Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • 2 Samweli 17
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika 2 Samweli

      • Hushai anavuruga shauri la Ahitofeli (1-14)

      • Daudi anaonywa; anamuponyoka Absalomu (15-29)

        • Barzilai na wengine wanaleta vyakula (27-29)

2 Samweli 17:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “akiwa zaifu katika mikono yote mbili.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Sa. 16:14
  • +Zab 37:12; 41:9; 55:12, 13

2 Samweli 17:5

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Sa. 15:32; 16:16

2 Samweli 17:7

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Sa. 15:34

2 Samweli 17:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “wako na uchungu wa nafsi.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 16:18; 2 Sa. 15:18; 23:8, 18; 1Nya 11:26
  • +Mez. 17:12
  • +1 Sa. 17:50; 18:7; 19:8; 2 Sa. 10:18

2 Samweli 17:9

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “mashimo; mabonde.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 22:1; 23:19

2 Samweli 17:10

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mwa 49:9; 2 Sa. 1:23; Isa 31:4
  • +1 Sa. 18:5

2 Samweli 17:11

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Amu 20:1
  • +1 Fal. 4:20

2 Samweli 17:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “ameamuru.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mez. 21:1
  • +2 Sa. 15:31, 34; 16:23; Mez. 19:21; 21:30
  • +Kum 2:30; 2Nya 25:20

2 Samweli 17:15

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Sa. 8:17; 15:35

2 Samweli 17:16

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “watamezwa.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Zab 35:24, 25

2 Samweli 17:17

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 1:42
  • +2 Sa. 15:27, 36; 18:19
  • +Yosh. 15:7, 12; 18:16, 20; 1 Fal. 1:9

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    ‘Nchi Nzuri’, uku. 20-21

2 Samweli 17:18

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Sa. 16:5; 19:16

2 Samweli 17:20

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 1:19; Yosh. 2:3-5; 1 Sa. 19:12, 14; 21:2

2 Samweli 17:21

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Sa. 17:1, 2

2 Samweli 17:23

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “akajinyonga.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yosh. 15:20, 51; 2 Sa. 15:12
  • +2 Fal. 20:1
  • +1 Sa. 31:4; 1 Fal. 16:18; Zab 5:10; 55:23; Mt 27:3, 5; Mdo 1:18

2 Samweli 17:24

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mwa 32:1, 2; Yosh. 13:24, 26

2 Samweli 17:25

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Sa. 19:13; 20:4, 10
  • +2 Sa. 8:16
  • +1Nya 2:16, 17

2 Samweli 17:26

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 32:1; Kum 3:15

2 Samweli 17:27

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 3:11; Yosh. 13:24, 25; 2 Sa. 12:26, 29
  • +2 Sa. 9:3-5
  • +2 Sa. 19:31, 32; 1 Fal. 2:7

2 Samweli 17:29

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “fromage.” Tnn., “maziwa ya ngombe yenye kuganda.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mez. 11:25
  • +1 Sa. 25:18; 2 Sa. 16:2

