Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Wapende Wale Ambao Mungu Anawapenda
    “Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
    • KUJIFUNZA KUTOKANA NA MIFANO ILIYO KATIKA BIBLIA

      8. Ni nini kinachokuvutia kuhusu urafiki kati ya (a) Naomi na Ruthu? (b) wale vijana watatu Waebrania? (c) Paulo na Timotheo?

      8 Maandiko yana mifano mingi ya watu waliofaidika kwa kuchagua marafiki wanaofaa. Unaweza kusoma kuhusu urafiki kati ya Naomi na binti-mkwe wake, Ruthu, kati ya wale vijana watatu Waebrania ambao waliendelea kuwa marafiki wakiwa Babiloni, na kati ya Paulo na Timotheo. (Ruthu 1:16; Danieli 3:17, 18; 1 Wakorintho 4:17; Wafilipi 2:20-22) Hata hivyo, acheni tuzungumzie mfano mwingine wa pekee: urafiki kati ya Daudi na Yonathani.

      9, 10. Urafiki kati ya Daudi na Yonathani ulitegemea nini?

      9 Biblia inasema kwamba baada ya Daudi kumuua Goliathi, “nafsi ya Yonathani ikashikamana na nafsi ya Daudi, na Yonathani akaanza kumpenda kama nafsi yake mwenyewe.” (1 Samweli 18:1) Hivyo, urafiki ulio imara ukasitawi ijapokuwa umri wao ulitofautiana sana, na urafiki huo ukaendelea mpaka Yonathani alipokufa vitani.c (2 Samweli 1:26) Urafiki wa karibu kati ya Daudi na Yonathani ulitegemea nini?

      10 Daudi na Yonathani walikuwa marafiki wakubwa kwa sababu walimpenda Mungu na walitamani sana kuendelea kuwa waaminifu kwake. Wote wawili walitaka kumpendeza Mungu. Kila mmoja wao alikuwa na sifa zilizomvutia mwenzake. Bila shaka, Yonathani alivutiwa na uhodari na bidii ya kijana huyo ambaye alitetea jina la Yehova bila woga. Naye Daudi alimheshimu mwanamume huyo aliyekuwa na umri mkubwa kuliko yeye na ambaye aliunga mkono kwa ushikamanifu mipango ya Yehova na kutanguliza mapendezi ya Daudi bila ubinafsi. Kwa mfano, fikiria kilichotukia wakati Daudi alipovunjika moyo akiwa amekimbilia nyikani ili kuhepa ghadhabu ya Mfalme Sauli mwovu, baba ya Yonathani. Yonathani alionyesha ushikamanifu wa pekee alipoamua ‘kwenda kwa Daudi ili autie nguvu mkono wake kuhusiana na Mungu.’ (1 Samweli 23:16) Wazia jinsi Daudi alivyohisi rafiki yake mpendwa alipofika na kumtegemeza na kumtia moyo!d

      11. Unajifunza nini kuhusu urafiki kutokana na mfano wa Yonathani na Daudi?

      11 Tunajifunza nini kutokana na mfano wa Yonathani na Daudi? Jambo kuu tunalojifunza ni kwamba urafiki kati ya watu unapaswa kutegemea hasa urafiki wao pamoja na Mungu. Tunapositawisha urafiki pamoja na wale walio na imani kama yetu, maadili kama yetu, na tamaa kama yetu ya kuendelea kuwa waaminifu kwa Mungu, tunaweza kuzungumza pamoja nao kuhusu maoni, hisia, na mambo yanayotutia moyo na kutujenga. (Waroma 1:11, 12) Tunapata marafiki wa aina hiyo kati ya waabudu wenzetu. Je, hiyo inamaanisha kwamba kila mtu anayehudhuria mikutano kwenye Jumba la Ufalme ni rafiki mzuri? Hapana, haiwi hivyo nyakati zote.

  • Wapende Wale Ambao Mungu Anawapenda
    “Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
    • c Daudi alikuwa kijana—“mvulana tu”—alipomuua Goliathi, na alikuwa na umri wa miaka 30 hivi Yonathani alipokufa. (1 Samweli 17:33; 31:2; 2 Samweli 5:4) Yonathani, ambaye alikuwa na umri wa miaka 60 hivi alipokufa, alikuwa amemzidi Daudi kwa miaka 30 hivi.

      d Kama inavyoonyeshwa katika 1 Samweli 23:17, Yonathani alisema mambo matano ili kumtia moyo Daudi: (1) Alimsihi Daudi asiogope. (2) Alimhakikishia Daudi kwamba Sauli hangefanikiwa. (3) Alimkumbusha Daudi kwamba atapokea ufalme, kama Mungu alivyoahidi. (4) Aliahidi kwamba atakuwa mshikamanifu kwa Daudi. (5) Alimwambia Daudi kwamba hata Sauli anajua kwamba yeye ni mshikamanifu kwa Daudi.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki