Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Leo

Alhamisi, Septemba 4

Huko kutakuwa na barabara kuu, naam, njia inayoitwa Njia ya Utakatifu.—Isa. 35:8.

Wayahudi waliorudi kutoka Babiloni walipaswa kuwa “watu watakatifu” kwa Mungu wao. (Kum. 7:6) Hata hivyo, hilo halikumaanisha kwamba hawakuhitaji kufanya mabadiliko ili kumfurahisha Yehova. Wayahudi wengi waliozaliwa huko Babiloni walikuwa wameathiriwa na njia ya kufikiri na mazoea ya Wababiloni. Miaka mingi baada ya kikundi cha kwanza cha Wayahudi kurudi Israeli, Gavana Nehemia alishangaa alipotambua kwamba watoto ambao walikuwa wamezaliwa huko Israeli, hata hawakuwa wamejifunza lugha ya Kiyahudi. (Kum. 6:​6, 7; Neh. 13:​23, 24) Watoto hao wangewezaje kujifunza kumpenda na kumwabudu Yehova ikiwa hawangeweza kuelewa Kiebrania—lugha kuu ambayo ilitumiwa kuandika Neno la Mungu? (Ezra 10:​3, 44) Basi, Wayahudi hao walihitaji kufanya mabadiliko makubwa, lakini ingekuwa rahisi zaidi kwao kufanya mabadiliko hayo wakiwa huko Israeli, ambako ibada safi ilikuwa inarudishwa hatua kwa hatua.—Neh. 8:​8, 9. w23.05 15 ¶6-7

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Ijumaa, Septemba 5

Yehova huwategemeza wote wanaoanguka na kuwainua juu wote walioinama chini.—Zab. 145:14.

Inasikitisha kwamba hata tuwe tumechochewa au tuna nidhamu kadiri gani, bado huenda tutakabili vipingamizi vinavyofanya iwe vigumu kufikia malengo yetu. Kwa mfano, “matukio yasiyotarajiwa” yanaweza kuchukua muda tunaohitaji ili tufanyie kazi lengo letu. (Mhu. 9:11) Huenda tukakabili hali ngumu ambayo itatuacha tukiwa tumevunjika moyo na kuishiwa nguvu. (Met. 24:10) Kwa kuwa hatujakamilika, huenda tukafanya makosa ambayo yatafanya iwe vigumu kutimiza lengo letu. (Rom. 7:23) Au huenda tukahisi tu kwamba tumechoka. (Mt. 26:43) Ni nini kinachoweza kutusaidia kushinda vipingamizi au hali ngumu? Kumbuka, kipingamizi hakimaanishi kwamba umeshindwa. Biblia inasema kwamba huenda tukakabili tena na tena matatizo au hali ngumu. Hata hivyo, pia inataja wazi kwamba tunaweza kusimama tena. Naam, ukisonga mbele licha ya vipingamizi, unamthibitishia Yehova kwamba unataka kumfurahisha. Bila shaka, Yehova anafurahi sana anapoona ukijitahidi kutimiza lengo lako! w23.05 30 ¶14-15

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumamosi, Septemba 6

[Iweni] vielelezo kwa kundi.—1 Pet. 5:3.

Upainia unamsaidia mwanamume kijana kujifunza jinsi ya kufanya kazi vizuri pamoja na watu mbalimbali. Pia, unamsaidia kupanga bajeti vizuri na kushikamana nayo. (Flp. 4:​11-13) Njia nzuri ya kuanza utumishi wa wakati wote ni kufanya upainia msaidizi, jambo ambalo litakusaidia kuwa tayari kuanza upainia wa kawaida. Upainia unaweza kufungua mlango unaoongoza kwenye aina nyingine za utumishi wa wakati wote, kutia ndani kutumikia ukiwa mjenzi au Mwanabetheli. Wanaume Wakristo wanapaswa kuwa na lengo la kustahili kuwatumikia ndugu na dada zao wakiwa wazee wa kutaniko. Biblia inasema kwamba wanaume wanaojitahidi kufikia jukumu hilo ‘wanatamani kazi njema.’ (1 Tim. 3:1) Kwanza, ni lazima ndugu astahili kutumikia akiwa mtumishi wa huduma. Watumishi wa huduma wanawasaidia wazee kwa njia nyingi hususa. Wazee na watumishi wa huduma wanawatumikia kwa unyenyekevu ndugu na dada zao na kushiriki kwa bidii katika huduma. w23.12 28 ¶14-16

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki