Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Leo

Jumanne, Septemba 2

Roho huchunguza ndani ya mambo yote, hata mambo mazito ya Mungu.—1 Kor. 2:10.

Ikiwa upo kwenye kutaniko kubwa na unahisi kwamba mara nyingi hupati nafasi ya kutoa maelezo, huenda ukashawishiwa kutoinua mkono tena. Lakini usiache kujitahidi kutoa maelezo. Tayarisha maelezo kadhaa kwa ajili ya kila mkutano. Kisha ikiwa hutachaguliwa kutoa maelezo mwanzoni mwa funzo, bado utakuwa na nafasi nyingine ya kutoa maelezo mkutano unapoendelea. Unapotayarisha Funzo la Mnara wa Mlinzi, fikiria jinsi kila fungu linavyohusiana na kichwa kikuu cha makala. Ukifanya hivyo, inaelekea kwamba utakuwa tayari kutoa maelezo wakati wowote wa funzo. Isitoshe, unaweza kujitayarisha kutoa maelezo katika mafungu ambayo yanazungumzia mafundisho mazito ya Biblia ambayo ni vigumu zaidi kuyaelezea. Kwa nini? Kwa sababu huenda si watu wengi watainua mkono katika sehemu hiyo. Namna gani ikiwa unatambua kwamba baada ya mikutano kadhaa bado hujapata nafasi ya kutoa maelezo? Kabla ya mkutano, mweleze yule anayeongoza swali ambalo ungependa kujibu. w23.04 21-22 ¶9-10

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumatano, Septemba 3

Yosefu akaamka . . . na kufanya kama alivyoambiwa na malaika wa Yehova, akampeleka mke wake nyumbani.—Mt. 1:24.

Yosefu alikuwa tayari kufuata mwongozo wa Yehova, na hilo lilimfanya awe mume mzuri. Katika pindi tatu tofauti, alipata mwongozo kutoka kwa Yehova kuhusu familia yake. Kila mara, alitii bila kusita, hata ilipomaanisha kufanya mabadiliko makubwa. (Mt. 1:20; 2:​13-15, 19-21) Kwa kufuata mwongozo wa Yehova, Yosefu alimlinda Maria, akamtegemeza, na kumwandalia mahitaji yake. Wazia jinsi matendo ya Yosefu yalivyomfanya Maria ampende na kumheshimu hata zaidi! Waume, mnaweza kumwiga Yosefu kwa kutafuta ushauri katika Biblia kuhusu jinsi ya kutunza familia zenu. Unapofuata ushauri huo, hata ikimaanisha kufanya mabadiliko fulani, unaonyesha kwamba unampenda mke wako na unaimarisha ndoa yenu. Dada mmoja nchini Vanuatu ambaye amefunga ndoa kwa zaidi ya miaka 20 anasema hivi: “Mume wangu anapotafuta na kufuata mwongozo wa Yehova, ninamheshimu hata zaidi. Ninajihisi salama, na nina uhakika katika maamuzi anayofanya.” w23.05 21 ¶5

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Alhamisi, Septemba 4

Huko kutakuwa na barabara kuu, naam, njia inayoitwa Njia ya Utakatifu.—Isa. 35:8.

Wayahudi waliorudi kutoka Babiloni walipaswa kuwa “watu watakatifu” kwa Mungu wao. (Kum. 7:6) Hata hivyo, hilo halikumaanisha kwamba hawakuhitaji kufanya mabadiliko ili kumfurahisha Yehova. Wayahudi wengi waliozaliwa huko Babiloni walikuwa wameathiriwa na njia ya kufikiri na mazoea ya Wababiloni. Miaka mingi baada ya kikundi cha kwanza cha Wayahudi kurudi Israeli, Gavana Nehemia alishangaa alipotambua kwamba watoto ambao walikuwa wamezaliwa huko Israeli, hata hawakuwa wamejifunza lugha ya Kiyahudi. (Kum. 6:​6, 7; Neh. 13:​23, 24) Watoto hao wangewezaje kujifunza kumpenda na kumwabudu Yehova ikiwa hawangeweza kuelewa Kiebrania—lugha kuu ambayo ilitumiwa kuandika Neno la Mungu? (Ezra 10:​3, 44) Basi, Wayahudi hao walihitaji kufanya mabadiliko makubwa, lakini ingekuwa rahisi zaidi kwao kufanya mabadiliko hayo wakiwa huko Israeli, ambako ibada safi ilikuwa inarudishwa hatua kwa hatua.—Neh. 8:​8, 9. w23.05 15 ¶6-7

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki