Cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati
25 Tena, Daudi na wakubwa wa vikundi vya utumishi waliweka pembeni wana fulani wa Asafu, Hemani, na Yedutuni+ ili watoe unabii wakiwa na vinubi, vyombo vya kamba,+ na matoazi.+ Haya ndiyo yalikuwa majina ya wanaume wenye vyeo wenye waliwekwa kwenye utumishi huo, 2 kati ya wana wa Asafu: Zakuri, Yosefu, Netania, na Asharela, wana wa Asafu wenye walikuwa chini ya uongozi wa Asafu, mwenye alitoa unabii chini ya uongozi wa mufalme. 3 Kutoka kwa Yedutuni,+ wana wa Yedutuni: Gedalia, Zeri, Yeshaya, Shimei, Hashabia, na Matitia,+ sita (6), chini ya uongozi wa Yedutuni baba yao, mwenye alitoa unabii akiwa na kinubi, akimushukuru na kumusifu Yehova.+ 4 Kutoka kwa Hemani,+ wana wa Hemani: Bukia, Matania, Uzieli, Shebueli, Yerimoti, Hanania, Hanani, Eliata, Gidalti, Romamti-ezeri, Yoshbekasha, Maloti, Hotiri, na Mahazioti. 5 Hao wote walikuwa wana wa Hemani, muonaji wa mufalme katika mambo yenye kuhusiana na Mungu wa kweli kwa ajili ya utukufu wake;* basi Mungu wa kweli alimupatia Hemani watoto wanaume kumi na ine (14) na watoto wanamuke watatu (3). 6 Hao wote walikuwa chini ya uongozi wa baba yao kwa ajili ya uimbaji kwenye nyumba ya Yehova, wakiwa na matoazi, vyombo vya kamba, na vinubi+ kwa ajili ya utumishi wa nyumba ya Mungu wa kweli.
Chini ya uongozi wa mufalme kulikuwa Asafu, Yedutuni, na Hemani.
7 Hesabu yao pamoja na ndugu zao wenye walizoezwa ili kumuimbia Yehova, wote wenye ujuzi, ilikuwa mia mbili makumi munane na munane (288). 8 Basi wakapiga kura+ kwa ajili ya kazi zao, mudogo sawa na mukubwa, mwenye ujuzi pamoja na mwanafunzi.
9 Kura ya kwanza kuanguka ilikuwa ya Asafu kwa ajili ya Yosefu,+ ya pili kwa ajili ya Gedalia+ (yeye na ndugu zake na wana wake walikuwa kumi na mbili [12]); 10 ya tatu (3) kwa ajili ya Zakuri,+ wana wake na ndugu zake, kumi na mbili (12); 11 ya ine (4) kwa ajili ya Izri, wana wake na ndugu zake, kumi na mbili (12); 12 ya tano (5) kwa ajili ya Netania,+ wana wake na ndugu zake, kumi na mbili (12); 13 ya sita (6) kwa ajili ya Bukia, wana wake na ndugu zake, kumi na mbili (12); 14 ya saba (7) kwa ajili ya Yesharela, wana wake na ndugu zake, kumi na mbili (12); 15 ya munane (8) kwa ajili ya Yeshaya, wana wake na ndugu zake, kumi na mbili (12); 16 ya kenda (9) kwa ajili ya Matania, wana wake na ndugu zake, kumi na mbili (12); 17 ya kumi (10) kwa ajili ya Shimei, wana wake na ndugu zake, kumi na mbili (12); 18 ya kumi na moja (11) kwa ajili ya Azareli, wana wake na ndugu zake, kumi na mbili (12); 19 ya kumi na mbili (12) kwa ajili ya Hashabia, wana wake na ndugu zake, kumi na mbili; 20 ya kumi na tatu (13), ya Shubaeli,+ wana wake na ndugu zake, kumi na mbili (12); 21 ya kumi na ine (14), ya Matitia, wana wake na ndugu zake, kumi na mbili (12); 22 ya kumi na tano (15), kwa ajili ya Yeremoti, wana wake na ndugu zake, kumi na mbili (12); 23 ya kumi na sita (16), kwa ajili ya Hanania, wana wake na ndugu zake, kumi na mbili (12); 24 ya kumi na saba (17), kwa ajili ya Yoshbekasha, wana wake na ndugu zake, kumi na mbili (12); 25 ya kumi na munane (18), kwa ajili ya Hanani, wana wake na ndugu zake, kumi na mbili (12); 26 ya kumi na kenda (19), kwa ajili ya Maloti, wana wake na ndugu zake, kumi na mbili (12); 27 ya makumi mbili (20), kwa ajili ya Eliata, wana wake na ndugu zake, kumi na mbili (12); 28 ya makumi mbili na moja (21), kwa ajili ya Hotiri, wana wake na ndugu zake, kumi na mbili (12); 29 ya makumi mbili na mbili (22), kwa ajili ya Gidalti,+ wana wake na ndugu zake, kumi na mbili (12); 30 ya makumi mbili na tatu (23), kwa ajili ya Mahazioti,+ wana wake na ndugu zake, kumi na mbili (12); 31 ya makumi mbili na ine (24), kwa ajili ya Romamti-ezeri,+ wana wake na ndugu zake, kumi na mbili (12).