-
“Kutetea na Kuthibitisha Kisheria Habari Njema”Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Vizuizi Vikali Mikononi mwa Mahakama
Suala la kusalimu bendera kama lilivyohusu watoto wa shule wa Mashahidi wa Yehova lilifika kwa mara ya kwanza kwenye mahakama za Amerika mwaka wa 1935 katika kesi ya Carlton B. Nicholls v. Mayor and School Committee of Lynn (Massachusetts).f Kesi hiyo ilipelekwa kwenye Mahakama Kuu Zaidi ya Massachusetts. Katika 1937, mahakama iliamua, kwamba hata iwe ni nini ambayo Carleton Nichols, Jr., na wazazi wake walisema waliamini, imani ya kidini haikuhusika, kwa sababu ilisema, “salamu ya bendera na kiapo cha ushikamanifu yanayozungumziwa hapa hayahusu dini katika njia yoyote ifaayo. . . . Hayahusu maoni ya mtu yeyote kwa Muumba wake. Hayahusu uhusiano wake na Mfanyi wake.” Wakati suala la kusalimu bendera kwa lazima lilipokatiwa rufani kwenye Mahakama Kuu Zaidi ya Marekani katika kesi ya Leoles v. Landersg katika 1937, na tena katika Hering v. State Board of Educationh katika 1938, Mahakama ilitupilia mbali kesi hizo kwa sababu kwa maoni yayo, hilo halikuwa suala la maana la kitaifa kuweza kujadiliwa. Katika 1939 Mahakama tena ilitupilia mbali rufani iliyohusu suala lilo hilo, katika kesi ya Gabrielli v. Knickerbocker.i Siku iyo hiyo, bila kusikiza hoja za maneno, walikubali uamuzi usiopendeleka wa mahakama ya chini katika kesi ya Johnson v. Town of Deerfield.j
Hatimaye, katika 1940, Mahakama ilisikiliza kikamili kesi iliyoitwa Minersville School District v. Gobitis.k Kundi kubwa la mawakili mashuhuri walitoa hoja katika kesi hiyo kwa pande zote. J. F. Rutherford alitoa hoja ya maneno kwa niaba ya Walter Gobitas na watoto wake. Mshiriki wa idara ya sheria ya Chuo Kikuu cha Harvard aliwakilisha Shirika la Mawakili wa Marekani na Chama cha Kutetea Uhuru wa Raia katika kutoa hoja dhidi ya kusalimu bendera kwa lazima. Hata hivyo, hoja zao zilikataliwa, na kukiwa na mmoja tu aliyekuwa na maoni tofauti, Mahakama Kuu Zaidi iliamua mnamo Juni 3, kwamba watoto ambao hawangesalimu bendera wangefukuzwa kutoka shule za umma.
-
-
“Kutetea na Kuthibitisha Kisheria Habari Njema”Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Karibu mwezi mmoja baadaye—mnamo Juni 14, Siku ya Bendera ya kila mwaka ya taifa—Mahakama Kuu Zaidi tena ilibadili uamuzi wayo, wakati huu kuhusiana na uamuzi katika kesi ya Gobitis, wakifanya hivyo katika kesi iliyoitwa West Virginia State Board of Education v. Barnette.c Iliamua kwamba “hakuna ofisa, wa juu au wa chini, awezaye kuonyesha yale yanayokubalika na ya kweli katika siasa, utukuzo wa taifa, dini, au mambo mengineyo au kuwalazimisha raia waungame kwa maneno au watende kupatana na imani yao.” Hoja nyingi zilizotolewa katika uamuzi huo zilitumiwa baadaye nchini Kanada na Mahakama ya Rufani ya Ontario katika kesi ya Donald v. Hamilton Board of Education, na Mahakama Kuu Zaidi ya Kanada ilikataa kubatilisha uamuzi huo.
Kupatana na uamuzi wayo katika kesi ya Barnette, na katika siku hiyohiyo, katika kesi ya Taylor v. State of Mississippi,d Mahakama Kuu Zaidi ya Marekani iliamua kwamba Mashahidi wa Yehova hawangeweza kwa kufaa kushtakiwa uhaini kwa kueleza sababu zao za kutosalimu bendera na kwa kufundisha kwamba mataifa yote yako upande wa ushinde kwa sababu yanapinga Ufalme wa Mungu. Maamuzi hayo pia yalitayarisha njia kwa maamuzi yaliyofuata yenye kupendeleka katika mahakama nyinginezo katika kesi zilizohusu wazazi Mashahidi ambao watoto wao walikuwa wamekataa kusalimu bendera shuleni, pamoja na katika masuala yaliyohusu uajiri na utunzi wa watoto. Hali ilikuwa imebadilika kabisa.e
-
-
“Kutetea na Kuthibitisha Kisheria Habari Njema”Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
[Sanduku katika ukurasa wa 684]
Ushahidi kwa Mahakama Kuu Zaidi ya Marekani
Alipotokea mbele ya Mahakama Kuu Zaidi ya Marekani akiwa mshauri wa kisheria katika kesi ya “Gobitis,” Joseph F. Rutherford, mshiriki wa Shirika la Mawakili wa New York na msimamizi wa Watch Tower Society, alikazia fikira waziwazi juu ya umaana wa kujinyenyekeza kwa utawala wa Yehova Mungu. Yeye alisema:
“Mashahidi wa Yehova ni wale wanaotoa ushuhuda kwa jina la Mungu Mweza Yote, ambaye jina lake pekee ni YEHOVA. . . .
