Cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati
10 Sasa Wafilisti walikuwa wanapigana na Israeli. Na watu wa Israeli wakakimbia kutoka mbele ya Wafilisti, na wengi wakaanguka wakiwa wameuawa kwenye Mulima Gilboa.+ 2 Wafilisti wakamukaribia sana Sauli na wana wake, na Wafilisti wakamupiga na kumuua Yonatani, Abinadabu, na Malki-shua,+ wana wa Sauli. 3 Pigano likakuwa kali sana juu ya Sauli, na wapiga-mishale wakamupata, na wapiga-mishale hao wakamuumiza.+ 4 Kisha Sauli akamuambia mubeba-silaha wake: “Chomoa upanga wako unitoboe nao, ili watu hawa wenye hawatahiriwe wasikuje na kunitendea bila huruma.”*+ Lakini mubeba-silaha wake hakutaka, kwa sababu aliogopa sana. Basi Sauli akakamata upanga na kuuangukia.+ 5 Wakati mubeba-silaha wake aliona kwamba Sauli amekufa, yeye pia akaangukia upanga wake mwenyewe na akakufa. 6 Basi Sauli na wana wake watatu (3) wakakufa, na watu wote wa nyumba yake wakakufa pamoja.+ 7 Wakati watu wote wa Israeli katika bonde* waliona kwamba kila mutu alikuwa amekimbia na kwamba Sauli na wana wake walikuwa wamekufa, wakaanza kuacha miji yao na kukimbia; kisha Wafilisti wakakuja na kukaa ndani.
8 Siku yenye ilifuata, wakati Wafilisti walikuja kuondoa vitu kwenye miili ya wale wenye waliuawa, walikuta Sauli na wana wake wakiwa wameanguka kwenye Mulima Gilboa.+ 9 Basi wakaondoa vitu kwenye mwili wake na kuondoa kichwa chake na silaha zake, na wakatuma ujumbe katika inchi yote ya Wafilisti ili kueneza habari hiyo kwa sanamu zao+ na kwa watu. 10 Kisha wakatia silaha zake katika nyumba ya* mungu wao na wakafungia mufupa wake wa kichwa kwenye nyumba ya Dagoni.+
11 Wakati watu wote wa Yabeshi+ katika Gileadi walisikia mambo yote yenye Wafilisti walikuwa wamemutendea Sauli,+ 12 wapiganaji-vita wote wakasimama na kubeba maiti ya Sauli na maiti za wana wake. Wakawaleta Yabeshi na kuzika mifupa yao chini ya muti mukubwa katika Yabeshi,+ na wakafunga kwa siku saba (7).
13 Basi Sauli akakufa kwa sababu ya ukosefu wa uaminifu wenye alionyesha kumuelekea Yehova kwa sababu hakutii neno la Yehova,+ pia kwa sababu ya kutafuta shauri kutoka kwa mutu mwenye kupashana habari na pepo wachafu+ 14 kuliko kumuuliza Yehova. Kwa hiyo Yeye akamuua na kumupatia Daudi mwana wa Yese ufalme.+