Cha Kwanza cha Wafalme
1 Sasa Mufalme Daudi alikuwa amezeeka,+ alikuwa ameishi miaka mingi,* na hata kama walikuwa wanamufunika kwa nguo, hakuweza kupata joto. 2 Kwa hiyo watumishi wake wakamuambia: “Kijana mwanamuke, bikira, atafutwe kwa ajili ya bwana wangu mufalme, na atamutumikia mufalme akiwa mutunzaji wake. Atalala katika mikono yako ili bwana wangu mufalme apate joto.” 3 Wakatafuta katika eneo lote la Israeli kijana mwanamuke mwenye sura na umbo ya muzuri, na wakapata Abishagi+ Mushunamu+ na wakamuleta ndani kwa mufalme. 4 Kijana huyo mwanamuke alikuwa mwenye sura na umbo ya muzuri sana, na akakuwa mutunzaji wa mufalme na alikuwa anamutumikia, lakini mufalme hakufanya naye ngono.
5 Wakati ule, Adoniya+ mwana wa Hagiti alikuwa anajiinua, kwa kusema: “Nitakuwa mufalme!” Alijitengenezea gari na akakuwa na wapanda-farasi na wanaume makumi tano (50) wa kukimbia mbele yake.+ 6 Lakini baba yake alikuwa hajamukemea* hata siku moja kwa kusema: “Sababu gani umefanya hivi?” Alikuwa pia na sura ya muzuri sana, na mama yake alimuzaa kisha Absalomu. 7 Alizungumuza na Yoabu mwana wa Seruya na Abiatari+ kuhani, na wakamusaidia Adoniya na kumuunga mukono.+ 8 Lakini Sadoki+ kuhani, Benaya+ mwana wa Yehoyada, Natani+ nabii, Shimei,+ Rei, na wale wapiganaji-vita+ wenye nguvu wa Daudi hawakumuunga Adoniya mukono.
9 Mwishowe Adoniya akatoa zabihu+ za kondoo, ngombe, na wanyama wenye kunenepa pembeni ya jiwe la Zoheleti, lenye kuwa karibu na En-rogeli, na akaalika ndugu zake wote wana wa mufalme, na wanaume wote wa Yuda watumishi wa mufalme. 10 Lakini hakualika Natani nabii, Benaya na wale wapiganaji-vita wenye nguvu, ao Sulemani ndugu yake. 11 Kisha Natani+ akamuambia Bat-sheba,+ mama ya Sulemani:+ “Je, haukusikia kwamba Adoniya+ mwana wa Hagiti amekuwa mufalme, na bwana wetu Daudi hajue jambo lolote kuhusu hilo? 12 Sasa kuja, tafazali, nikupatie shauri, ili uokoe uzima wako mwenyewe na uzima wa* mwana wako Sulemani.+ 13 Uende uingie kwa Mufalme Daudi na umuambie, ‘Je, haiko wewe, bwana wangu mufalme, ndiye ulimuapia mutumishi wako, kwa kusema: “Mwana wako Sulemani atakuwa mufalme kisha mimi, na yeye ndiye atakaa kwenye kiti changu cha ufalme”?+ Basi sababu gani Adoniya amekuwa mufalme?’ 14 Wakati utakuwa ungali pale ukisema na mufalme, nitaingia nyuma yako na kuhakikisha maneno yako.”
