Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Leo

Jumapili, Septemba 28

Maadui wangu watakimbia siku nitakayoomba msaada. Nina hakika kuhusu jambo hili: Mungu yuko upande wangu.—Zab. 56:9.

Mstari huo unafunua njia iliyomsaidia Daudi kushinda woga wake. Ingawa uhai wake ulikuwa hatarini, alitafakari mambo ambayo Yehova angemfanyia wakati ujao. Daudi alijua kwamba Yehova angemwokoa kwa wakati unaofaa. Isitoshe, Yehova alikuwa ametangaza kwamba Daudi angekuwa mfalme anayefuata wa Israeli. (1 Sam. 16:​1, 13) Daudi alikuwa na uhakika kwamba jambo lolote ambalo Yehova aliahidi lingetimia. Yehova ameahidi atakufanyia nini? Hatutarajii kwamba atukinge kutokana na matatizo yote. Lakini kumbuka kwamba majaribu yoyote ambayo huenda ukakabili katika mfumo huu wa mambo, Yehova atayaondoa katika dunia mpya inayokuja. (Isa. 25:​7-9) Bila shaka Muumba wetu ana nguvu za kufufua wafu, kutuponya, na kuondoa wapinzani wote.—1 Yoh. 4:4. w24.01 6 ¶12-13

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumatatu, Septemba 29

Mwenye furaha ni mtu ambaye amesamehewa kosa lake, ambaye dhambi yake imefunikwa.—Zab. 32:1.

Fikiria kuhusu wakfu na ubatizo wako. Ulichukua hatua hizo kwa sababu ulitaka kusimama upande wa Yehova. Kumbuka mambo ambayo yalikusaidia kusadiki kwamba umepata kweli. Ulipata ujuzi sahihi kumhusu Yehova na ukaanza kumheshimu na kumpenda akiwa Baba yako wa mbinguni. Ulisitawisha imani na ukachochewa kutubu. Moyo wako ulikuchochea kuacha mazoea yasiyofaa na kuishi kulingana na mapenzi ya Mungu. Ulifarijika ulipotambua kwamba Mungu amekusamehe. (Zab. 32:2) Ulihudhuria mikutano ya Kikristo na ukaanza kuwaambia wengine kuhusu mambo mazuri uliyokuwa unajifunza. Sasa ukiwa Mkristo aliyejiweka wakfu na kubatizwa, unatembea kwenye barabara ya uzima ukiwa umeazimia kuendelea kutembea katika barabara hiyo. (Mt. 7:​13, 14) Na usimame imara na thabiti katika ujitoaji wako kwa Yehova na sikuzote uendelee kutii amri zake. w23.07 17 ¶14; 19 ¶19

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumanne, Septemba 30

Mungu ni mwaminifu, naye hatawaacha mjaribiwe kupita mnavyoweza kuhimili, bali pamoja na majaribu hayo ataifanya pia njia ya kutokea ili mweze kuyavumilia.—1 Kor. 10:13.

Ukitafakari sala uliyotoa ulipojiweka wakfu kwa Yehova, utapata nguvu za kushinda kishawishi chochote. Kwa mfano, je, utamchezea kimapenzi mwenzi wa ndoa wa mtu mwingine? Bila shaka hapana! Tayari ulishamwahidi Yehova kwamba hutafanya jambo kama hilo. Ikiwa hutaruhusu tamaa mbaya zisitawi, hutahitaji kupambana baadaye ili kuzing’oa. ‘Utajiepusha’ na “kijia cha waovu.” (Met. 4:​14, 15) Ukikumbuka azimio la Yesu la kumpendeza Baba yake, utakataa haraka na kwa uthabiti jambo lolote ambalo unajua halitampendeza Mungu ambaye umejiweka wakfu kwake. (Mt. 4:10; Yoh. 8:29). Ukweli ni kwamba majaribu na vishawishi vinakupa nafasi ya kuonyesha kwamba umeazimia ‘kuendelea kumfuata’ Yesu. Unapofanya hivyo, unaweza kuwa na uhakika kwamba Yehova atakusaidia. w24.03 9-10 ¶8-10

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki