Yobu
32 Basi wanaume hao watatu (3) wakaacha kujaribu kumujibu Yobu, kwa sababu alijiona kuwa mwenye haki.*+ 2 Lakini Elihu mwana wa Barakeli ule Mubuzi+ wa familia ya Ramu, alikuwa amekasirika sana. Kasirani yake iliwaka juu ya Yobu kwa sababu alijaribu kujionyesha kuwa mutu mwenye kufanya mambo yenye kuwa sawa pa nafasi ya Mungu.+ 3 Pia, alikasirikia sana marafiki watatu (3) wa Yobu kwa sababu hawakupata jibu lakini walikuwa wamemutangaza Mungu kuwa muovu.+ 4 Elihu alikuwa amengojea mbele ya kumujibu Yobu, kwa sababu walikuwa na miaka mingi kuliko yeye.+ 5 Wakati Elihu aliona kwamba wale wanaume watatu (3) hawakukuwa na neno la kujibu, kasirani yake ikawaka. 6 Kwa hiyo Elihu mwana wa Barakeli ule Mubuzi, akaanza kuzungumuza, na kusema:
Kwa hiyo, kwa heshima, nilijizuia,+
Na sikupima kuwaambia mambo yenye ninajua.
7 Niliwaza, ‘Acha miaka iseme,*
Na acha wingi wa miaka utangaze hekima.’
8 Lakini ni roho yenye kuwa ndani ya watu,
Pumuzi ya Mweza-Yote, ndiyo inawapatia uelewaji.+
9 Haiko kuishi miaka mingi tu ndiko kunamufanya* mutu akuwe na hekima,
Na haiko wazee peke yao ndio wanaelewa mambo yenye kuwa sawa.+
10 Kwa hiyo ninasema, ‘Munisikilize,
Na mimi pia nitawaambia mambo yenye ninajua.’
11 Muangalie! Nilingojea maneno yenu;
Niliendelea kusikiliza mawazo yenu+
Wakati mulikuwa munatafuta mambo ya kusema.+
12 Niliwasikiliza kwa uangalifu,
Lakini hakuna mutu katikati yenu mwenye aliweza kumuonyesha Yobu kosa lake*
Ao kujibu mawazo yake.
13 Kwa hiyo musiseme, ‘Tumepata hekima;
Mungu ndiye anamupinga, hapana mwanadamu.’
14 Yobu hakuelekeza maneno yake kwangu,
Kwa hiyo sitamujibu kwa kutumia mawazo yenu.
15 Wamekuwa na wasiwasi, hawana tena majibu;
Hawana tena neno la kusema.
16 Nimengojea, lakini hawaendelee kusema;
Wamesimama pale tu, bila neno lingine la kujibu.
17 Kwa hiyo mimi pia nitatoa jibu;
Mimi pia nitasema mambo yenye ninajua,
18 Kwa maana niko na maneno mengi;
Roho yenye kuwa ndani yangu inanisukuma.
19 Sehemu zangu za ndani ziko kama divai yenye haina nafasi ya kupitisha hewa,
Kama chupa mupya za ngozi za kuwekea divai zenye zinakaribia kupasuka.+
20 Acha niseme ili nipate kitulizo!
Nitafungua midomo yangu na kutoa jibu.