15 Kwa hiyo Bat-sheba akaingia kwa mufalme, katika chumba chake cha ndani. Mufalme alikuwa amezeeka sana, na Abishagi+ Mushunamu alikuwa anamutumikia mufalme. 16 Kisha Bat-sheba akainama na kushusha uso chini mbele ya mufalme, na mufalme akasema: “Ombi lako ni nini?” 17 Akajibu: “Bwana wangu, wewe ndiye ulimuapia mutumishi wako kwa jina la Yehova Mungu wako, ‘Mwana wako Sulemani atakuwa mufalme kisha mimi, na yeye ndiye atakaa kwenye kiti changu cha ufalme.’+ 18 Lakini angalia! Adoniya amekuwa mufalme, na bwana wangu mufalme hajue jambo lolote kuhusu hilo.+ 19 Alitoa zabihu za ngombe-dume, wanyama wenye kunenepa, na kondoo wengi sana na alialika wana wote wa mufalme na Abiatari kuhani na Yoabu mukubwa wa jeshi;+ lakini hakumualika mutumishi wako Sulemani.+ 20 Na sasa, bwana wangu mufalme, macho ya Israeli wote yako juu yako ili uwaambie ni nani mwenye atakaa kwenye kiti cha ufalme cha bwana wangu mufalme kisha yeye. 21 Kama haufanye vile, wakati tu bwana wangu mufalme atalala na kupumuzika pamoja na mababu zake, mimi na pia mutoto wangu Sulemani tutaonwa kuwa wasaliti.”
22 Na wakati alikuwa angali anasema na mufalme, Natani nabii akaingia.+ 23 Mara moja mufalme akaambiwa hivi: “Angalia Natani nabii!” Akaingia mbele ya mufalme na akainamisha uso wake mupaka chini mbele ya mufalme. 24 Kisha Natani akasema: “Bwana wangu mufalme, je, ulisema, ‘Adoniya atakuwa mufalme kisha mimi, na yeye ndiye atakaa kwenye kiti changu cha ufalme’?+ 25 Kwa maana leo ameshuka kuenda kutoa zabihu+ za ngombe-dume, wanyama wenye kunenepa, na kondoo wengi sana, na alialika wana wote wa mufalme na wakubwa wa jeshi na Abiatari kuhani.+ Wako kule wanakula na kunywa pamoja naye, na wanaendelea kusema, ‘Mufalme Adoniya aishi siku nyingi!’ 26 Lakini hakunialika mimi, mutumishi wako, wala Sadoki kuhani, wala Benaya+ mwana wa Yehoyada, wala Sulemani mutumishi wako. 27 Je, bwana wangu mufalme ameruhusu jambo hili bila kumuambia mutumishi wako ni nani mwenye anapaswa kukaa kwenye kiti cha ufalme cha bwana wangu mufalme kisha yeye?”
28 Sasa Mufalme Daudi akajibu: “Muniitie Bat-sheba.” Basi akaingia na kusimama mbele ya mufalme. 29 Kisha mufalme akaapa kiapo: “Kama vile hakika Yehova anaishi, yeye mwenye aliniokoa* kutoka katika taabu yote,+ 30 kama vile nilikuapia kwa Yehova Mungu wa Israeli, nikisema, ‘Sulemani mwana wako atakuwa mufalme kisha mimi, na yeye ndiye atakaa kwenye kiti changu cha ufalme pa nafasi yangu!’ ni vile nitafanya siku hii.” 31 Halafu Bat-sheba akainama na kushusha uso wake mupaka chini mbele ya mufalme na kusema: “Bwana wangu Mufalme Daudi aishi milele!”
32 Mara moja Mufalme Daudi akasema: “Muniitie Sadoki kuhani, Natani nabii, na Benaya+ mwana wa Yehoyada.”+ Basi wakaingia mbele ya mufalme. 33 Mufalme akawaambia: “Muende pamoja na watumishi wa bwana wenu, na mupandishe mutoto wangu Sulemani juu ya nyumbu* wangu mwenyewe,+ na mumushushe mupaka Gihoni.+ 34 Sadoki kuhani na Natani nabii watamutia mafuta+ kule akuwe mufalme juu ya Israeli; kisha mupige baragumu na kusema, ‘Mufalme Sulemani aishi siku nyingi!’+ 35 Kisha mumufuate nyuma, na ataingia na kukaa kwenye kiti changu cha ufalme; na atakuwa mufalme pa nafasi yangu, na nitamupatia daraka la kuwa kiongozi juu ya Israeli na juu ya Yuda.” 36 Mara moja Benaya mwana wa Yehoyada akamuambia mufalme: “Amina! Yehova Mungu wa bwana wangu mufalme ahakikishe jambo hilo. 37 Kama vile Yehova alikuwa pamoja na bwana wangu mufalme, basi akuwe pia pamoja na Sulemani,+ na Yeye afanye kiti chake cha ufalme kikuwe kikubwa zaidi kuliko kiti cha ufalme cha bwana wangu Mufalme Daudi.”+
38 Kisha Sadoki kuhani, Natani nabii, Benaya+ mwana wa Yehoyada, na Wakereti na Wapeleti+ wakashuka na wakamupandisha Sulemani juu ya nyumbu wa Mufalme Daudi,+ na wakamupeleka mupaka Gihoni.+ 39 Kisha Sadoki kuhani akakamata pembe ya mafuta+ kutoka katika hema+ na akamutia Sulemani mafuta,+ na wakaanza kupiga baragumu, na watu wote wakaanza kusema kwa sauti kubwa: “Mufalme Sulemani aishi siku nyingi!” 40 Kisha watu wote wakamufuata na kupanda, wakipiga filimbi na kufurahi sana, na hivyo dunia ikapasuka na kufunguka kwa sababu ya makelele yao.+
41 Adoniya na wale wote wenye alialika wakasikia jambo hilo wakati walikuwa wamemaliza kula.+ Wakati tu Yoabu alisikia sauti ya baragumu, akasema: “Sababu gani kuko makelele hayo ya fujo katika muji?” 42 Wakati alikuwa angali anasema, Yonatani+ mwana wa Abiatari kuhani akakuja. Kisha Adoniya akasema: “Ingia, kwa maana wewe ni mwanaume muzuri,* na unapaswa kuleta habari njema.” 43 Lakini Yonatani akamujibu Adoniya: “Hapana! Bwana wetu Mufalme Daudi amefanya Sulemani kuwa mufalme. 44 Mufalme alituma pamoja naye Sadoki kuhani, Natani nabii, Benaya mwana wa Yehoyada, na Wakereti na Wapeleti, na wakamupandisha juu ya nyumbu wa mufalme.+ 45 Halafu Sadoki kuhani na Natani nabii wakamutia mafuta kuwa mufalme kule Gihoni. Kisha wakapanda kutoka kule wakifurahi, na muji uko katika fujo. Hayo ndiyo makelele yenye mulisikia. 46 Zaidi ya hayo, Sulemani amekaa kwenye kiti cha ufalme. 47 Jambo lingine, watumishi wa mufalme wameingia ili kumupongeza bwana wetu Mufalme Daudi, kwa kusema, ‘Mungu wako afanye jina la Sulemani likuwe na utukufu kuliko jina lako, na Yeye afanye kiti chake cha ufalme kikuwe kikubwa kuliko kiti chako cha ufalme!’ Kisha mufalme akainama kwenye kitanda. 48 Na pia mufalme alisema, ‘Yehova Mungu wa Israeli asifiwe, mwenye leo amechagua mutu wa kukaa kwenye kiti changu cha ufalme na ameruhusu macho yangu mwenyewe yaone jambo hilo!’”
49 Na wale wote wenye walialikwa na Adoniya wakaogopa sana, na kila mumoja wao akasimama na kuenda katika njia yake. 50 Adoniya aliogopa pia kwa sababu ya Sulemani, basi akaondoka na kuenda na akashika pembe za mazabahu.+ 51 Sulemani akaletewa habari hii: “Angalia, Adoniya ameogopa Mufalme Sulemani; na ameshika pembe za mazabahu, akisema, ‘Mufalme Sulemani aniapie kwanza kwamba hataua mutumishi wake kwa upanga.’” 52 Halafu Sulemani akasema: “Kama anatenda kwa njia yenye kufaa, hakuna hata unywele mumoja wa kichwa chake wenye utaanguka chini; lakini kama mambo ya mubaya yanapatikana ndani yake,+ atakufa.” 53 Basi Mufalme Sulemani akatuma watu wamushushe kutoka kwenye mazabahu. Halafu akaingia na kuinama mbele ya Mufalme Sulemani, kisha Sulemani akamuambia: “Uende kwenye nyumba yako.”