Cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati
14 Mufalme Hiramu+ wa Tiro alituma wajumbe kwa Daudi, pamoja na mbao za mierezi, mafundi wa kujenga kwa majiwe,* na wafanyakazi wa miti ili wamujengee Daudi nyumba.*+ 2 Na Daudi akajua kwamba Yehova alikuwa amemuweka imara kabisa kuwa mufalme juu ya Israeli,+ kwa maana ufalme wake ulikuwa umeinuliwa sana kwa ajili ya watu Wake Israeli.+
3 Daudi alichukua bibi wengine zaidi+ katika Yerusalemu, na Daudi akazaa watoto wanaume na watoto wanamuke wengine zaidi.+ 4 Haya ndiyo majina ya watoto wake wenye walizaliwa Yerusalemu:+ Shamua, Shobabu, Natani,+ Sulemani,+ 5 Ibhari, Elishua, Elpeleti, 6 Noga, Nefegi, Yafia, 7 Elishama, Beeliada, na Elifeleti.
8 Wakati Wafilisti walisikia kwamba Daudi alikuwa ametiwa mafuta kuwa mufalme juu ya Israeli wote,+ Wafilisti wote wakapanda kuja kumutafuta Daudi.+ Wakati Daudi alisikia jambo hilo, akaenda kupigana nao. 9 Kisha Wafilisti wakaingia na wakaendelea kufanya mashambulizi katika Bonde* la Refaimu.+ 10 Daudi akamuuliza Mungu, kwa kusema: “Je, nipande kuenda kupigana na Wafilisti? Je, utawatia katika mukono wangu?” Halafu Yehova akamuambia: “Panda uende, na hakika nitawatia katika mukono wako.”+ 11 Basi Daudi akapanda kuenda Baal-perasimu,+ na akawapiga na kuwaua kule. Halafu Daudi akasema: “Mungu wa kweli amepasua njia katikati ya maadui wangu kupitia mukono wangu, kama njia yenye kupasuliwa na maji.” Ndiyo sababu waliita mahali pale Baal-perasimu.* 12 Wafilisti wakaacha miungu yao pale, na wakati Daudi alitoa amri, miungu hiyo iliteketezwa katika moto.+
13 Kisha wakati fulani Wafilisti wakafanya tena shambulizi katika bonde.*+ 14 Daudi akamuuliza tena Mungu, lakini Mungu wa kweli akamuambia: “Usipande moja kwa moja kuwafuatilia. Lakini, uzunguke nyuma yao, na uwashambulie mbele ya miti midogo-midogo ya mibaka.+ 15 Na wakati utasikia sauti ya mwendo juu ya miti midogo-midogo ya mibaka, fanya shambulizi lako, kwa maana Mungu wa kweli atakuwa ametoka kuenda mbele yako ili kupiga na kuua jeshi la Wafilisti.”+ 16 Basi Daudi akafanya kama vile Mungu wa kweli alimuamuru,+ na wakapiga na kuua jeshi la Wafilisti kuanzia Gibeoni mupaka Gezeri.+ 17 Na sifa ya Daudi ikaenea katika inchi zote, na Yehova akatia woga wake juu ya mataifa yote.+