Maandiko ingine

2 Sam. 17:22 Sa. 16:14
2 Sam. 17:2Zab 37:12; 41:9; 55:12, 13
2 Sam. 17:52 Sa. 15:32; 16:16
2 Sam. 17:72 Sa. 15:34
2 Sam. 17:81 Sa. 16:18; 2 Sa. 15:18; 23:8, 18; 1Nya 11:26
2 Sam. 17:8Mez. 17:12
2 Sam. 17:81 Sa. 17:50; 18:7; 19:8; 2 Sa. 10:18
2 Sam. 17:91 Sa. 22:1; 23:19
2 Sam. 17:10Mwa 49:9; 2 Sa. 1:23; Isa 31:4
2 Sam. 17:101 Sa. 18:5
2 Sam. 17:11Amu 20:1
2 Sam. 17:111 Fal. 4:20
2 Sam. 17:14Mez. 21:1
2 Sam. 17:142 Sa. 15:31, 34; 16:23; Mez. 19:21; 21:30
2 Sam. 17:14Kum 2:30; 2Nya 25:20
2 Sam. 17:152 Sa. 8:17; 15:35
2 Sam. 17:16Zab 35:24, 25
2 Sam. 17:171 Fal. 1:42
2 Sam. 17:172 Sa. 15:27, 36; 18:19
2 Sam. 17:17Yosh. 15:7, 12; 18:16, 20; 1 Fal. 1:9
2 Sam. 17:182 Sa. 16:5; 19:16
2 Sam. 17:20Kut 1:19; Yosh. 2:3-5; 1 Sa. 19:12, 14; 21:2
2 Sam. 17:212 Sa. 17:1, 2
2 Sam. 17:23Yosh. 15:20, 51; 2 Sa. 15:12
2 Sam. 17:232 Fal. 20:1
2 Sam. 17:231 Sa. 31:4; 1 Fal. 16:18; Zab 5:10; 55:23; Mt 27:3, 5; Mdo 1:18
2 Sam. 17:24Mwa 32:1, 2; Yosh. 13:24, 26
2 Sam. 17:252 Sa. 19:13; 20:4, 10
2 Sam. 17:252 Sa. 8:16
2 Sam. 17:251Nya 2:16, 17
2 Sam. 17:26Hes 32:1; Kum 3:15
2 Sam. 17:27Kum 3:11; Yosh. 13:24, 25; 2 Sa. 12:26, 29
2 Sam. 17:272 Sa. 9:3-5
2 Sam. 17:272 Sa. 19:31, 32; 1 Fal. 2:7
2 Sam. 17:29Mez. 11:25
2 Sam. 17:291 Sa. 25:18; 2 Sa. 16:2
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
2 Samweli 17:1-29

Cha Pili cha Samweli

17 Kisha Ahitofeli akamuambia Absalomu: “Tafazali, acha nichague watu elfu kumi na mbili (12 000) na nisimame na kumufuatilia Daudi usiku wa leo. 2 Nitamukuta akiwa amechoka na bila nguvu,*+ na nitamutia woga; na watu wote wenye kuwa pamoja naye watakimbia, na nitamupiga na kumuua mufalme peke yake.+ 3 Kisha nitarudisha watu wote kwako. Kurudia kwa watu wote kunategemea jambo lenye litamupata mutu mwenye uko unatafuta. Kisha watu wote watakuwa na amani.” 4 Pendekezo hilo lilikuwa sawa kabisa mbele ya macho ya Absalomu na wazee wote wa Israeli.

5 Lakini, Absalomu akasema: “Tafazali muite pia Hushai+ Mwarki, na tusikie jambo lenye atasema.” 6 Kwa hiyo Hushai akakuja kwa Absalomu. Kisha Absalomu akamuambia: “Hili ndilo shauri lenye Ahitofeli alitoa. Je, tufuate shauri lake? Ikiwa hapana, wewe utuambie.” 7 Basi Hushai akamuambia Absalomu: “Shauri lenye Ahitofeli alitoa haliko la muzuri wakati huu!”+

8 Hushai akaendelea kusema: “Unajua muzuri kwamba baba yako na wanaume wake wako na nguvu,+ na wamekata tamaa* kama vile dubu mwenye amepoteza watoto wake katika pori.+ Tena, baba yako ni mupiganaji-vita,+ na hatakaa usiku wote pamoja na watu. 9 Sasa hivi amejificha ndani ya moja la mapango* ao mahali pengine;+ na kama atakuwa wa kwanza kushambulia, wale wenye watasikia habari hiyo watasema, ‘Watu wenye kumufuata Absalomu wameshindwa!’ 10 Hata mwanaume hodari mwenye moyo wake uko kama wa simba+ hakika utayeyuka kwa sababu ya woga, kwa maana Israeli wote wanajua kwamba baba yako ni mwanaume mwenye nguvu+ na kwamba wanaume wenye kuwa pamoja naye wako hodari. 11 Ninatoa shauri hili: Acha Israeli wote wakusanyike kwako, kuanzia Dani mupaka Beer-sheba,+ wengi kama chembe za muchanga pembeni ya bahari,+ na uwaongoze katika vita. 12 Tutamushambulia mahali popote penye atapatikana, na tutakuja juu yake kama vile umande unaanguka kwenye udongo; na hakuna hata mumoja wao mwenye ataokoka, wala yeye wala mumoja wa watu wenye kuwa pamoja naye. 13 Kama anakimbilia katika muji fulani, Israeli wote watapeleka kamba katika muji huo, na tutaukokota mupaka katika bonde, na hakuna hata jiwe la kidogo lenye litabakia.”

14 Basi Absalomu na watu wote wa Israeli wakasema: “Shauri la Hushai Mwarki liko la muzuri zaidi+ kuliko shauri la Ahitofeli!” Kwa maana Yehova alikuwa ameazimia* kuvuruga shauri la muzuri la Ahitofeli,+ ili Yehova alete musiba juu ya Absalomu.+

15 Kisha wakati fulani Hushai akamuambia Sadoki na Abiatari+ makuhani: “Ni hivi Ahitofeli alimushauri Absalomu na wazee wa Israeli, na ni hivi nilishauri. 16 Sasa mutume ujumbe haraka kwa Daudi na kumuonya: ‘Usibakie kwenye nafasi za kuvukia za jangwa usiku wa leo, lakini vuka kabisa, kama hafanye vile, mufalme na watu wote wenye kuwa pamoja naye wataharibiwa.’”*+

17 Yonatani+ na Ahimaazi+ walikuwa wanakaa En-rogeli;+ basi mutumishi mumoja mwanamuke akaenda na kuwaambia, nao wakaenda kumuambia Mufalme Daudi, kwa maana hawakupima kuonekana wakiingia katika muji. 18 Lakini, kijana mumoja mwanaume akawaona na kumuambia Absalomu. Basi wote wawili wakaenda haraka na kufika kwenye nyumba ya mutu fulani kule Bahurimu+ mwenye alikuwa na kisima katika kiwanja chake. Wakashukia ndani ya kisima, 19 na bibi ya mwanaume huyo akatandika kifuniko juu ya kisima hicho na kukifunika kwa nafaka yenye kupondwa-pondwa; hakuna mwenye alijua kuhusu jambo hilo. 20 Watumishi wa Absalomu wakakuja kwa mwanamuke huyo kwenye nyumba yake na kuuliza: “Ahimaazi na Yonatani wako wapi?” Mwanamuke huyo akajibu: “Walipita hapa wakaenda kwenye maji.”+ Kisha watu hao wakawatafuta lakini hawakuwapata, basi wakarudia Yerusalemu.

21 Kisha watu hao kuenda, walitoka katika kisima na kuenda na kumujulisha Mufalme Daudi. Wakamuambia: “Musimame na muvuke haraka maji haya, kwa maana hili ndilo shauri lenye Ahitofeli alitoa juu yenu.”+ 22 Mara moja Daudi na watu wote wenye walikuwa pamoja naye wakasimama na kuvuka Yordani. Kufikia asubui sana, hakuna hata mutu mumoja mwenye hakukuwa amevuka Yordani.

23 Wakati Ahitofeli aliona kwamba shauri lake halikufuatwa, akatandika punda na kuenda kwenye nyumba yake katika muji wake.+ Kisha kupatia watu wa nyumba yake maagizo,+ akajitundika.*+ Basi akakufa na kuzikwa mahali kwenye mababu zake walizikwa.

24 Wakati huo, Daudi akaenda Mahanaimu,+ na Absalomu akavuka Yordani pamoja na watu wote wa Israeli. 25 Absalomu akamuweka Amasa+ kuwa musimamizi wa jeshi pa nafasi ya Yoabu;+ Amasa alikuwa mwana wa mwanaume mwenye kuitwa Itra Mwisraeli, mwenye alilala na Abigaili,+ binti ya Nahashi, dada ya Seruya, mama ya Yoabu. 26 Israeli na Absalomu wakapiga kambi katika inchi ya Gileadi.+

27 Wakati tu Daudi alifika Mahanaimu, Shobi mwana wa Nahashi kutoka muji wa Raba+ wa Waamoni, Makiri+ mwana wa Amieli kutoka Lo-debari, na Barzilai+ Mugileadi kutoka Rogelimu 28 wakaleta vitanda, beseni, vyungu vya udongo, ngano, shayiri, unga, nafaka yenye kukaangwa, maharagi ya munene-munene, dengu, nafaka yenye kukauka, 29 asali, siagi, kondoo, na jibini.* Walileta vitu hivyo vyote kwa ajili ya Daudi na watu wenye walikuwa pamoja naye ili wakule,+ kwa maana walisema: “Watu wamesikia njaa na wamechoka na wako na kiu katika jangwa.”+

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine