Cha Pili cha Samweli
9 Kisha Daudi akasema: “Je, kungali mutu fulani wa nyumba ya Sauli mwenye ninaweza kuonyesha upendo mushikamanifu kwa ajili ya Yonatani?”+ 2 Sasa kulikuwa mutumishi wa nyumba ya Sauli mwenye aliitwa Siba.+ Kwa hiyo wakamuita akuje kwa Daudi, na mufalme akamuuliza: “Wewe ni Siba?” Akajibu: “Mimi ni mutumishi wako.” 3 Mufalme akaendelea kusema: “Je, kungali mutu fulani wa nyumba ya Sauli mwenye ninaweza kuonyesha upendo mushikamanifu wa Mungu?” Siba akamujibu mufalme: “Kungali mwana mumoja wa Yonatani; ni kilema wa miguu yote mbili.”+ 4 Mufalme akamuuliza: “Iko* wapi?” Siba akamujibu mufalme: “Iko* katika nyumba ya Makiri+ mwana wa Amieli kule Lo-debari.”
5 Mara moja Mufalme Daudi akamuitisha na akamutosha katika nyumba ya Makiri mwana wa Amieli kule Lo-debari. 6 Wakati Mefibosheti mwana wa Yonatani mwana wa Sauli alifika mbele ya Daudi, mara moja akaanguka uso chini na kuinama uso chini. Kisha Daudi akasema: “Mefibosheti!” naye akajibu: “Mimi huyu mutumishi wako.” 7 Daudi akamuambia: “Usiogope, kwa maana hakika nitakuonyesha upendo mushikamanifu+ kwa ajili ya Yonatani baba yako, na nitakurudishia udongo wote wa Sauli babu yako, na utakula chakula* kwenye meza yangu sikuzote.”+
8 Basi akainama uso chini na kusema: “Mutumishi wako ni nani, hivi kwamba umegeuza uangalifu* wako kuelekea imbwa mwenye kufa+ kama mimi?” 9 Sasa mufalme akamuitisha Siba, mutumishi wa Sauli, na akamuambia: “Kila kitu chenye kilikuwa cha Sauli na cha nyumba yake yote ninamupatia mujukuu wa bwana wako.+ 10 Utalima udongo kwa ajili yake—wewe na wana wako na watumishi wako—na mutakusanya mavuno ya udongo huo ili watu wa mujukuu wa bwana wako wapate chakula. Lakini Mefibosheti, mujukuu wa bwana wako, atakula chakula kwenye meza yangu sikuzote.”+
Sasa Siba alikuwa na wana kumi na tano (15) na watumishi makumi mbili (20).+ 11 Basi Siba akamuambia mufalme: “Mutumishi wako atafanya mambo yote yenye bwana wangu mufalme anaamuru mutumishi wake afanye.” Kwa hiyo Mefibosheti akakuwa anakula kwenye meza ya Daudi* kama mumoja wa wana wa mufalme.” 12 Sasa Mefibosheti pia alikuwa na kijana mwanaume mwenye aliitwa Mika;+ na watu wote wenye waliishi katika nyumba ya Siba wakakuwa watumishi wa Mefibosheti. 13 Na Mefibosheti aliishi Yerusalemu, kwa maana sikuzote alikula kwenye meza ya mufalme;+ na alikuwa kilema wa miguu yote mbili.+