“Ninaelekeza fikira kwenye uhakika wa kwamba Yehova Mungu, aliahidi miaka zaidi ya elfu sita iliyopita, juu ya kusimamisha serikali ya uadilifu kupitia Mesiya. Atatimiza ahadi hiyo kwa wakati wake. Mambo ya hakika ya siku za leo kulingana na unabii yanaonyesha kwamba wakati huo u karibu. . . .
“Mungu, Yehova, ndiye chanzo pekee cha uhai. Hakuna mtu mwingine anayeweza kutoa uhai. Jimbo la Pennsylvania haliwezi kutoa uhai. Serikali ya Amerika haiwezi. Mungu alifanya sheria hii [kukataza ibada ya sanamu], kama vile Paulo anavyosema, ili kulinda salama watu Wake na ibada ya sanamu. Mnasema hilo ni jambo dogo. Na ndivyo lilivyokuwa lile tendo la Adamu la kula tunda lililokatazwa. Si lile tofaa alilokula Adamu, bali ni lile tendo lake la kutomtii Mungu. Suala ni ikiwa mwanadamu atamtii Mungu au atatii mfumo fulani wa kibinadamu. . . .
“Ninakumbusha Mahakama hii (si lazima nifanye hivyo) kwamba katika kesi ya ‘Church v. United States’ Mahakama hii ilisema kwamba Amerika ni taifa la Kikristo; na hiyo inamaanisha kwamba ni lazima Amerika itii sheria ya Kimungu. Pia inamaanisha kwamba Mahakama hii inatambua kisheria uhakika wa kwamba sheria ya Mungu ndiyo kuu zaidi. Na ikiwa mtu anaamini kwa kudhamiria kwamba sheria ya Mungu ni kuu zaidi na anajiendesha mwenyewe kwa kudhamiria kulingana nayo, hakuna mamlaka ya kibinadamu inayoweza kudhibiti au kuingilia dhamiri yake. . . .
“Naomba nikubaliwe kuelekeza fikira kwenye jambo hili: kwamba mwanzoni mwa kila kikao cha Mahakama hii mtangazaji hutangaza maneno haya: ‘Mungu okoa Marekani na Mahakama hii inayoheshimika.’ Na sasa ninasema, Mungu okoa Mahakama hii inayostahika isitende kosa litakaloongoza watu hawa wa Marekani kuwa jamii yenye mamlaka kamili na kuharibu uhuru wote unaohakikishiwa na Katiba. Hili ni jambo lililo takatifu kwa kila Mwamerika anayempenda Mungu na Neno Lake.”
[Sanduku katika ukurasa wa 687]
Matukio Yaliyotangulia Kubadilishwa kwa Uamuzi
Katika 1940, wakati Mahakama Kuu Zaidi ya Amerika ilipoamua, katika kesi ya “Minersville School District v. Gobitis,” kwamba watoto wa shule wangetakiwa kusalimu bendera, mahakimu wanane kati ya tisa waliunga mkono uamuzi huo. Ni Hakimu Stone pekee aliyepinga. Lakini miaka miwili baadaye, walipokuwa wakiandikisha tofauti zao katika kesi ya “Jones v. Opelika,” mahakimu wengine watatu (Black, Douglas, na Murphy) walitumia pindi hiyo kusema kwamba waliamini kwamba kesi ya “Gobitis” ilikuwa imeamuliwa vibaya kwa sababu ilikuwa imeshusha uhuru wa kidini. Hiyo ilimaanisha kwamba mahakimu wanne kati ya tisa waliunga mkono kubadilishwa kwa uamuzi katika kesi ya “Gobitis.” Mawakili wawili kati ya wale watano waliokuwa wamepuuza uhuru wa kidini walistaafu. Kulikuwa na wengine wawili wapya (Rutledge na Jackson) wakati kesi iliyofuata ya kusalimu bendera ilipopelekwa kwenye Mahakama Kuu Zaidi. Katika 1943, katika kesi ya “West Virginia State Board of Education v. Barnette,” wote wawili waliunga mkono uhuru wa kidini badala ya jambo la kushurutishwa kusalimu bendera. Hivyo, huku mahakimu 6 dhidi ya 3 zikiunga mkono, mahakama ilibadilisha msimamo iliyokuwa imechukua katika kesi tano za mapema (“Gobitis,” “Leoles,” “Hering,” “Gabrielli,” na “Johnson”) zilizokuwa zimekatwa rufani katika Mahakama hiyo.
Kwa kupendeza, katika kupinga uamuzi wa kesi ya “Barnette,” Hakimu Frankfurter alisema hivi: “Kama vile imekuwa katika nyakati zilizopita, Mahakama itabadilisha msimamo wayo mara kwa mara. Lakini ninaamini kwamba Mahakama hii haijapata kamwe kubatilisha maamuzi yayo ili kupunguza uwezo wa serikali ya kidemokrasia, kabla ya kesi hizi za Mashahidi wa Yehova (isipokuwa mabadiliko madogomadogo yaliyopatikana baadaye).”
-
-
“Kutetea na Kuthibitisha Kisheria Habari Njema”Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
[Picha katika ukurasa wa 686]
Mahakimu wa Mahakama Kuu Zaidi ya Marekani ambao, 6 dhidi ya 3 walikataa jambo la kushurutishwa kusalimu bendera katika kesi ya “Barnette,” wakiunga mkono uhuru wa ibada. Hiyo ilibatilisha uamuzi wa mapema wa Mahakama iyo hiyo katika kesi ya “Gobitis”
Watoto walio- husika katika kesi hizo
Lillian na William Gobitas
Marie na Gathie Barnette
-