayefuata wa Israeli. (1 Sam. 16:​1, 13) Daudi alikuwa na uhakika kwamba jambo lolote ambalo Yehova aliahidi lingetimia. Yehova ameahidi atakufanyia nini? Hatutarajii kwamba atukinge kutokana na matatizo yote. Lakini kumbuka kwamba majaribu yoyote ambayo huenda ukakabili katika mfumo huu wa mambo, Yehova atayaondoa katika dunia mpya inayokuja. (Isa. 25:​7-9) Bila shaka Muumba wetu ana nguvu za kufufua wafu, kutuponya, na kuondoa wapinzani wote.—1 Yoh. 4:4. w24.01 6 ¶12-13

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumatatu, Septemba 29

Mwenye furaha ni mtu ambaye amesamehewa kosa lake, ambaye dhambi yake imefunikwa.—Zab. 32:1.

Fikiria kuhusu wakfu na ubatizo wako. Ulichukua hatua hizo kwa sababu ulitaka kusimama upande wa Yehova. Kumbuka mambo ambayo yalikusaidia kusadiki kwamba umepata kweli. Ulipata ujuzi sahihi kumhusu Yehova na ukaanza kumheshimu na kumpenda akiwa Baba yako wa mbinguni. Ulisitawisha imani na ukachochewa kutubu. Moyo wako ulikuchochea kuacha mazoea yasiyofaa na kuishi kulingana na mapenzi ya Mungu. Ulifarijika ulipotambua kwamba Mungu amekusamehe. (Zab. 32:2) Ulihudhuria mikutano ya Kikristo na ukaanza kuwaambia wengine kuhusu mambo mazuri uliyokuwa unajifunza. Sasa ukiwa Mkristo aliyejiweka wakfu na kubatizwa, unatembea kwenye barabara ya uzima ukiwa umeazimia kuendelea kutembea katika barabara hiyo. (Mt. 7:​13, 14) Na usimame imara na thabiti katika ujitoaji wako kwa Yehova na sikuzote uendelee kutii amri zake. w23.07 17 ¶14; 19 ¶19

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki