Cha Pili cha Wafalme
5 Sasa Naamani, mukubwa wa jeshi la mufalme wa Siria alikuwa mutu wa maana mwenye kuheshimiwa na bwana wake, kwa sababu kupitia yeye Yehova alikuwa amepatia Siria ushindi.* Alikuwa mupiganaji-vita mwenye nguvu, hata kama alikuwa na ukoma.* 2 Katika shambulizi lao moja, Wasiria walimukamata mateka mutoto mumoja mudogo mwanamuke kutoka inchi ya Israeli mwenye alifikia kuwa mutumishi wa bibi ya Naamani. 3 Ule mutoto mwanamuke alimuambia bimukubwa wake: “Ingekuwa muzuri kama bwana wangu angeenda kuona nabii+ katika Samaria! Basi angemuponyesha ukoma wake.”+ 4 Basi akaenda* na kumuelezea bwana wake na kumuambia mambo yenye ule mutoto mwanamuke wa Israeli alikuwa amesema.
5 Kisha mufalme wa Siria akasema: “Uende sasa! Na nitatuma barua kwa mufalme wa Israeli.” Basi akaenda, akabeba talanta* kumi (10) za feza, vipande elfu sita (6 000) vya zahabu, na nguo kumi za kubadilisha. 6 Akamupelekea mufalme wa Israeli barua hiyo, yenye kusema: “Pamoja na barua hii yenye umepata, ninatuma mutumishi wangu Naamani ili umuponyeshe ukoma wake.” 7 Wakati tu mufalme wa Israeli alisoma barua hiyo, alipasua nguo zake na kusema: “Je, mimi ni Mungu, ili niweze kuua ao kufanya mutu aendelee kuishi?+ Kwa maana anatuma mutu huyu kwangu, na kuniambia nimuponyeshe ukoma wake! Muone ninyi wenyewe kwamba anatafuta ugomvi na mimi.”
8 Lakini wakati Elisha mutu wa Mungu wa kweli alisikia kwamba mufalme wa Israeli amepasua nguo zake, mara moja akatuma ujumbe kwa mufalme: “Sababu gani ulipasua nguo zako? Tafazali, umuache akuje kwangu ili ajue kwamba kuko nabii katika Israeli.”+ 9 Basi Naamani akakuja na farasi wake na magari yake ya vita na akasimama kwenye muingilio wa nyumba ya Elisha. 10 Hata hivyo, Elisha akatuma mujumbe amuambie: “Uende, uoge mara saba (7)+ katika Yordani,+ na mwili wako utaponyeshwa, na wewe utakuwa safi.” 11 Halafu Naamani akakasirika na akaanza kuondoka, na kusema: “Angalia, nilisema katika moyo wangu, ‘Atatoka na kuja kwangu na atasimama hapa na ataitia jina la Yehova Mungu wake, akipitisha mukono wake mbele na nyuma juu ya ukoma ili auponyeshe.’ 12 Je, Abana na Farpari, mito ya Damasko,+ haiko muzuri kuliko maji yote ya Israeli? Je, siwezi kuoga mule na kuwa safi?” Basi akageuka na kuenda akiwa na kasirani kali.
13 Sasa watumishi wake wakamukaribia na kusema: “Baba yangu, kama nabii alikuambia ufanye jambo fulani lenye haliko la kawaida, je, haungelifanya? Namna gani basi hauwezi kufanya hata zaidi, kwa kuwa amekuambia tu, ‘Oga na ukuwe safi’?” 14 Halafu akashuka na kujitumbukiza* katika Yordani mara saba (7), kulingana na neno la mutu wa Mungu wa kweli.+ Kisha mwili wake ukaponyeshwa na kuwa kama mwili wa kijana mudogo,+ na akakuwa safi.+
15 Kisha akarudia kwa ule mutu wa Mungu wa kweli,+ yeye na wote wenye walikuwa pamoja naye,* na akasimama mbele yake na kusema: “Sasa ninajua kwamba hakuna Mungu mahali pengine popote katika dunia yote isipokuwa katika Israeli.+ Sasa, tafazali, kubali zawadi* kutoka kwa mutumishi wako.” 16 Hata hivyo, Elisha akasema: “Kama vile hakika Yehova anaishi mwenye ninatumikia,* sitaikubali.”+ Akamukaza aikubali, lakini akaendelea kukataa. 17 Mwishowe Naamani akasema: “Kama haiko vile, tafazali, acha mutumishi wako apewe kutoka katika inchi hii muzigo wa udongo wenye unaweza kubebwa na nyumbu wawili, kwa maana mutumishi wako hatatoa tena toleo la kuteketezwa ao zabihu kwa miungu mingine yoyote isipokuwa kwa Yehova. 18 Lakini Yehova asamehe mutumishi wako kwa jambo hili moja: Wakati bwana wangu anaingia katika nyumba ya* Rimoni ili kuinama ndani, yeye anaegemea kwenye mukono wangu, kwa hiyo ninalazimika kuinama kwenye nyumba ya Rimoni. Wakati nitakuwa ninainama kwenye nyumba ya Rimoni, tafazali, Yehova asamehe mutumishi wako kwa ajili ya jambo hilo.” 19 Basi Elisha akamuambia: “Uende kwa amani.” Wakati alikuwa ametoka kwake na kusafiri mbali kidogo, 20 Gehazi+ mutumishi wa Elisha mutu wa Mungu wa kweli+ akasema katika moyo wake: ‘Angalia, bwana wangu ameachilia huyu Musiria Naamani+ kwa kukataa kupokea vitu vyenye alileta. Kama vile hakika Yehova anaishi, nitakimbia na kumufuata na nitakamata kitu fulani kutoka kwake.’ 21 Kwa hiyo Gehazi akafuata mbio Naamani. Wakati Naamani alimuona mutu fulani akimufuata akiwa anakimbia, akashuka kutoka kwenye gari lake ili akutane naye na akasema: “Je, mambo yote ni sawa?” 22 Halafu akasema: “Mambo yote ni sawa. Bwana wangu amenituma, akisema, ‘Angalia! Sasa hivi vijana wawili kutoka eneo lenye milima la Efraimu kutoka kwa wana wa manabii wamekuja kwangu. Tafazali, uwapatie talanta moja ya feza na nguo mbili za kubadilisha.’”+ 23 Naamani akasema: “Sawa, kamata talanta mbili.” Akaendelea kumukaza,+ na akafunga talanta mbili za feza katika mifuko mbili, pamoja na nguo mbili za kubadilisha, na akavipatia watumishi wake wawili, na wakavibeba mbele yake.
24 Wakati alifika Ofeli,* akavikamata katika mukono wao na akavitia katika nyumba na akaacha watu hao waende. Kisha wao kuondoka, 25 akaingia na kusimama karibu na bwana wake. Sasa Elisha akamuambia: “Umetoka wapi, Gehazi?” Lakini akasema: “Mutumishi wako hakuenda mahali popote.”+ 26 Elisha akamuambia: “Je, moyo wangu haukukuwa pale pamoja na wewe wakati ule mutu alishuka kutoka kwenye gari lake ili kukutana na wewe? Je, huu ni wakati wa kukubali feza ao kukubali nguo ao mashamba ya mizeituni ao mashamba ya mizabibu ao kondoo ao ngombe ao watumishi wanaume ao watumishi wanamuke?+ 27 Sasa ukoma wa Naamani+ utashikamana na wewe pamoja na wazao wako milele.” Mara moja akatoka mbele yake akiwa na ukoma, mweupe kama teluji.*+